Skythelimit
Member
- Jul 19, 2023
- 62
- 135
Naunga mkono hoja.Wimbo wa taifa la Tanganyika;
Nchi yangu nzuri Tanganyika,
Amani, Upendo twadumisha,
Hekima, Nidhamu, Maadili,
Wote kwa pamoja tutalinda.
Mungu ibaliki,
Wabaliki watanganyika,
Wabaliki na majirani.
Kazi kwa bidii tutafanya,
Na uchumi wetu kuukuza,
Hii ni Tanganyika,
Tanganyika X2.
Majirani wetu kama Kenya, Uganda, Zanzibar, Malawi, DRC n.k wasipokuwa na amani hata sisi Tanganyika tutatereka kuanza kupokea wakimbizi.Wabaliki na majilani
Hayo ndiyo yanatukwamishwa, mpaka siku wakijikuta Tanganyika ni koloni la zenjibar ndiyo yatabaki yanajutaMakijani hayaitaki Tanganyika mpaka siku zenji watuteme jumlajumla!!
Waimbie sebuleni kwako watanganyika wako Mimi haunihusu kwa kuwa ni MtanzaniaKwa kuwa wenzetu Zanzibari wameamua kuwa na kila kitu chao kinachowatambulisha kama taifa nadhani na sisi watanganyika ni muda wa kuanza kufufua matumaini ya kuwa na utambulisho wetu kama taifa.
Bendera tunayo;
View attachment 3096531
Wimbo wa taifa la Tanganyika;
Nchi yangu nzuri Tanganyika,
Amani, Upendo twadumisha,
Hekima, Nidhamu, Maadili,
Wote kwa pamoja tutalinda.
Mungu ibariki,
Wabariki watanganyika,
Wabariki na majirani.
Kazi kwa bidii tutafanya,
Na uchumi wetu kuukuza,
Hii ni Tanganyika,
Tanganyika X2.
Wimbo upo short and clear huku maudhui yetu kama taifa yakiwa ndani mwake.
Viongozi wetu mlioko serikalini mna jukumu kubwa la kuitetea Tanganyika kwa sababu ni taifa lilopatikana kwa sacrifice ya mababu wetu wengi katika miaka ya 1945 hadi 1961, kulepelekea uhuru wa taifa la Tanganyika. Kwa hiyo siyo busara kuwaacha wazanzibari wanajivunia nchi yao huku sisi tukiopotezea Tanganyika yetu.
Ili mawazo haya ya utanganyika yasiwepo kwenye vichwa vya watanzania mhakikishe kwamba Zanzibar inajua mipaka yake kwa kukubali kuwa taifa moja la Tanzania huku ikipotezea utaifa huo inaojivika, hapo na sisi watanganyika tutakubali kuipoteza Tanganyika yetu na kujivunia utanzania wetu.
View attachment 3096567
Sasa hivi kama taifa hatuukubali huu usemi wa wahenga "wajinga ndio waliwao"
Viva Tanganyika
Mungu ibariki Tanganyika.
Tanganyika ilikufa mwaka 1964 na hatafufuka. 95% ya wanaoishi sasa wamezaliwa ndani ya Tanzania, it doesn't make sense kulilia jina ambalo haliwahusu.Huu wimbo nimeusikia na kuuimba hata kabla ya Muungano huu wa kimagumashi. Ni wakati sasa urudi kutumika kama ilivyokuwa baada ya uhuru:
1. Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanganyika jina lako ni tamu sana.
Nilalapo nakuwaza wewe,niamkapo ni heri mama wee,
Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote.
2. Tanganyika Tanganyika, ninapokwenda safarini,
Kutazama maajabu, biashara nayo makazi,
Sitaweza kusahau mimi, mambo mema ya kwetu hakika,
Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote.
3. Tanganyika Tanganyika, watu wengi wanakusifu,
Siasa yako na desturi, iliyotuletea uhuru,
Hatuwezi kusahau sisi, mambo mema ya kwetu hakika,
Tanganyika Tanganyika, nakupenda kwa moyo wote.
Yeah, marekebisho yawe kwenye kuupunguza maana nimrefu sana..Wimbo wa Taifa la Tanganyika uwe ule wa Tazama ramani! Ufanyiwe tu maboresho machache ili uendane na wakati. Tune ya huo wimbo iko poa sana.