gudJohnson
Member
- Aug 24, 2015
- 33
- 54
Habari za leo ndugu madereva mnaoendesha gari aina ya Toyota IST hapa jijini Dar na kwingineko kote Tanzania.
Awali ya yote niwapongeze kwa hatua ya kumiliki usafiri ambao unawawezesha kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa wakati. Hiyo ni hatua muhimu ya maisha ambayo kila mmoja angetamani kuifikia.
Dhumuni la waraka huu ni kuwaomba sana muwe makini mnapokua barabarani. Baadhi yenu mmekua na tabia mbaya sana muwapo barabarani na kujiona kwamba nyie ndo mna haraka sana kuliko watumiaji wengine wa barabara.
Kumekua na matukio mengi ya ku-overtake bila umakini (recklessly) na kupelekea kero kwa watumiaji wengine barabarani. Yani unakuta kajamaa kamejikunja kwenye ka-IST kake, halafu kanajifanya ndio kana haraka kuliko wengine. Jamani, sio kwamba huto tugari twenu ndo tunakimbia kuliko haya ma Ford Ranger yetu. Nawaomba sana muwe wastaarabu kwenye uendeshaji wa tugari twenu jamani.
Wito wangu kwenu ni kwamba muwe na adabu na nidhamu mnapokua barabarani ili sote kwa pamoja tutumie barabara zetu kwa uhuru.
Naomba kuwasilisha.
Awali ya yote niwapongeze kwa hatua ya kumiliki usafiri ambao unawawezesha kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa wakati. Hiyo ni hatua muhimu ya maisha ambayo kila mmoja angetamani kuifikia.
Dhumuni la waraka huu ni kuwaomba sana muwe makini mnapokua barabarani. Baadhi yenu mmekua na tabia mbaya sana muwapo barabarani na kujiona kwamba nyie ndo mna haraka sana kuliko watumiaji wengine wa barabara.
Kumekua na matukio mengi ya ku-overtake bila umakini (recklessly) na kupelekea kero kwa watumiaji wengine barabarani. Yani unakuta kajamaa kamejikunja kwenye ka-IST kake, halafu kanajifanya ndio kana haraka kuliko wengine. Jamani, sio kwamba huto tugari twenu ndo tunakimbia kuliko haya ma Ford Ranger yetu. Nawaomba sana muwe wastaarabu kwenye uendeshaji wa tugari twenu jamani.
Wito wangu kwenu ni kwamba muwe na adabu na nidhamu mnapokua barabarani ili sote kwa pamoja tutumie barabara zetu kwa uhuru.
Naomba kuwasilisha.