Wizi kupitia mitandao ya simu

Wizi kupitia mitandao ya simu

Pablo

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2017
Posts
2,441
Reaction score
2,547
Sehemu ya Kwanza

Habari,
Tafadhari usivuke bila kusoma uzi huu ni muhimu hata kama sio kwako bali itasaidia watu wako wa karibu. Leo nimeona niweke wazi ni jinsi gani matapeli wanavyozidi kuwaliza ndugu zetu kupitia mitandao ya simu.

Takribani miezi 6 sasa wizi huu umeshamili na unakua siku hadi siku, nitoe angalizo tu uzi huu hauna nia ya kuelezea uzaifu wa mitandao ambayo wateja wake wanaongoza kuibiwa kwa kuwa mitandao yetu ina strong security ya kutosha katika kukabiliana na mianya ya wizi kupitia mitandao bali uzi huu ni kuweka wazi ili kama una ndugu yako usambaze ujumbe huu awe makini asije lia kilio cha maumivu na kisichokuwa na ukomo maana akishajua ameibiwa ataomba dunia ipasuke atumbukie ndani.

Wateja wanaoongoza kuibiwa ni wateja wa 075,076,074....nazani mnanielewa kwa hizo code.. ipo hivi matapeli hawa humpigia mteja simu na kujitambulisha wanatokea huduma kwa wateja wa mtandao husika na kumtaarifu ushindi wa zawadi au "bonus" neno linalotumika mara kwa mara na huenda mbali zaidi kwa kumuuliza maswali machache kuhusu salio lake muda huo na mteja akiuliza kwanini mnauliza salio langu wakati ninyi mpo mtandaoni mnaona salio nililonalo matepeli hujibu kwamba tunataka kuwa na uhakika kama wewe ni mmiliki wa simu hii tukumie "bonus" yako.

Baada ya mteja kutaja kiasi cha salio lake mfano Sh.895,000/= matapeli humtaka mteja atafute simu nyingine kisha atume ujumbe mfupi "sms" neno ZAWADI kwenda kwenye namba ya hao matapeli. mteja akishatuma sms hupigiwa kwenye hiyo simu aliyotuma sms na kuambiwa achukue simu yake na kufuata maelezo atayopewa hapa ndo utapeli unapoanzia.......

Mteja huambiwa apige menu ya pesa ya mtandao husika yaani *150*00# nazani mnajua code hii mnaielewa ni mtandao gani kisha kuambiwa achague kipengele cha tuma pesa mteja hushtuka kama anaibiwa kwa hayo maelezo lakini huambiwa kuna code zitatumwa kwahiyo akifika mbele akipata hizo code awasomee ili wamtumie bonus yake.

Mteja huamini na kufuata hatua ambayo itampa hizo code ili apokee bonus yake kisha Mteja huambiwa achague kutuma pesa kwenda mitandao mingine na hapa ndo ujanja na akili za matapeli hawa hutumika kuliza ndugu zetu.

Mteja ataambiwa aandike namba za bahati kwenye kipengele cha kuweka namba (ukiwa unatuma pesa) mfano wa namba zinazotumiwa mara kwa mara ni 654321456 usipokuwa makini huwezi jua hizo code ni namba ya simu ya mtandao flan.

Haijawekwa 0 tu hapo mwanzo lakini mtandao hutambua hiyo namba na kuruhusu muamala. Kwa kuwa mteja hajui ni namba ya simu huaminishwa kuwa kuna masage itakuja na code hivyo asonge mbele, baada ya kuweka namba hufuatia kipengele cha kuweka kiasi (nazani wote tunafahamu hatua hii) hapa matapeli humwambia mteja aweke code nyingine ambazo ni 00892111 ( juu nimeweka mfano wa kiasi kinachotapeliwa) mteja bado haamini kama anatepeliwa kwa kuwa kwa macho na fikla za kawaida tu huwezi jua kama hiyo ni 892,111/=Tsh.

Hatua inayofuata ni weka namba ya siri, mteja anauliza mboni namba ya siri? Hujibiwa kuna masage itakuja ututajie ili tukupe bonus yako na mteja huingiza namba ya siri na kuruhusu muamala....Dah masage inayofuata ndio humtoa mteja gizani

"imethibitishwa umetuma Tsh 892,111 kwenda namba 654321456 risiti namba 4HGY32Gl"

Kisha tapeli hukata simu na huwa hawaizimi kwa kuwa wanajua utakuwa ukipoteza muda kuwapigia na wao bila kupokea na huku alietumiwa pesa akiitoa bila wasiwasi wowote, mteja akiona jamaa hapokei simu huamua kupiga simu huduma kwa wateja wa mtandao wake na kwa kuwa ametuma pesa kwenda mtandao mwingine huduma kwa wateja hawana access ya kuzuia isitolewe na humshauri apige mtandao alikotuma. Akipiga kule huambiwa pesa imeshatolewa. Kilio kinachofuatia ni cha maumivu na kusaga meno.

