Who created God? Who made him? Where did he come from?


Umetaja mabaya unayosema ni mabaya kwa kiwango chako cha kufikiri, hujataja mazuri ambayo Mungu amekuwa akufanya juu yako, uwepo wako duniani ni upendo tosha aliokufanyia Mungu na sidhani km unamlalamikia kuwa kwanini alikufanya uje duniani. Kiranga nilikwambia kwa uwezo wetu wa kufikiri sisi binadamu ni mdogo sn, nilikupa mfano kuwa sisimizi ajifanye kutaka kulingana uwezo wa kufikiri na ww binadamu, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa. Ukimfikiria Mungu in physical matter hutapata jibu, ila ukimfikiria Spiritually utafika mbali na utamuona Mungu
 
Sina chakukujibu coz tayari imani yako imeshashuka
 
Hata siku moja hututaweza ku describe kitu ambacho kiko unlimited na fahamu zetu ambazo ziko limited
 

Hujajibu swali.

Ni kama nakuuliza "kwa nini mama aliyemzaa mwanawe kwa upendo wote aende kumchinjiia mbali wakati ana uwezo na upendo wote wote wa kutomchinja?".

Halafu unanijibu nisiangalie mabaya tu, niangalie kwamba mama kambeba mtoto tumboni na kumnyonyesha.

Swali langu hujalijibu.
 
Thinking beyond perception ni mbaya sana unaeza ukawa kichaa!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
wewe unajua au unaamini mungu hayupo ??

Kutokana na kila tunachokijua hadi sasa kuhusu dunia ama ulimwengu huu hakuna haja ya mungu!na kwa sababu hakuna ushahidi basi hayupo. Kama una ushahidi lete hapa
 
si kila swali lina jibu.

"mimi niko ambaye niko" yeye alikuwako, yuko na ataendelea kuwepo milele yote.

kaa uamini hivyo, ukiendelea kuchunguza utakuwa chizi.
 
Haiingii akilini kabisa. time is real and its here. anything real must adhere to reality such as time.., unless God isn't real.., is it..?!

Time ni mfumo wa kibinaadamu tu. Ukiiliza wazee wako kabla wazungu hawajaja kulikuwa hamna time. Huwezi kupata majibu uliyonayo kichwani kumhusu Mungu usipoweka swala la imani. UKITAKA KUPATA UWEPO WA MUNGU LAZIMA UWE NA IMANI KUMHUSU.
 
Kutokana na kila tunachokijua hadi sasa kuhusu dunia ama ulimwengu huu hakuna haja ya mungu!na kwa sababu hakuna ushahidi basi hayupo. Kama una ushahidi lete hapa

kwa nini hakuna haja ya uwepo wa mungu
haja yako ni nini ili ujue mungu yupo au hayupo ??
 
kwa nini hakuna haja ya uwepo wa mungu

Kwa sababu hakuna kinachohitaji mungu ama uwepo wa mungu ili kiwepo!
haja yako ni nini ili ujue mungu yupo au hayupo ??

Mungu ni idea na sio real figure ama spirit kama mnavoita.Ni idea tu ambayo ipo tu.
Haja yangu ni kwamba ilikuwaje mungu mwenye upendo wote na nguvu zote akashindwa kuepusha maovu katika dunia aliyoiumba na kuipenda kweli?.Kwa nini kama kwel yupo anashindwa kumwangamiza huyo mnaemwita shetani!?.Je shetani anafanya mambo yake kwa mamlaka ya nani?
 

ulitaka kiwepo nini ili uamini mungu yupo au hayupo ?

Kila kinachotokea ni mipango ya mungu hivyo unavyotafsiri wewe kama maovu labda kwa mungu sio maovu??
Kama binadamu hatuna maana moja ya tafsiri itakuwa wewe na mungu ??
 

Je unaweza kuipa infinity (&#8734😉 value ? Naomba jibu la ∞-1.
 
Wakuu mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kama kweli niachane na imani za mababu zangu wa kale (bfr colonialism) na kuadopt hizi imani mpya za kikoloni katika suala la kidini. Kitu kinachonipa utata nimegundua kwamba Mungu wa kikoloni (namaanisha imani za kidini zilizoletwa na wageni afrika) be it Allah or Jehovah na Miungu ya kijadi wote wana sifa zifuatazo zinazorandana.

  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanatumika kuombwa msaada hasa nyakati za shida, hofu au hatari inapomkabili binadamu.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wametengewa maeneo maalumu yanayoheshimiwa sana kwa ajili ya kuendeshea ibada, sadaka/makafara mbali mbali mfano misikiti, mahekalu, mipango, milima maalum au miti mikubwa.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanainfluence utamaduni, kasumba au mtindo wa maisha wa binadamu ambao wanawaamini mfano uislamu na tamaduni zake, ukristo na tamaduni zake, upagani na tamaduni zake.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanatumika katika kuongoza binadamu waishi katika misingi inayokubalika ktk jamii kwa hofu ya kupata laana, adhabu za kiroho baada ya kifo au mabalaa mbalimbali ktk jamii.
  • Iwe mungu wa kikoloni au mungu wakijadi wote hawa wanahubiri ukuu na ufalme kwamba hakuna kiumbe yoyote mwenye ukuu na ufalme kushinda wao, na hivyo in return mwanadamu inabidi atoe sadaka au kafara kama kuonyesha utii wake kwa mungu husika.
  • KAMA IKO NYINGINE ONGEZEA WEWE

Bado sijaona hasa mungu yupi kati ya hao anamzidi mwenzie na hili swala la kuchanganywa imani liko sana kwa hizi nchi zetu za dunia ya tatu lakini huwezi kuongea kitu kwa wahindi na Hindu religion yao wala wachina na majirani zao na Budha wao (just to mention the few)

Jumatatu kareem
(dont bother with spelling errors just focus on the content)
 

Swali hili halijapata jibu bado.
 

Aina hii ya swali linatakiwa liulizwe na mtu ambae anakubali uwepo wa Mungu na Shetani

Unapotengeneza swali kwa ku assume ni tatizo kwakuwa tayari hiyo ni assumption

Kama hukubali uwepo wa Mungu huna haja ya kuhoji kitu kisichokuwepo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…