CHA The GREAT
JF-Expert Member
- Nov 11, 2010
- 651
- 854
Kama Mtanzania na kama raia wengine wa taifa hili ninayo haki kikatiba ya kutoa maoni kuhusu jambo lolote linalohusu jamii yangu kwa maslahi mapana ya taifa. Kwa hivyo basi, napenda kuchukua nafasi hii kutoa wito wangu ili mjadala kuhusu fao la kujitoa uanzishwe kwa kushirikisha wadau muhimu katika suala hili.
Itakumbukwa kwamba, mwezi Februari, 2018 kulikuwa na mjadala kuhusu marekebisho ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambapo fao la kujitoa lilikuwa sehemu ya mjadala huo. Hadi mwisho wa siku, maamuzi yalifuta utaratibu wa fao la kujitoa.
Kwa nini natoa wito kwa jambo hili?
Tangu wakati wa mjadala huo hadi hivi sasa baada ya muswada huo kupitishwa na bunge kwa kufuta fao la kujitoa, kumekuwa na maoni ambayo yanakinzana na maamuzi ya kufutwa fao la kujitoa. Tuliambiwa kwamba, vyama vya wafanyakazi vilishirikishwa katika hatua muhimu za jambo hili hadi kufika hapa lilipo. Ila ukiuliza maoni ya wengi ambao kimsingi ndiyo wenye fedha hizo kwenye mifuko ya jamii, utagundua kuwa, maoni yao hayakufanyiwa kazi au yalipuuzwa, kitu ambacho kwa mtazamo wangu haikuwa sahihi. Kwa hali hii, hata kama vyama vya wafanyakazi vilishirikishwa, basi havikuwasilisha maoni sahihi na halisi, au matakwa na mapendekezo ya wafanyakazi ambao ndiyo wenye fedha hizo. Kwa sababu hii, kuna umuhimu wa kuanzisha mjadala mpana utakaowashirikisha wadau wote muhimu kwa maana ya wafanyakazi moja kwa moja, na wengineo ili mwisho wa siku kila mmoja aondoke akiwa karidhika.
Nawasilisha.
Itakumbukwa kwamba, mwezi Februari, 2018 kulikuwa na mjadala kuhusu marekebisho ya sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii ambapo fao la kujitoa lilikuwa sehemu ya mjadala huo. Hadi mwisho wa siku, maamuzi yalifuta utaratibu wa fao la kujitoa.
Kwa nini natoa wito kwa jambo hili?
Tangu wakati wa mjadala huo hadi hivi sasa baada ya muswada huo kupitishwa na bunge kwa kufuta fao la kujitoa, kumekuwa na maoni ambayo yanakinzana na maamuzi ya kufutwa fao la kujitoa. Tuliambiwa kwamba, vyama vya wafanyakazi vilishirikishwa katika hatua muhimu za jambo hili hadi kufika hapa lilipo. Ila ukiuliza maoni ya wengi ambao kimsingi ndiyo wenye fedha hizo kwenye mifuko ya jamii, utagundua kuwa, maoni yao hayakufanyiwa kazi au yalipuuzwa, kitu ambacho kwa mtazamo wangu haikuwa sahihi. Kwa hali hii, hata kama vyama vya wafanyakazi vilishirikishwa, basi havikuwasilisha maoni sahihi na halisi, au matakwa na mapendekezo ya wafanyakazi ambao ndiyo wenye fedha hizo. Kwa sababu hii, kuna umuhimu wa kuanzisha mjadala mpana utakaowashirikisha wadau wote muhimu kwa maana ya wafanyakazi moja kwa moja, na wengineo ili mwisho wa siku kila mmoja aondoke akiwa karidhika.
Nawasilisha.