My take :
Kuwa makini wezi hawa wanambinu nyingi sana na soon ntaweka hapa njia nyingine zinazotumiwa na hawa wezi wa mitandao kuliza ndugu zetu.

Ninawashukuru voda na airtel ambao ukipiga namba 100 huduma kwa wateja wanakupa taarifa za wizi huu kupitia maelezo ya awali, kwa kiasi flani wamefanikiwa kupunguza japo siyo kumaliza kabisa tatizo.

Wakuu.nawasilisha.


Sehemu ya pili.

Habari wadau ...! juzi kati nilipost juu ya wizi unaoliza ndugu zetu kila kukicha kupitia mitandao ya simu.

Sehemu hii ntaonyesha ni jinsi gani wezi hutumia akili ama mteja huibiwa kijinga kwa kutokujua kupitia mawakala wausajiri (freelancer) fake au wasio waaminifu.

Ipo hivi upo nyumbani kwako umetulia sebureni ukipiga stor na wife au kucheki kideo mda si punde wanapita mawakala wa mtandao wowote(tigo,voda,aitel n.k n.k) wakijifanya wanasajiri laini,kusajiri huduma za nivushe,m-pawa, timiza au kukamilisha sajiri za laini ya mitandao husika, ukiwa mmoja wa wanaohitaji huduma kati ya hizo unawaita na kuwaeleza shida yako na wao watakuomba utoe laini yako uwape ili waweke kwenye simu yao kwa kuwa lazima watumie simu yao ya kazi ili kukuhudumia. Tuchukulie mfano. Mteja anahitaji kusajiliwa m-pawa ya vodacom, msajiri huchukua laini ya mteja na kuiweka kwenye simu yake ya usajiri na kujifanya anasajiri. Itafika kipindi atakupa simu uweke namba ya siri ili kukamilisha usajiri wako. Pasipo kujua kama wakala usajiri ameingia katika menu ya m-pesa na kufuata hatua zote za kutuma pesa na kinachosubiriwa ni namba ya siri ili kuruhusu muamala. Mteja ataingiza namba ya siri na kumrudishia wakala usajiri aendelee na zoezi kumbuka ukiweka neno siri namba hubakia zilivyo (hazifichiki). My friend kama una laki tano au milioni zote zitahamishwa na sms zote zitafutwa muda huo huo ili kuficha ushahidi, kumbuka huwa wanauliza salio la mpesa ili kukuhakikishia huduma ya m-pawa kukamilika. Wakala huenda mbali zaidi na kubadili namba ya siri ya mteja kisha kumwambia kuwa zoezi limekamilika baada ya saa 24 m-pawa itakuwa active ili mteja aendelee kutumia. Mwisho huomba malipo ya huduma na kutokomea. Mteja akija kushtuka ni pale anapo fanya muamala na majibu huambiwa namba ya siri sio sahihi Akipiga simu huduma kwa wateja atapewa taarifa ya fedha zake kuhamishwa na upande wa pili umeshatoa hizo pesa. Kinachofuatia ni kilio kwa uchungu sababu ya kutokujua au uzembe

My take: tuwakumbushe watumiaji wa mitandao hii kuwa makini kwa kuwa kila kukicha mbinu zina badilika na wizi unashamili kila iitwapo leo. Next time ntaweka sehemu ya tatu kuhusu mawakala wa tigopesa, airtel money au m-pesa wanavyolizwa na kupoteza mitaji yao .


Asante
emoji112.png
 
Asante sanaaa mkuu na huu wizi hufanywa hasaa kwenye tigo pesa na m pesaa wanacheza sanaa ba akili za watu na details zote huwa zinatoka kwa hao jamaa wa IT kutoka mitandao nimetaja hapo juu....
 
Mimi washanipigia mara mbili. Mara ya kwanza sikuwa na salio, wakataka niweke 50,000 ndio nipate sms ya ushindi, nami nikatafakari kwanza nikaona wao ndio akili zao hazina akili.

Mara ya pili alipoanza tu kunipa story za kishinda nikamuuliza inakuwaje mnatumia namba ya kawaida kama yangu wakati nimezoea nikipigiwa na mtandao namba inakuwa fupi sana au inaanza na 009.... Kilichofuata akakata simu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vodacom Tanzania mshachua hatua gani kuwadhibiti hawa jamaa wanaoumiza wateja wenu au mnasubiri Rais aseme ndio mchukue hatua.
Wameanza chukua hatua mkuu. Nmeeleza hapo jui. Ukipiga 100 unakutana na sauti inayo kutahadharisha juu ya wizi huu.

sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Vodacom Tanzania mshachua hatua gani kuwadhibiti hawa jamaa wanaoumiza wateja wenu au mnasubiri Rais aseme ndio mchukue hatua.
Kwa hili sioni hapo kampuni za simu zinaingiaje lawamani...sanasana wanachoweza kufanya wao labda ni kutoa tu tahadhari.

