Elections 2010 Wizi wa Kura unafanyika hivi...

Jun 13, 2010
22
1
Wizi wa kura unaanza na Tume ya Uchaguzi inapotangaza idadi ya wapiga kura waliosajiliwa. Katika idadi hii kunakuwa na pasenti kubwa ya WAPIGA KURA HEWA. Hawa wapiga kura hewa watatumika kujaza mapengo pale mgombea wa CCM atakapoonekana kuelemewa.

Ili kutumia hizi kura feki wanakuwa pia na VITUO VYA KUPIGA KURA FEKI ambavyo vinakuwa na masanduku ya kupiga kura kama yaliyoko kwenye vituo vya kweli.

Hizi kura zinapigwa kisirisiri largely na usalama wa taifa na kuwekwa kwenye haya masanduku ya vituo hewa siku kadhaa kabla ya uchaguzi.

Mawakala wa uchaguzi wanasimamia kura katika vituo halali tu na hivyo vingine vilivyo feki of course hawana habari navyo. Kwa hiyo matokeo ya kura wanayoyafahamu mawakala ni yale ya vituo waliko tu na hata haya yanaweza kukumbwa na matatizo ya

(i) orodha ya wapiga kura kuwa na majina kibao ya wapiga kura hewa na watu kuandaliwa kuja kupiga kura kwa niaba ya hayo majina bandia,
(ii) kura zao kuweko kwenye masanduku kabla ya kupiga kura au
(iii) watu walioandaliwa kutumbukiza bulunguti la kura kwenye sanduku.

Kura kadhaa zimeshapatikana kwenye masanduku zikiwa zimeshikamana kwa njia ambayo ni wazi kuwa zimetumbukizwa na mtu mmoja. Tatizo hili laweza kupunguzwa, ijapokuwa siyo kumalizwa, kwa kutumia masanduku yalio transparent lakini nasikia masanduku hayatakuwa hivyo.

Tume ya uchaguzi ndiyo inayoruhusu haya yote yatokee na ndiyo inayojumlisha kura na kutangaza matokeo na jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa ni wazi kuwa waliyoitayarisha hiyo sheria walikuwa na dhamira ya kuwezesha wizi wa kura na kutumia Tume kuhalalisha wizi huo.

Kutumia wakurugenzi wa Halmashauri kama wasimamizi wa uchaguzi majimboni ni nyenzo kubwa ya kufanikisha haya kwani wakurugenzi wote wanateuliwa na Rais directly au indirectly na Waziri wa TAMISEMI na you can be sure that they are all loyal members of CCM. Mambo mengine kama kuwarubuni mawakala wa vyama vingine au kuwahonga wagombea wajitoe dakika za mwisho ni mwendelezo tu wa msingi huu wa kuwaibia wananchi haki yao ya kuchagua viongozi wao.

Kwa jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa, Tume ya Uchaguzi inaweza kumtangaza mgombea ambaye actually amepata kura chache kuwa mshindi na kutoa namba tu zanazodai kuwa huyu kashinda kwa kura nyingi ijapokuwa si hivyo.

Wizi wa kura uliofanyika Iran na Afganistan kwenye chaguzi zao za mwisho ni mifano mizuri ya kuwafumbua macho Watanzania kuhusu tatizo hili.

Huwezi kuiba hela uache kuiba kura, and vice versa!
 
Nguchiro, usemayo ni kweli kabisa. Nimeshuhudia haya katika chaguzi ndogo mbili:

BUSANDA: Rafiki yangu aliye ndani kabisa ya mikakati ya wizi wa kura katika CCM alinipigia simu usiku siku hiyo kuwa wamezidiwa kuwa kidogo lakini wanajiandaa "kwenda chumba cha ndani, na kufikia asubuhi hali itabadilika".

BIHARAMULO: Rafiki huyo huyo akanipigia simu saa 2 usiku na kusema Chadema wanaongoza na vimebaki vituo vinne "ambavyo haviwezi kubadili tofauti iliyopo". Mnamo saa 7 usiku akaniandikia txt message ikisema, "tunaingia chumba cha ndani, usiwe na wasiwasi, kufikia asubuhi mambo yatanyoka".

