The Palm Beach
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 3,612
- 9,269
Hivi hii tuiteje kweli? Kufuru dhidi Mungu Yehova, ujinga, upumbavu au ni kilele cha kiburi cha CCM na watawala wao..?
Mimi nimejaribu kufikiri huyu mbunge alikuwa amefikiri nini kumtetea Rais Samia Suluhu Hassan against Askofu Josephat Gwajima kwa kauli yake hii...?
Je, ubinadamu wa mtoto wa Rais aitwaye Abdul kumbe ni wa thamani zaidi kuliko mamia ya raia wasio na hatia (innocent citizens) waliokwisha kutekwa, kuteswa, kupotezwa na kuuwawa na vyombo vya serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan...?
Je, Abbas Tarimba ana maana ya kuwa damu ya kina Mdude, Deusdedit Soka, Manengelo, Padri Charles Kitima, Tundu Lissu na wengine zaidi ya 83 ni za wanyama mbwa na nguruwe tu kwa thamani kulinganisha Abdul - binadamu kwa sbb ni mtoto wa Rais Samia Suluhu Hassan...?
Duuh, this is a blasphemy of highest degree....!
Je, alikuwa na maana kuwa wazazi wa hawa watoto, Watanzania wenzake Abbas Tarimba hawakuzaa kwa uchungu kama Bi Samia Suluhu Hassan alivyozaa vilevile na kulea hawa watoto waliouwawa kikatili na Polisi wa Tanzania kwa amri ya Rais Samia...?
➡️Hebu nisaidieni kuelewa...➡️