Ukiwa makini huwezi kuingia kwenye mitego kama hii....kama ni bonus kwa nini upewe maelezo meengi ya kuipata, ili hali hata voda wakitaka kutuma yale magawiwo yao ya M pesa, Mtu unapokea tu ujumbe na salio bila kutakiwa kufanya chochote, sasa Mtu akupe maelezo mareefu na wewe unafuatisha tu....hapo unastahili kuibiwa tu hakuna namna.

Wizi ambao ningewalaumu Makampuni ni kama from no where unakuta salio limepungua ili hali wewe hujafanya muamala wowote.
 
Tatizo nilionalo hapo ni kukosa maarifa ya hivi vitu...
Kitendo cha kupokea simu inayokuambia kwamba umeshinda bahati nasibu kwa mchezo ambao haujashiriki ni lazima uwe very carefully na kuwaignore baada ya kusikiliza masharti yao.
Bonus huwa inatumwa tu wala haitaji mlolongp wote huo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Elimu elimu elimu
Hivi kweli mtu unaona kabisa unabonyeza codes za M-PESA kisha unachagua namba moja tuma pesa hushtuki tu? Njaa hizi zitatuua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wizi unafanyika na hasaaa ukiwa mteja mpyaaa na ukiweka hela haipiti mda wanakupigia simu hawaa jamaa hawafai hata kidogo je tujiulize details wanapata wapi hasaaaaa naomba vodaa muwe makini na wafanyakazi wenu maana hao ndio wanaharibu biashara.....

Kuna siku walinipigia nikafata maelezo yote kila mahali mpaka nafikia kuweka pin kwa sababu nilishajuwa hii game then nikamuuliza jamaa ina maana unataka niweke pin hizi hela zitaenda kwa mama yako au baba yako??

Jamaa akakasilika na kukata simu pale pale...
 
Nilishawahi kutoa tahadhari kuhusiana na hawa matapeli na kuna no niliituma huku,jamaa walinipigia na kujitambulisha ni voda huduma kwa wateja,alipoanza kunipa maelekezo yake nikamuuliza una uhakika unafanya kazi voda

d671d3606f5aec3790f96dd095a0fefe.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa walitaka kunipiga nikawaambia kama hamna taarifa zangu siwezi kuwatajia salio wala kufanya chochote.

Baadae siku mbili zilizofuata, nikapigiwa simu na voda huduma kwa wateja nimeshinda nogesha upendo 1M. Ealipoanza tu nikawaambia naenda kushtaki polisi, jamaa akashangaa mbona sifurahii. Nilipokata nikapiga 100 kuwaeleza kuandamwa na matapeli, wakasema wangenipigia baada ya dakika tano, kweli walinipigia na kunihakikishia nimeshinda siku hiyo na pesa yangu itawekwa kwa Mpesa ndani ya masaa 24. Kweli kwenye saa tisa alasiri nikapokea unumbe imethibitishwa.....nikahamisha huo mpunga kwanza kabla hawajafanya vitu vyao, nilikua siamini bado...kwa mara ya kwanza nikaamini kwamba haya mambo yapo.

Ila inabidi hatua zichukuliwe kupambana na hawa wahalifu tukizingatia kwamba namba zote zimesajiliwa.
 
Nilishawahi kutoa tahadhari kuhusiana na hawa matapeli na kuna no niliituma huku,jamaa walinipigia na kujitambulisha ni voda huduma kwa wateja,alipoanza kunipa maelekezo yake nikamuuliza una uhakika unafanya kazi voda

d671d3606f5aec3790f96dd095a0fefe.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa wezi hata jina haliji utaona ujumbe tu "unatuma Tsh 00895211 kwenda 652456325 bonyeza 1 kuthibitisha au 2 kubatilisha" sasa cyo rahisi kujua hizo namba na hizo pesa na by that time jamaa wanakwambia wahi kuthibitisha isije ku cancel na wateja wanathibitisha fasta. Dah aseee afu ni watu wajinga na wengine wenye akili zao timamu kabisa wanaibiwa.

sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Unaweza ona kama masihara vile, lakini kuna watu wanaibiwa kipuuzi puuzi sana
Yaani wastani wateja 25 wanaibiwa kwa siku tena ni zaid ya 5M inapotea kila siku kwa utapeli huu.. Wanatia hasira hawa watu..nina hasira nao kinyama

sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Wizi unafanyika na hasaaa ukiwa mteja mpyaaa na ukiweka hela haipiti mda wanakupigia simu hawaa jamaa hawafai hata kidogo je tujiulize details wanapata wapi hasaaaaa naomba vodaa muwe makini na wafanyakazi wenu maana hao ndio wanaharibu biashara.....

Kuna siku walinipigia nikafata maelezo yote kila mahali mpaka nafikia kuweka pin kwa sababu nilishajuwa hii game then nikamuuliza jamaa ina maana unataka niweke pin hizi hela zitaenda kwa mama yako au baba yako??

Jamaa akakasilika na kukata simu pale pale...
Wewe una bahati uliijua game mapema.

sent from my iPhone 7s using JamiiForum mobile app.
 
Back
Top Bottom