Wilaya ya Temeke umeme kukatika kila siku

kamtesh

JF-Expert Member
Jul 26, 2014
1,395
512
Wana jamvi, hili tatizo limekua sugu huku Temeke. Umeme ni shida sana na kila siku hukatika na weekend ndo usiseme. Kwanzia asubuhi mpaka usiku. Ukuwapigia simu, wanakwambia matengenezo. Ukihoji kama walitangaza, wana kwambia ndio kwenye Radio Tumaini. Kwakweli ni kichekesho. Tangazo la shirika la umma lutangazwa kupitia radio Tumaini. Hivi kweli, Jana umeme siku nzima mulikata, Leo tena mumekata, hata ndani ya wiki nikukata tuu. Ebu twambie kitu kimoja. Nimgao au tatizo nini? Tangazeni wilaya ya Temeke haitakua na umeme kwa wiki, au mwezi mmoja ili kwaajiri ya matengenezo. Mumefika mahara, sasa munakata umeme bila kujali, hamtoi matangazo yaani, alie ongea waziri Muhongo kwamba tumechoka wananchi kukatiwa umeme hovyo, ndo hii hali. This is too much, no stable power, just not fare.
Naomba kama humu ndani kuna wadao wa hili shirika watwambi. Kwasababu hats meneja wao wa Tanesco kurasini haeleweki. Natoa hoja!
 
Duuuuh...yaelekea una hasira sana na hao Tanesco mkuu!!.
Ila samahani wewe ni "Mrundi"?.
 
Back
Top Bottom