Kwa sababu sababu baadhi ya mafundi hao wamehamia upinzani ni vema Chadema wakaanza tangu LEO kuandaa check list ya mbinu za wizi wa kura. Nawatajia chache, nyingine wani-PM nisaidie:

1. Wawepo watu tangu sasa, kuhakiki idadi wa wapiga kura kati ya TEC na majimbo
2. Wahakiki physically vituo vya kupigia kura na idadi ya wapiga kura
3. Wahakiki vyumba vilivyomo ndani ya ukumbi na ikibidi wawe na UWT yao

ANGALIZO: Naomba niwe kama Shehe Yahya: Kama kutatokea vita katika taifa letu, itatokana na wizi wa kura. It is a matter of few selfless individuals kuchukua live bullets, then, CCM watakaa chini kijadili muafaka maana wanajua kuwa watakuwa wameiba. It has happened in Zanzibar, Kenya, Zimbabwe, Malawi and others.

Nasikitika kuyasema haya, MUNGU NISAIDIE.
 
ANGALIZO: Naomba niwe kama Shehe Yahya: Kama kutatokea vita katika taifa letu, itatokana na wizi wa kura. It is a matter of few selfless individuals kuchukua live bullets, then, CCM watakaa chini kijadili muafaka maana wanajua kuwa watakuwa wameiba. It has happened in Zanzibar, Kenya, Zimbabwe, Malawi and others.

Nasikitika kuyasema haya, MUNGU NISAIDIE.

Mimi naona woga wetu ndio unatuponza. CCM wanalijua hilo na ndio maana michezo ya kijinga kama hiyo haifanyiki maeneo ya wazee wa kazi kama Tarime. Nadhani muda si mrefu Tarime itaanza kuenea nchi nzima kwani CCM hawawezi kuendelea kutufanya wajinga milele.
 
Inatia moyo kuona bado kuna mashujaa wengi Tanzania. Watanzania kama wale wa Tarime hawawezi kunyanganywa UHURU wao. Tunasali ili hiyo hali ya kujitolea kutetea haki ya wananchi kuchagua viongozi wao iwaingie Watanzania wengi zaidi.

Hakuna ubishi kwamba CCM wanaiba kura. Mbinu zao zinafunuliwa, na hilo litasaidia.

There are no free lunches. Freedom costs.
 
Katika hili mawakala wawe makini na kura za kila kituo.

Zaidi kila chama hususan Chadema tuwe na Timu ya watu makini wakujumuisha kura za vituo vyote Tanzania pindi zinapotangazwa. Mawakala wetu wakiwa waaminifu hii ni rahisi. Kwani mawakala wa kila kituo watatoa matokeo yao sahihi na Timu ya chama itapata matokeo hayo. Hata kabla Tume haijatangaza.

Hiyo itarahisisha kufumania hizo kura feki za Tume ya uchaguzi ambao wana mpango wa kuwabeba CCM na ufisadi wao.
 
Vizuri hii kitu imekuwa bayana lakini maadamu imekuwa bayana basi angalizo kwetu.
Baija Bolobi katoa sehemu ya ufumbuzi.
 
Katika hili mawakala wawe makini na kura za kila kituo.

Zaidi kila chama hususan Chadema tuwe na Timu ya watu makini wakujumuisha kura za vituo vyote Tanzania pindi zinapotangazwa. Mawakala wetu wakiwa waaminifu hii ni rahisi. Kwani mawakala wa kila kituo watatoa matokeo yao sahihi na Timu ya chama itapata matokeo hayo. Hata kabla Tume haijatangaza.

Hiyo itarahisisha kufumania hizo kura feki za Tume ya uchaguzi ambao wana mpango wa kuwabeba CCM na ufisadi wao.

Ila mkakati wa kuthibiti vituo feki utakuwaje? Na kazi ya kuhakiki vituo inafanyikaje? Tume ya Uchaguzi ya Tanzania haiaminiki.
 
Katika hili mawakala wawe makini na kura za kila kituo.

Zaidi kila chama hususan Chadema tuwe na Timu ya watu makini wakujumuisha kura za vituo vyote Tanzania pindi zinapotangazwa. Mawakala wetu wakiwa waaminifu hii ni rahisi. Kwani mawakala wa kila kituo watatoa matokeo yao sahihi na Timu ya chama itapata matokeo hayo. Hata kabla Tume haijatangaza.

Hiyo itarahisisha kufumania hizo kura feki za Tume ya uchaguzi ambao wana mpango wa kuwabeba CCM na ufisadi wao.

