Wizara ya kilimo mnatia aibu

Wizara ya kilimo mnatia aibu

MVB Jr

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2016
Posts
489
Reaction score
1,554
Bagamoyo_Crops_Suitability_Map.jpg


Wakuu hii ni ramani ya bagamoyo inayoonyesha mgawanyiko wa hali ya udongo na umahsusi wa udongo kwa ajili ya uzalishaji wa kundi fulani la mazao.

Hii ramani ni moja kati ya nyingi zilizoandaliwa na wizara ya kilimo kama rasilimali kwa taifa na kuwa uploaded kwenye website yao kwa minajili ya kutaarifa umma wa watanzania na wakimataifa juu ya hali ya udongo katika maeneo mbalimbali ya nchi na ubora wa udongo kwa ajili ya uzalishaji wa kundi fulani la mazao.

Cha ajabu hizi ramani hazina ubora kabisa, ukizingatia funguo za baadhi ya ramani kusomeka kwa shida sana au kutosomeka kabisa. Picha hizi zipo kichoyo sana, kupelekea niamini walilazimishwa kuziupload na bahati mbaya aliyewalazimisha hakuhakiki utekelezaji wake..!

Binafsi nitoe wito kwa wizara ya kilimo kuzirekebisha hizi ramani, maana hii ni rasilimali nyeti na yenye maslahi mapana kwa taifa na jamii ya kimataifa kwa ujumla. Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia ni aibu kama wizara kupandisha taarifa isiyo na ubora kama rasilimali.

Nawasilisha.
 
Kweli aisee,hizo ramani za wizara ya kilimo ni za hovyo kabisaa!!
 
Hilo ni kweli na linipa shida sana wakati nipo shule....naamini watalishughulikia ila wizara inatia aibu kwa kweli
 
Bagamoyo_Crops_Suitability_Map.jpg


Wakuu hii ni ramani ya bagamoyo inayoonyesha mgawanyiko wa hali ya udongo na umahsusi wa udongo kwa ajili ya uzalishaji wa kundi fulani la mazao.

Hii ramani ni moja kati ya nyingi zilizoandaliwa na wizara ya kilimo kama rasilimali kwa taifa na kuwa uploaded kwenye website yao kwa minajili ya kutaarifa umma wa watanzania na wakimataifa juu ya hali ya udongo katika maeneo mbalimbali ya nchi na ubora wa udongo kwa ajili ya uzalishaji wa kundi fulani la mazao.

Cha ajabu hizi ramani hazina ubora kabisa, ukizingatia funguo za baadhi ya ramani kusomeka kwa shida sana au kutosomeka kabisa. Picha hizi zipo kichoyo sana, kupelekea niamini walilazimishwa kuziupload na bahati mbaya aliyewalazimisha hakuhakiki utekelezaji wake..!

Binafsi nitoe wito kwa wizara ya kilimo kuzirekebisha hizi ramani, maana hii ni rasilimali nyeti na yenye maslahi mapana kwa taifa na jamii ya kimataifa kwa ujumla. Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia ni aibu kama wizara kupandisha taarifa isiyo na ubora kama rasilimali.

Nawasilisha.

Nakupongeza sana mkuu kwa kuliona hili, wizara hii ni miongoni mwa wizara za ovyo kweli kweli. Ina wasomi wengi sana wenye elimu kubwa hadi PhD na MSc lakini hata ukiangalia miundombinu ya majengo ya taasisi zake zinasikitisha sana, huezi amini kwamba ndani ya majengo haya kuna watu wenye elimu kubwa vile. Hivyo mimi sishangai kuwa na taarifa duni kwenye web yao. Kituo cha Utafiti wa kilimo cha Mlingano, Tanga ndio hutoa hizo ramani inawezekana hawakiwezeshi maana nilipita pale mwezi julai 2017 mazingira yake yamechoka kipo hoi. kama wapo humu wakubwa wa wizara jirekebisheni.
 
Tena mmesahu kama form four failure ambao hata vyeti hawakaguliwi wanalipwa posho 300,000/= kwa mwezi plus nyumba, maji na umeme BURE. Sasa mwenye MSc. Ana anapata udhalendo wapi?
 
Back
Top Bottom