Elections 2010 Wizi wa Kura unafanyika hivi...



Ndugu yangu tusije tukajidanganya kwamba kura zikishahesabiwa vituoni na mawakala wakapata kopi ndiomwisho wa mchezo. Kumbuka kwamba matokeo ya urais hayapingwi mahakamani kwahiyo tume ikichakachua na ikatangaza mshindi kinyume na matakwa ya wapiga kura hayo makaratasi ya vituoni hayatakuwa na maana yoyote. Hakuna namna hapa ni lazima vyama vijipange kucheza ngoma na NEC jino kwa jino, wakiwaachia nafasi kidogo tu wameumia. Hata Kenya mwaka 2007 mawakala walikuwa na makaratasi yao na baada ya ODM kufanya majumuisho wakakuta Raila ameshinda lakini kivuiti hakuona aibu kufanya uchakachuaji. Lazima kujua kila kitu kinachofanyika kuhusiana na kura zetu, lazima tuzilinde kura zetu kadri tunavyoweza kuanzia vituoni hadi nec.
 

Duh! Bora ungebaki kuhubiri yaliyoandikwa kwenye Biblia kama ulivyofanywa hapo mwisho kuliko kuandika haya ya laptop na "connectivity kwenye database". Mengine yote uliyoya-bullet ni matokeo ya kuchanganya technolojia ya "kuhesabu kura" na technolojia ya kutuma matokeo makao makuu. Ili mradi unajua buzz words za "connectivity", "route" na "database" basi ushakuwa mtaalamu wa haya mambo! Mweeee! :A S angry:
 

Yale yale ya buzz words! :doh:
 
Ukitaka kujua kuwa CCM kwa kutumia vibaraka wake wa Tume wamedhamiria kuiba kura msikilize Mwenyekiti alichosema kuhusu lini matokeo ya Urais yataanza kutangazwa eti kwa kisingizio cha nchi kuwa kubwa. Kama kweli watatumia digital tallying system, sioni sababu ya matokeo ya nchi nzima kutokuwa tayari kabla ya saa 12 asubuhi ya siku ya tarehe 1 Novemba. Kura zinahesabiwa kjatika vituo vya kupigia kura ambavyo vina wapiga kura wasiozidi 500. Kwa uelewa wangu, kura 500 za uraisi, kura 500 za ubunge na kura 500 za udiwani zinaweza kuhesabika ndani ya masaa 2 tu. wakishamaliza ni rahisi kutuma kwa sms matokeo kwenye makao makuu ya jimbo (tallying center). Hawa wakishapokea wanaziingiza kwenye mtambo wa kujumulishia na wakati huo huo zinaanza kuonekana makao makuu ya Tume (central tallying system). Kwa hiyo hata kama vituo viko remote kiasi gani, kama mtandao unafanya kazi vizuri, hakuna sababu ya kusubiri kuanza kutoa matokeo hadi siku ya tatu.

Hawa wanania ya kuchakachua matokeo kwa kusingizia umbali. Ninawasihi CHADEMA na CUF wateue watu makini na wasitegemee kuwa kile kilichomo kwenye masanduku ndicho kinachotangazwa. Tuige kutoka Kenya vitu vichache. Kule inasemekana kuwa ilipoundwa Tume ya kuchunguza kilichoendelea katika uchaguzi, ilidhihirika kuwa katika masanduku yote yaliyofunguliwa hakuna ambalo idadi ya kura ililingana na idadi ya kura zilizotangazwa na Tume ya Uchaguzi. Vilevile hata zile karatasi za kuhesabia kura ujumlishaji ulifanywa kimakosa katika majimbo karibu yote waliyoamua kuyafanyia uchunguzi. Kwahiyo ni vizuri Wakala wakasisitiza kupatiwa nakala ya kura kama walivyozihesabu na wawe na tallying centers zao kuhakikisha kuwa kura walizopata katika kila jimbo ndizo zinazotangazwa. Ikitokea vinginevyo wafanye haraka kuzuia kutangazwa matokeo ili hesabu zifanyike upya ikibidi masanduku yote yahesabiwe upya.

Mawakala wasiwepo mle ndani kama mapambo. Masanduku yanapaswa kuwa transparent na yenye serial nambaz ambazo zinafuatana ili kuondoa uwezekano wa masanduku mengine kuwekwa badala ya yale yaliyotumika. Ingawa kuna uwezekano wa masanduku bandia kutengenezwa na kuwekwa serial numberz zilezile, si vibaya kuchukua tahadhari, labda hawana akili kama hizo. Lingine ambalo nadhani limefanywa makusudi ni hili la Mwema jana kusema kuwa baada ya kupiga kura watu warejee majumbani kwao na wasubiri matokeo kwenye vyombo vya habari. Kwani utaratibu wa zamani wa kuwa mita mia toka vituo vya kuhesabia kura au kupigia kura una ubaya gani? Kweli hii siyo janja ya kuleta mamluki wapige kura au kuleta masanduku yenye kura tayari?

This is just an eye opener kwa wale wenye kutaka matokeo ya haki. CCM mwaka huu wana hali mbaya, lakini hata system haijakuwa tayari kwa mageuzi. Watafanya kila wawezalo kuzuia utashi wa wananchi. Hii ni kawaida ya serikali yoyote fisadi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…