Zaidi ya hiyo ni lazima Chadema na vyama vingine vya upinzani wawaambie wananchi na viongozi wenye tabia ya kuiba kura kuwa mwaka huu kura zikiibiwa Tutaingia Msituni na kuanzisha VITA vya Kuiondoa CCM kwa nguvu. Hili litakuwa ni tishio kwa wale wenye tabia mbovu, so wajue wakiiba na kudhulumu mtu basi matatizo yatawajia wao, na watakuwa wakimbizi! Wakati mwingine Matishio yanasaidia....ndio mana Mchungaji wa Marekani hakuchoma KURAN! Tutumie mbinu hii!
 
Wizi wa kura unaanza na Tume ya Uchaguzi inapotangaza idadi ya wapiga kura waliosajiliwa. Katika idadi hii kunakuwa na pasenti kubwa ya WAPIGA KURA HEWA. Hawa wapiga kura hewa watatumika kujaza mapengo pale mgombea wa CCM atakapoonekana kuelemewa.

Ili kutumia hizi kura feki wanakuwa pia na VITUO VYA KUPIGA KURA FEKI ambavyo vinakuwa na masanduku ya kupiga kura kama yaliyoko kwenye vituo vya kweli.

Hizi kura zinapigwa kisirisiri largely na usalama wa taifa na kuwekwa kwenye haya masanduku ya vituo hewa siku kadhaa kabla ya uchaguzi.

Mawakala wa uchaguzi wanasimamia kura katika vituo halali tu na hivyo vingine vilivyo feki of course hawana habari navyo. Kwa hiyo matokeo ya kura wanayoyafahamu mawakala ni yale ya vituo waliko tu na hata haya yanaweza kukumbwa na matatizo ya

(i) orodha ya wapiga kura kuwa na majina kibao ya wapiga kura hewa na watu kuandaliwa kuja kupiga kura kwa niaba ya hayo majina bandia,
(ii) kura zao kuweko kwenye masanduku kabla ya kupiga kura au
(iii) watu walioandaliwa kutumbukiza bulunguti la kura kwenye sanduku.

Kura kadhaa zimeshapatikana kwenye masanduku zikiwa zimeshikamana kwa njia ambayo ni wazi kuwa zimetumbukizwa na mtu mmoja. Tatizo hili laweza kupunguzwa, ijapokuwa siyo kumalizwa, kwa kutumia masanduku yalio transparent lakini nasikia masanduku hayatakuwa hivyo.

Tume ya uchaguzi ndiyo inayoruhusu haya yote yatokee na ndiyo inayojumlisha kura na kutangaza matokeo na jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa ni wazi kuwa waliyoitayarisha hiyo sheria walikuwa na dhamira ya kuwezesha wizi wa kura na kutumia Tume kuhalalisha wizi huo.

Kutumia wakurugenzi wa Halmashauri kama wasimamizi wa uchaguzi majimboni ni nyenzo kubwa ya kufanikisha haya kwani wakurugenzi wote wanateuliwa na Rais directly au indirectly na Waziri wa TAMISEMI na you can be sure that they are all loyal members of CCM. Mambo mengine kama kuwarubuni mawakala wa vyama vingine au kuwahonga wagombea wajitoe dakika za mwisho ni mwendelezo tu wa msingi huu wa kuwaibia wananchi haki yao ya kuchagua viongozi wao.

Kwa jinsi sheria ya uchaguzi ilivyoandikwa, Tume ya Uchaguzi inaweza kumtangaza mgombea ambaye actually amepata kura chache kuwa mshindi na kutoa namba tu zanazodai kuwa huyu kashinda kwa kura nyingi ijapokuwa si hivyo.

Wizi wa kura uliofanyika Iran na Afganistan kwenye chaguzi zao za mwisho ni mifano mizuri ya kuwafumbua macho Watanzania kuhusu tatizo hili.

Ndio maana likatiba letu la nchi linasema NEC wakitangaza tu matokeo ya urais hakuna mahakama yeyote inayoweza kushughulikia malalamiko kuhusu matokeo hayo! 1995 DTV walitangaza CUF kushinda kule Z'bar na ZEC kutangaza CCM! Ni wizi mtupu na ushenzi!!
 
Ndio maana likatiba letu la nchi linasema NEC wakitangaza tu matokeo ya urais hakuna mahakama yeyote inayoweza kushughulikia malalamiko kuhusu matokeo hayo! 1995 DTV walitangaza CUF kushinda kule Z'bar na ZEC kutangaza CCM! Ni wizi mtupu na ushenzi!!

