Woga wangu wa kuogopa kuoa.

Woga wangu wa kuogopa kuoa.

kwamtoro

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2010
Posts
4,922
Reaction score
3,244
Woga wangu wa kutokujua. nitakuwa na furaha? Nitapata ugumu? Nitashidwa?
Ni ukurasa mwingine mkubwa katika maisha yangu, sijui itakavyo kuwa. Nasikia ushauri na hadithi za waliopo kwenye ndoa na wale ambao walikuwepo sasa wapo njee ya ulingo, zinachanganya sana.

Woga mwingine ni wa kuoa mtu siyo sahihi katika maisha yangu. Kisha itazaliwa unhappy marriage. Hali hii itadumu mpaka siku ya kufa sababu katika akili yangu amna wazo la divorce. Wazo langu kubwa ni kuwa na ndoa ya furaha

Je mwana MMU, woga wako wa kuoa/kuolewa ni upi?




 
Woga wangu wa kutokujua. nitakuwa na furaha? Nitapata ugumu? Nitashidwa?
Ni ukurasa mwingine mkubwa katika maisha yangu, sijui itakavyo kuwa. Nasikia ushauri na hadithi za waliopo kwenye ndoa na wale ambao walikuwepo sasa wapo njee ya ulingo, zinachanganya sana.

Woga mwingine ni wa kuoa mtu siyo sahihi katika maisha yangu. Kisha itazaliwa unhappy marriage. Hali hii itadumu mpaka siku ya kufa sababu katika akili yangu Hamna wazo la divorce. Wazo langu kubwa ni kuwa na ndoa ya furaha

Je mwana MMU, woga wako wa kuoa/kuolewa ni upi?




Hapo pagumu sana inawezekana usipende ila ikabidi.
 
Tatizo vijana hamjiamini na kama umefika miaka 18 bado hujiamini hapa dunian kwamba unauwezo wa kupambana na jambo lolote juu ya maisha yako ujue ni hatari mfano bro wakati anaoa alitoa maneno makari sana mbele ya mchungaji na ndugu kwa ujumla,alisema me namuona huyu mwanamke ila akija kubadilika nikamkanja hakusikia nitaachana nae mala moja bila kujari mtu yoyote wala taasisi yoyote kwani mwanamke hawezi kunikosesha amani ndani ya maisha yangu ya hapa duniani.toka siku ndugu na jamaa wanamuona jamaa ni noma sana
 
mimi nahisi naogopa zaidi yako wewe...........au labda sijampata.....nachoogopa zaidi ni kupata stress kutokana na mke....namuomba Mungu yassije kunitokea.
 
nakumbuka ule usemi unaosema BORA UKOSEE KUJENGA NYUMBA KULIKO KUKOSEA KUOA!
pia ile tofauti ya complete na finish!
unapopata mwanamke mstaarabu,mwenye heshima na nidhamu umekuwa COMPLETELY! lakini unapompata mcharuko,mpenda pesa,asiyejiheshimu hapo umekuwa FINISHED!!
 
kwamtoro kinachokupa woga wala sio hicho cha kusikia fulani kaachika au fulani ndoa yake ina mgogoro au fulani yule kaoa ila kila siku mnakimbizana nae kwenye kutafuta mpango wa kando au fulani kaoa au kuolewa ila nyumba yake kila siku ina kelele ila kwako wewe ni ule woga wenyewe
nasema hivyo kwa sababu usilale mlango wazi kutegemea ndoa nzuri ya maelewano itakuja kama miujiza wala usitarajie mke mwema ambaye ana kila sababu ya kuitwa mke mwema atakuja tuu na usidhani kuwa mtakaa kwenye ndoa bila mkwaruzano au bila kutokea rabsha kidogo na ndoa yako itakuwa kama maji mtungini imetulia bila shida yoyote.

Ndoa ni wewe utakayeitengeneza ukiamua iwe mcharuko itakuwa na ukiamua itulie na mkae kwa amani na mke wako ndani ya nyumba itakua. na tegemea pia kutofautiana maana nyote mmelelewa katika mazingira tofauti kila mmoja amelelewa kivyake mnakutana ukubwani msitegemee kuwa kila kitu kitakuwa salama. Tofauti zipo muhimu ni kujaribu sasa kukutanisha tofauti zenu muunde kitu kipya na muishi kulingana na mazingira mapya ndoa yenu.
Kweli wengi wa waolewaji wamekuwa vituko wanataka waishi maisha ya kwenye movie ambayo kuhalisia na kwa mazingira yetu hayatawezekana ila ndo hivyo tunapambana kujiweka sawa ili mwolewaji asikute kweusi ila akutane na mwanga na maisha yanayofanana fanana na ya waigizaji wa Nolywood

Kingine kwamtoro oa kwa kuwa unajua nataka kufanya hivyo na usioe kwa shinikizo la fulani au kwa kuwa fulani kaoa na mimi ngoja nioe au wacha nioe niwaridhishe wazazi au ndugu au the whole world wasije wakadhania mimi sijakamilika
Oa kwa kuwa una furaha na unampenda na unamuona yule uliye nae yuko tayari kuolewa na sio kwa kuwa ni mzuri sana ukimwacha hutapata mwingine au unapenda sana mwendo wake au miguu yake au sura yake na hakuna wa kufanana nae ila oa kwa kuwa unahitaji kuoa
Sina woga wa ndoa na naifurahia sana ndoa na sija- regret kwa kufanya hivyo. (maelezo marefu sana samahani)
 
Last edited by a moderator:
Siogopi kuingia ktk ndoa koz kila ndoa ipo kipekee. Asikwambie mtu eti ndoa ndoano,kila mtu na ndoa yake na jinc atakavyoiendesha ndoa yake. Usiogope
 
Siogopi kuoa!
Nadhani sijampata anaestahili kuolewa!
Bado nipo ktk mchakato!
Najua mikwaruzano ni lazima itokee ktk ndoa!
...
Labda nikushauri tu!
Watu wanasema ndoa njema ni bahati! Mmmmh! Sipingi 1 kwa 1 ila sikubali 1 kwa 1!
Yap! Jitihadan wajada! Usisubiri Mungu akuchagulie na akuletee mke mwema!
 
Hongera kwa kuwa na woga wa kuingia maisha ya ndoa.watafiti wanasema ili kuyaingia maisha hayo kwa usahihi kuwa na woga kiasi ni jambo la muhimu sana.Wanasema kama unataka kuchukua hatua hiyo-kuoa/kuolewa nab hausikii woga kabisa kuna uwezekano ukakosea na kujuta baadae.Binafsi sijayaingia maisha hayo ila ninahofu kiasi na naamini itanisaidia.

Ushauri:usiruhusu woga wako upite kiasi kwa sababu hautakusaidia zaidi sana utakufunga na kukukosesha usifanye maamuzi sahihi,mwamini Mungu(kuwa na imani kwake) kwamba atakuongoza ufanye maamuzi sahihi kwa sababu ndie aliyekuleta duniani na hatopenda kukuona unajuta baadae.
 
Its part and parcel of life kijana! We all die at the end!
 
Utaogopa mpaka lini? We jilipue liwalo na liwe..........
 
Kitu chengine nyege zenyewe tu za siku hizi ni za kubahatatisha enzi za mababu husikii habari hizi Mara woga maratalaka hamukuelewana si uanacha tu sasa unafikiria nini
Tafuta mwanaume akuo basi
 
Maisha ni matamu sana kama utayapatia ukiwa hujaoa/olewa, utamu huo hutoweka pindi utapo oa/olewa. Endelea tu na woga wako ufurahie utamu wa maisha.
 
Back
Top Bottom