Wanajamii, jana jioni nilikuwa nikisikiliza idhaa ya Kiswahili ya BBC na kumsikia mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi-NEC akisema kwamba teknolojia ya kisasa itatumika kuhesabu kura za rais, yaani kura zikishahesabiwa vituoni, kutakuwa na mtu wa tume akiwa na laptop na connectivity katika database iliyopo NEC makao makuuili kutuma matokeo mara baada ya kuhesabiwa katika kituo cha kupigia kurakwa ajili ya compilation ya matokeo yote na kutangaza matokeo ya nchi nzima.Sasa wasiwasi wangu unakujakatika mambo yafuatayo:.....
Mwenye macho haambiwi tazama na biblia inasema kwamba "Kwa mtini,jifunzeni mfano"
Tumeshaona tume ya uchaguzi ilivyoharibu uchaguzi kwa Jirani zetu Kenya, pia tukumbuke jinsi George W. Bush alivyoshinda katika uchaguzi nchini Marekani!!! Kura ziliibiwa katika njia zinazoitwa za kisayansi.
Wito wangu kwa Vyama Makini- na hapa simaanishi CCM, NoNoNo, namaanisha vyama vinavyopigania uhuru wa kweli katika kumkomboa mtanzania view makini katika hili vya vilifuatilie kwa umakini sana.
Ni hayo tu.