Mzalendo2015
JF-Expert Member
- Aug 14, 2012
- 6,697
- 9,048
Hayawi hayawi yamekuwa..!!!
Kile alichowahi kukitabiri au kukibashiri Baba wa Taifa hili Mwalimu J.K.Nyerere(rip) wakti wa uhai wake kuhusu DHAMBI YA UBAGUZI kimetimia. Baba Nyerere alisisitiza kuwa kama dhambi hiyo itafanywa na Watanzania wenyewe wawe ni wa upande mmoja wa Muungano iwe ni Bara au Visiwani basi dhambi hiyo haina budi kututafuna kama Taifa!!!! Hapa chini nimeweka Link ya Youtube ili tuweze kufuatilia maneno haya kwa pamoja.
Sauti ya Baba wa Taifa imekuwa ikichezwa mara kwa mara kwenye vipindi vya redio na TV zetu ikiwemo TBC, Uhuru FM(WOSIA WA BABA) za Serikali kila siku. Viongozi wa sasa wa Taifa hili akiwemo Rais John Pombe Magufuli wanasikia sauti hii lakini wameziba nta kwene masikio. Ubaguzi wa Kisiasa unaofanywa kwa sasa katika Utawala huu wa A5 unatisha. Kwa uchache tu hebu nikujuze aina ya Ubaguzi ambao kwa sasa umeshika kasi na umeanza kutishia maisha na uhai wa Watanzania kwa kiwango cha kutisha.
Kile alichowahi kukitabiri au kukibashiri Baba wa Taifa hili Mwalimu J.K.Nyerere(rip) wakti wa uhai wake kuhusu DHAMBI YA UBAGUZI kimetimia. Baba Nyerere alisisitiza kuwa kama dhambi hiyo itafanywa na Watanzania wenyewe wawe ni wa upande mmoja wa Muungano iwe ni Bara au Visiwani basi dhambi hiyo haina budi kututafuna kama Taifa!!!! Hapa chini nimeweka Link ya Youtube ili tuweze kufuatilia maneno haya kwa pamoja.
Sauti ya Baba wa Taifa imekuwa ikichezwa mara kwa mara kwenye vipindi vya redio na TV zetu ikiwemo TBC, Uhuru FM(WOSIA WA BABA) za Serikali kila siku. Viongozi wa sasa wa Taifa hili akiwemo Rais John Pombe Magufuli wanasikia sauti hii lakini wameziba nta kwene masikio. Ubaguzi wa Kisiasa unaofanywa kwa sasa katika Utawala huu wa A5 unatisha. Kwa uchache tu hebu nikujuze aina ya Ubaguzi ambao kwa sasa umeshika kasi na umeanza kutishia maisha na uhai wa Watanzania kwa kiwango cha kutisha.
- Kubaguliwa kwa Vyama vya siasa kwa kunyimwa haki ya kufanya siasa, kupiga na kupigiwa kura katika ngazi zote za Uchaguzi.
- Serikali kukataa kupeleka fedha za Maendeleo katika majimbo au maeneo yaliyo chini ya Upinzani hasa CHADEMA.
- Wabunge na Viongozi wa Upinzani kufanywa ni maadui kwa kukamatwa, kuteswa na kufunguliwa kesi za Uchochezi kila wanapotumia uhuru wao wa kujieleza.
- Kupigwa risasi hadharani, kuteswa na kupotezwa katika mazingira ya kutatanisha kwa kutumia watu ''wasiojulikana''.