Itabidi tuanze kuwatupia mimacho hao NEC tangu sasa. Hivi list yao ni ipi? Ni wangapi? Maana inaelekea watu hawa ndio kila wakati wamechagua nani anashinda. Yaani kupiga kura kunaweza kuwa ni danganya toto tu.

Zama za chama kimoja alikuwa Chief Adam Sapi anatangaza kura za ndio ni ngapi na za hapana ni ngapi. Basi. Hukukuweko na uhakiki wowote.

Kuna uwakilishi wa vyama vyote huko NEC? Maana wale wa mwanzo walikuwa ni wa CCM. Itakuwaje kama kura anapata huyo lakini mshindi anakuwa yule? Maana haya mambo inabidi kuyafikiria kabla ya siku ya uchaguzi kufika.
 
Solution hapa ni transparent ballot boxes na pia NEC iweke hadharani vituo vyote vya kupiga kura viko wapi. Hawawezi kuja baadaye na kusema kuwa kuna vituo vya siri. Pia ushirikiano ni hakuna kwani vyombo vya habari vingekuwa vina wawakilishi wao kila kituo ktk unagalia kile kinachoendelea na kukiripoti.

Kenya walifanya hivi wakati Kibaki anagombania na ndio maana ikawa ngumu kuibwa kwani majibu yalikuwa yanatangazwa pao hapo na yanarushwa kwenye TV moja kwa moja na updates zinatolewa mara kwa mara. Tatizo ni kuwa hata baahdi ya wahandishi wenyewe wamekosa maadili ya taaluma yao ukitoa kutokuwa na uwezo wa kuchanganua mambo ya kila upande iwe siasa, michezo au biashara, n.k. Baada ya uchaguzi huu wananchi wawe mstari wa mbele kuomba NEC ivunjwe na iwe inapitiswa na Bunge kwa kushirikiana na vyama vyote vya kisiasa vilivyopo.

Hii itasaidia sana maana malalamiko yatakuwa machache, pia vyama vya siasa vipendekeze watu wao ili wawe members wa NEC Mpya. Hapo uwizi utakuwa umepunguzwa kwa kiasi fulani kwani kila member atakuwa loyal kwa chama chake na hawezi kukubali ujinga huo wa kutangaza matokeo yaliyogeuzwa hata iweje.
 
Katika moja ya mada zangu siku chache zilizopita nilighusia taarifa kuwa tayari kura zimeshapigwa.

Nilidokeza kuwepo kwa makontena matatu yaliyokuwa na vifaa vya kupigia kura kupelekwa mahali pasikofahamika badala ya bohari kuu ya taifa.

Nakubaliana na mleta mada hii kuwa kura feki hutayarishwa mapema kabla ya siku ya kupiga kura na maeneo ambayo kwa vyovyote vile ccm hawatarajiwi kushinda kama vile Kigoma kask, Tarime, Moshi, Hai, Karatu ..nk, kura feki zitapenyezwa ili kuuthibitishia ulimwengu kuwa nguvu za upinzani hasa CHADEMA ni za soda hivyo kuhalalisha wizi wa maeneo mengine.

Ni vema wote kwa pamoja tukawa macho kwa kutoa taarifa za kufichua mbinu zozote chafu kuelekea siku ya kupiga kura 31/10.
 
Ndiyo maana Jakaya kasema tayari ana kura za kushinda kwa kishindo! Na ndiyo maana hajali kama hatapata kura za wafanyakazi, wala wanafunzi, wala walimu, wala wakulima wa korosho, pamba, kahawa, mahindi, maharage, mihogo, n.k., wala wafugaji, wala wafanyabiashara wadogo na wa kati, wala wamachinga ... kwani tayari anazo kura za kutosha kushinda kwa kishindo?
 
Hapa ndo linakuja suala la mtandao. CCM wanatumia vyombo vya serikali ambavyo vina watu wanaolipwa mshahara ambao wanakuwa very loyal kwa waajiri wao kwani ajira ni ya kudumu.

Hizi mbinu zinajulikana sana, lakini ajabu ni kuwa mbinu hizi hizi zinatumika kila wakati. Tatizo si kuzijua, tatizo ni uwezo wa kupambana nazo na financial resources zitakazotumika kupambana na mbinu hizi. It is almost impossible.

