gimmy's
JF-Expert Member
- Sep 22, 2011
- 3,283
- 3,274
Ukijaribu kuitizama nafasi ya ukatibu mkuu ndani ya CDM tangu ang'atuke Dr slaa imepwaya hata sasa.
Mara zote mdomo husema chochote,kiwe kweli ama uongo lakini nafsi husema ukweli daima, mdomo unatabia yakuongopa lakini nafsi kamwe,nafsi ya binadamu haijawahi kupinda.Ili kuelewa hili inahitaji uwe na uelewa wa ziada.
Hapa nataka kumaanisha kwamba wapo watu wanao paza sauti zao kwamba Dr Slaa si lolote si Chochote lakini ni imani yangu sauti zao na nafsi zao hazizungumzi lugha moja.Kwa vyovyote nafsi zao zinawapinga kwani ni dhahir tangu nafasi hio iachwe na Dr Slaa na kukaimiwa imepwaya hata leo.
Hapa simaanishi kwamba pengo la dr Slaa haliwezi kuzibika,laa hasha,ila mpaka sasa bado pengo lake linaonekana wazi.
Na ndio maana nimewiwa kusema kwamba Dr Slaa ni katibu mkuu adimu kuwahi kutokea CHADEMA mpaka pale atakapopatikana mtu mwenye walau utendaji kazi wakufanana na yeye.
Tena hapa niweke wazi kwamba huyu Sumaye ambaye anatajwa kuvivaa viatu vya Dr Slaa kama ni kweli basi mguu utafutiwe kiatu kingine hiki sio saizi yake,mguu wake ni mdogo sana wakati Dr alicha kiatu kikubwa hivyo kitampwaya.
Mara zote mdomo husema chochote,kiwe kweli ama uongo lakini nafsi husema ukweli daima, mdomo unatabia yakuongopa lakini nafsi kamwe,nafsi ya binadamu haijawahi kupinda.Ili kuelewa hili inahitaji uwe na uelewa wa ziada.
Hapa nataka kumaanisha kwamba wapo watu wanao paza sauti zao kwamba Dr Slaa si lolote si Chochote lakini ni imani yangu sauti zao na nafsi zao hazizungumzi lugha moja.Kwa vyovyote nafsi zao zinawapinga kwani ni dhahir tangu nafasi hio iachwe na Dr Slaa na kukaimiwa imepwaya hata leo.
Hapa simaanishi kwamba pengo la dr Slaa haliwezi kuzibika,laa hasha,ila mpaka sasa bado pengo lake linaonekana wazi.
Na ndio maana nimewiwa kusema kwamba Dr Slaa ni katibu mkuu adimu kuwahi kutokea CHADEMA mpaka pale atakapopatikana mtu mwenye walau utendaji kazi wakufanana na yeye.
Tena hapa niweke wazi kwamba huyu Sumaye ambaye anatajwa kuvivaa viatu vya Dr Slaa kama ni kweli basi mguu utafutiwe kiatu kingine hiki sio saizi yake,mguu wake ni mdogo sana wakati Dr alicha kiatu kikubwa hivyo kitampwaya.