- Thread starter
- #41
BSC Ltd
Nyie ni wafanyabiashara. Naomba niwashauri kitu kimoja. Msipoteze muda wenu kubishana na wafanyakazi na wanasiasa. Kusema ukweli watu wengi walioko JF ukileta idea ya business wako negative sana. Kuna watu wachache sana humu ndani wanaweza kuzifanyia kazi idea zinazoletwa hapa ndani.
Wafanyakazi wengi tumefundishwa shuleni kuwa bora kuwafanyia kazi wengine, lakini si kufanya kazi inayokupa uhuru wa kuamua mambo yako. Unaobishana nao wengi wao ni watu wa mwisho wa mwezi. Mtu wa biashara hana haja ya kuanza kupata justification hapa ndani, baada ya kupata hii info na address yenu angekuja directly hapo Shekilango kujithibitishia na kuijua vizuri hii biashara ili kama anaweza afanye au kama haiwezi basi. Lakini mnapoteza muda wenu kujibizana na "wrong target".
Ujumbe umefika wenye nia ya kujikomboa kutoka kutumia chini ya dola moja kwa siku na kugombea daladala kuwahi kwa mwajiri anayekulipa mpaka uandamane wataufanyia kazi. Wanaotaka kuendelea kukopa magari ya kutembelea na kuyalipia kwa miaka mitano huku wanaishi chumba kimoja cha kupanga watatoa pre-mature judgement kuwaita ninyi matapeli.
Mfano
Kuna bwana mmoja aliwahi kutoa idea ya kuuza LUKU kwa ZAP na MPESA hapa jamii siku za nyuma. Watu wengi sana walitoa critic hasi bila hata kufanyia kazi hiyo idea. Kuna baadhi najua walikata tamaa, wengine waliifanyia kazi. Mimi nilikuwa na cousin wangu anatafuta kazi nikamfanyia analysis ya hiyo biashara akaona inafaa, akaifungua pale manzese. Nakuambia ni mwezi umepita, ofisi moja tu ameweza kupata faida ya TZS 400,000 kwa mtaji mdogo sana. Sasa hivi anahangaika afungue ofisi nyingine buguruni na mbagala.
Ahsante sana kwa mawazo yako mazuri sana. Ntazingatia.