Kuna kuweka mawakala feki sehemu ambazo upinzani ni dhaifu hasa huko vijijini. Takwimu zinaweza kukorogwa kirahisi. Maeneo ambayo mawakala wa upinzani ni watu wasio nakipato cha kutosha, ni rahisi kuwapa rushwa! Hiyo imetokea kwenye kura za maoni ya CCM kwa mawakala kununuliwa live, sasa sioni kwa nini CCM washindwe kufanya hivyo pale watakapoona upinzani ni tishio kwao.

Kuna enclaves ambazo wanazoa maelf ya kura ingawa response ya wananchi kupiga kura ni ndogo sana.

Kwa hiyo mbinu hizi zitaendelea kutumiwa miaka nenda miaka rudi. Njia pekee ni ya kupambana navyo ni vyama vya upinzani (chochote kitakachoweza) kuwa na watendaji wa kuajiriwa kila kijiji (nao wanaweza kununuliwa, ila ni vigumu kidogo kuliko hali ilivyo sasa hivi).

Kuna watu wengi huko vijijini wanajua huu huwa ni msimu wa mavuno kwao. Kwa hiyo sasa hivi watajitambulisha na vyama vya siasa ili waukwae uwakala na waweze kushiriki kwenye bonanza ya rushwa inayofuatana na uchaguzi. Wamekuwa wakifanya hivi miaka yote na watafanya hivyo mwaka huu na wataendelea kufanya hivyo mpaka hapo tutakapostaarabika na kuanza kutumia information technology kudhibiti uchafu huo.

Ni bahati mbaya sana, lakini hali huwa hivi. Sehemu ambazo wananchi wanaamua kukataa kushiriki uchafu huo ni chache sana. Mara nyingi unakuta ni mtu mmoja mmoja hapa na pale. Lakini walio wengi walioko kwenye huu mfumo wanashiriki. Fedha ya kumwaga kuwapa rushwa hawa watu inapokosekana au kupungua ndo mara nyingi matokeo yanakuwa yanayo akisi uchaguzi halisi. Kwa hivyo kuna sababu kubwa sana ya kudhibiti mzunguko wa fedha. Lakini kwa nchi kama Tanzania ambapo mtu unaweza kwenda benki leo unafungua account na kujaza mamilioni, na kuyatoa kesho bila kuulizwa ni vigumu kudhibiti utoaji hongo.

Lakin wizi huwa ni rampant kuliko tunavyofikiria.
 
Kwani nchi nyingine zimeweza vipi? kwa nini Tanzania ishindwe??

Wananchi wasimamie kura zao...

Kuna majimbo kura zinaibwa bila kificho, mpaka hata mgombea mwenyewe inaonyesha hajajipigia kura.... huu ni wendawazimu...

Kura zihesabiwe vituoni na ziwasilishwe kwa njia ya simu direct kwa vyombo vya habari
 
Mimi naona woga wetu ndio unatuponza. CCM wanalijua hilo na ndio maana michezo ya kijinga kama hiyo haifanyiki maeneo ya wazee wa kazi kama Tarime. Nadhani muda si mrefu Tarime itaanza kuenea nchi nzima kwani CCM hawawezi kuendelea kutufanya wajinga milele.

Tarime wazee wa kazi wale hawana masihara. Walicheleweshewa matokeo wakati wa uchaguzi mdogo kura zilikuwa zinataka kupigwa. Walivyochoka kusubiria matokeo wakaambizana wakasema "MRA, TUNAKAA KUSUBHIRHI NINI WAKATI TUNAJUA TUMEMCHAGUA NANI, TWENDENI NYUMBANI HALAFU KAMA KUNA MWANAUME HAPA ATANGAZE MATOKEO TOFAUTI NA YALE TUNAYOYAJUA", thubutu, kura hazikuibiwa tena na matokeo yalitangazwa kama yalivyokuwa.

Hao waache tu ni wanaume wa shoka mi nawakubali mno!
 
Kwani nchi nyingine zimeweza vipi? kwa nini Tanzania ishindwe??

Wananchi wasimamie kura zao...

Kuna majimbo kura zinaibwa bila kificho, mpaka hata mgombea mwenyewe inaonyesha hajajipigia kura.... huu ni wendawazimu...

Kura zihesabiwe vituoni na ziwasilishwe kwa njia ya simu direct kwa vyombo vya habari

Askofu;
Mi nakushangaa kidogo, kawaida sisi huwa tunaweza kufanya vile ambavyo wengine hawawezi, na hatuwezi kufanya vile ambayo wengine wanaweza!
 
Back
Top Bottom