Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Hivi karibuni kumekuwa na mfululizo wa mabenki kuibiwa fedha na wafanyakazi wake. Mara chache matukio haya yamekuwa yanaripotia. Mabenki huyafanya taarifa hizi kuwa siri ili kutoondoa imani kwa wateja wake.
Binafsi nimekuwa nikijiuliza nini kinamsukuma mfanyakazi kuliibia shirika lake. Baada ya kujipa muda wa kutosha na kufanya Utafiti Kidogo nimegundua sehemu kuu ya tatizo hili. Nitaitumia Benki ya standard Chartered kama case study.
Benki ya Standard Chartered imekumbwa na udokozi mfululizo; kuanzia mwishoni wa 2008 na mwanzoni mwa mwaka huu. Katika kila udokozi pesa iliyoibiwa ni US$ isiyopungua elfu 30. Wizi huu umekuwa ukifanywa na wafanyakazi. Kama nilivyoeleza awali, lengo langu ni kujua kwa nini mfanyakazi aliibie shirika lake na akubali kupoteza ajira yake, heshima yake kwa kupelekwa mahakamani, kuonekana kwenye luninga, n.k. Katika study yangu nimebaini jambo moja kuu ambalo kwa sentensi moja linaitwa: MATUMIZI MABOVU YA RASILIMALI WATU (Poor Human Resource Management). Ukichunguza zaidi kuchimba mzizi huu utabaini mengi sana miongoni mwao ni:
Madhara ya matatizo hayo hapo juu:
Wizi au sema udokozi katika Benki hii unachangiwa na wafanyakazi kutothaminiwa. Hali hii inasababisha wao kutoridhika na kazi waliyonayo na baadhi wanaona suluhu ni kuiba $ ambazo ni rahisi kuchukua nyingi kwa mkupuo. Binafsi siliungi mkono jambo hili na ndiyo maana najaribu kusoma chanzo cha mfanyakazi kukata tawi alilokalia.
Matukio ya wizi yanapokuwa mfululizo katika benki, wateja hukosa imani na benki husika. Hata kama benki hulipa fidia kwa mteja lakini taswira yake kaika jamii hubadilika.
Madhara mengine yanayoweza benki ni wimbi la kuacha kazi au kuhama kwa wafanyakazi wazoefu. Na hata kama ikiajiri wengine, bila kutafuta chanzo cha wizi na wafanyakazi kuhama na kutafuta ufumbuzi, mzimu huu utaendelea hata kwa wajao.
Kama itakuwa inaajiri watu wapya kila mara na wanaondoka, Benki itapoteza pesa nyingi katika Human Recruitment and Training. Pia ufanisi utazorota zaidi maana waajiriwa wengi watakuwa wageni na utamaduni wa benki hii.
Nini cha kufanya:
Kwa HR-Manager mwenye macho ya kusoma, ubongo wa kutafakali kweli na isiyo kweli na kama amejaliwa sikio la kusikia atafanya hatua zinazostahili. Miongoni mwao ni kuwapanga wafanyakazi katika nafasi ambazo wamesomea na wanaweza kuzimudu vema. Hatua hii lazima iende sambamba na kuwabadilishia maslahi.
Njia ya kuwatathmini wafanyakazi kwa kupitia Wasimamizi wao sio nzuri sana. Maana kama msimamizi ana shuki binafsi na mfanyakazi aliye chini yake, kwa nadra sana atamtendea haki. Ni vema kutumia njia nyingine. Kwa mfano: katika ufanisi unaweza kumpima mfanyakazi kwa kigezo cha Idadi ya slips alizoprocess kwa muhula, na katika umakini unaweza kuangalia rekodi ya DIFF alizopata mfanyakazi katika muhula.
Jayen,
Mteja wa SCB,
Tanzania
Binafsi nimekuwa nikijiuliza nini kinamsukuma mfanyakazi kuliibia shirika lake. Baada ya kujipa muda wa kutosha na kufanya Utafiti Kidogo nimegundua sehemu kuu ya tatizo hili. Nitaitumia Benki ya standard Chartered kama case study.
Benki ya Standard Chartered imekumbwa na udokozi mfululizo; kuanzia mwishoni wa 2008 na mwanzoni mwa mwaka huu. Katika kila udokozi pesa iliyoibiwa ni US$ isiyopungua elfu 30. Wizi huu umekuwa ukifanywa na wafanyakazi. Kama nilivyoeleza awali, lengo langu ni kujua kwa nini mfanyakazi aliibie shirika lake na akubali kupoteza ajira yake, heshima yake kwa kupelekwa mahakamani, kuonekana kwenye luninga, n.k. Katika study yangu nimebaini jambo moja kuu ambalo kwa sentensi moja linaitwa: MATUMIZI MABOVU YA RASILIMALI WATU (Poor Human Resource Management). Ukichunguza zaidi kuchimba mzizi huu utabaini mengi sana miongoni mwao ni:
- 2
- 3
- 4
- 5
Madhara ya matatizo hayo hapo juu:
Wizi au sema udokozi katika Benki hii unachangiwa na wafanyakazi kutothaminiwa. Hali hii inasababisha wao kutoridhika na kazi waliyonayo na baadhi wanaona suluhu ni kuiba $ ambazo ni rahisi kuchukua nyingi kwa mkupuo. Binafsi siliungi mkono jambo hili na ndiyo maana najaribu kusoma chanzo cha mfanyakazi kukata tawi alilokalia.
Matukio ya wizi yanapokuwa mfululizo katika benki, wateja hukosa imani na benki husika. Hata kama benki hulipa fidia kwa mteja lakini taswira yake kaika jamii hubadilika.
Madhara mengine yanayoweza benki ni wimbi la kuacha kazi au kuhama kwa wafanyakazi wazoefu. Na hata kama ikiajiri wengine, bila kutafuta chanzo cha wizi na wafanyakazi kuhama na kutafuta ufumbuzi, mzimu huu utaendelea hata kwa wajao.
Kama itakuwa inaajiri watu wapya kila mara na wanaondoka, Benki itapoteza pesa nyingi katika Human Recruitment and Training. Pia ufanisi utazorota zaidi maana waajiriwa wengi watakuwa wageni na utamaduni wa benki hii.
Nini cha kufanya:
Kwa HR-Manager mwenye macho ya kusoma, ubongo wa kutafakali kweli na isiyo kweli na kama amejaliwa sikio la kusikia atafanya hatua zinazostahili. Miongoni mwao ni kuwapanga wafanyakazi katika nafasi ambazo wamesomea na wanaweza kuzimudu vema. Hatua hii lazima iende sambamba na kuwabadilishia maslahi.
Njia ya kuwatathmini wafanyakazi kwa kupitia Wasimamizi wao sio nzuri sana. Maana kama msimamizi ana shuki binafsi na mfanyakazi aliye chini yake, kwa nadra sana atamtendea haki. Ni vema kutumia njia nyingine. Kwa mfano: katika ufanisi unaweza kumpima mfanyakazi kwa kigezo cha Idadi ya slips alizoprocess kwa muhula, na katika umakini unaweza kuangalia rekodi ya DIFF alizopata mfanyakazi katika muhula.
Jayen,
Mteja wa SCB,
Tanzania