Wizara ya Afya: Taarifa kwa umma kuhusu ugonjwa wa homa ya Dengue

Hakuna dengue wala ndugu yake dengue. Hizi ni mbinu tu za magamba za kutaka kuchota mabilioni ya pesa chini ya mwavuli wa dengue. Ccm kuweni na huruma na wananchi.


Mleta maada kwa taarifa yako hakuna dengue ila ni janja ya Magambawakishirikiana na baadhi ya madaktari wehu wanaokubali hujuma kwa taifa. Hata kwa mtu ambaye hajaenda shule atanielewa hapa. Mbu wa dengue ati ni Sharobaro hapendi maji machafu- only Magamba wanaweza kuthibitisha hili kwana wanajua Dar maeneo mengi maji ni machafu na wagonjwa wangukuwa wengi sana kama ni kweli. Mbu hao ndo waliingia hivi karibuni tu wakati wako miaka na miaka na watu hawaugui? lingine ni kwamba, ati tiba ni panado, mara dengue ni virusi na mengineyo. Dengue ni mtaji wa Magamba na ni ugonjwa hewa wa kuibia fedha za kuhonga kwani uchaguzi umewadia.
 
huu ugonjwa wa dengue ulivuma sana ila kitu kilichonipa wasiwasi sana wagonjwa wa ugonjwa walikuwa ni wasanii wa bongomovies wale wanajua ukweli dengue ilikuwa inshu ya kutengenezwa na serikali ya ccm kwa ajili ya kunufaisha wachache ugonjwa gani umevuma kwa muda mwenzi mmoja mpaka leo kimya ..serikali ya ccm imetufanya sisi wananchi ni wajinga kwa kudanganywa kwa kila kitu wana JFtuambiane ukweli hii serikali ya ccm inatuonaje??
 
800px-Dengue_fever_symptoms.svg.png


KWA UFUPI
Ni taarifa ya wizara baada kutokea mlipuko huo mapema mwaka huu.


Dar es Salaam. Kasi ya kuenea kwa homa ya dengue hapa nchini imepungua baada ya taarifa kuonyesha kuwa hakuna mgonjwa mpya kuanzia Julai 15.

Dk Vida Mmbaga, mtaalamu wa Kitengo cha Epidemiolojia cha Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, alisema kasi ya kuenea kwa ugonjwa huo ambao umeathiri watu 1384, inaendelea kupungua.

Alisema hadi sasa hakuna mgonjwa aliyelazwa wala kubainika kuwa virusi vya ugonjwa huo.

Alisema asilimia kubwa ya wananchi waliokumbwa na dengue walitoka Dar es Salaam, huku Wilaya ya kinondoni ikiongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi, ikifuatiwa na Ilala na Temeke.

"Mlipuko wa ugonjwa huu japo ulianza Februari, ulishika kasi Mei, lakini Juni ulianza kupungua kutokana na juhudi zilizowekwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali," alisema Dk Vida.

Alisema hii ni mara ya tatu kwa homa ya dengue kuibuka nchini. Mara ya kwanza ilikuwa Julai 2010, Juni 2013 na mwaka huu ambao umesababisha madhara zaidi.

Aliwata wananchi kuendelea kufuata kanuni za afya, ikiwa ni pamoja na kuangamiza mazalia ya mbu wanaoeneza magonjwa mengine.

Pia aliwataka kuendelea kwenda vituo vya afya kwa ajili ya vipimo kila wanapohisi dalili za homa.

Pia alishauri watu kuachana na tabia ya kutumia dawa bila ushauri wa kitaalamu.

Dk Vida alisema tangu kutokea kwa ugonjwa huo ni watu wanne tu kutoka Dar es Salaam waliopoteza maisha.chanzo.Hakuna mgonjwa mpya wa dengue - Kitaifa - mwananchi.co.tz




800px-Aedes_aegypti_feeding.jpg





 
Ugonjwa huu ulitanganzwa kwa namna ya pekee,hasa viongozi wetu wa serikali na baadhi ya Madaktari wetu.

Na tulisikia kuwa uliua Watanzania wenzetu. Swali langu,huu ugonjwa umeishia wapi?.

Kwa nini hawajatuambia dawa waliotumia kuutokomeza maana tunashukuru kama wameutokomeza kabisa.

Wasipotuambia tunaibua maswali mengi mojawapo ni au lilikuwa ni dili tu.

Maana kuna semina nyingi yawezekana zilifanywa na wizara ya afya.

Na inawezekana kabisa serikali ilitoa fungu kubwa. Je, hizo pesa zilienda wapi kama fungu lilitoka?
 
Sasa hivi wamehamia Ebola ,wamemkamata jamaa wa watu na kumzushia ana Ebola ,na kusabisha hospitali ya Temeke watu kuikimbia hospitali ni tupu ,watu wanaogopa hata kushika ukuta wa hospitali.
 
Ugonjwa huu ulitanganzwa kwa namna ya pekee,hasa viongozi wetu wa serikali na baadhi ya Madaktari wetu. Na tulisikia kuwa uliua Watanzania wenzetu. Swali langu,huu ugonjwa umeishia wapi?.

Kwa nini hawajatuambia dawa waliotumia kuutokomeza maana tunashukuru kama wameutokomeza kabisa. Wasipotuambia tunaibua maswali mengi mojawapo ni au lilikuwa ni dili tu. Maana kuna semina nyingi yawezekana zilifanywa na wizara ya afya. Na inawezekana kabisa serikali ilitoa fungu kubwa. Je, hizo pesa zilienda wapi kama fungu lilitoka?

Walizusha tu kuzima agenda muhimu za nchi
 
dengue ilikuwa ni noma kama kweli ilikuwa ni zengwe kweli nimeamini hakuna mtu anayejali maisha ya mwingine
 
Dengue ni ugonjwa wa msimu subiri masika ijayo.
Kwa hiyo masika tu yakianza tutegemee dengue?, mbona masika yapo miaka yote ya nyuma na dengue hatujaiona,au malaria kali ndo dengue maana wasije kuwa walituchanganya tu.
 
Wewe unaongelea Dengue wakati wenzio wamebuni mradi mwingine almaarufu EBOLA. mafisadi huwawezi. Hapa watapiga hela ndefu kuliko dengue
 
Serikali ilitangaza tangia tar 16 June hawakupata taarifa ya maambukizi mapya baada ya Dr. cheni na ray c kula mafungu yao! Ungonjwa bado hupo coz serikali bado haijatangaza kama umepungua au kwisha kabisa.
 
Back
Top Bottom