Werrason Ngiama Vs Fally Ipupa nani zaidi?

Losambo

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
2,612
864
Wadau wa masebene nadhani mtakubaliana nami kuwa katika kizazi cha muziki wa Congo saizi huwezi kuzungumza bila kumtaja Werrason au Fally Ipupa.

Hawa wote ni wakali mbaya, ukianza na Werrasson album yake ya Techno Malewa imewapagaisha wengi.

Fally Ipupa nae ni kitisho ukichukua baadhi ya nyimbo zake kama Sopeka n.k zinazidi kumuweka juu.

Watu hawa wanafanana kitu kimoja, wote ni wakali wa live perfomance.

Hapo ndipo napenda tujikite zaidi. Licha ya kuwa na nyimbo nzuri lakini wanapokuwa live hutisha zaidi.

Baada ya kuwapamba kila mmoja nani zaidi kati yao?

Ni Werrasson Ngiama au Fally Ipupa?

Karibuni wadau wa masebene.

Nawasilisha.
 
Huyo ipupa ni mpiga makelele kama beberu, hampati werason ngiama, tena hawatii pua kwa jb mpiana mukulu!!
 
Huyo ipupa ni mpiga makelele kama beberu, hampati werason ngiama, tena hawatii pua kwa jb mpiana mukulu!!
Kweli kabisa,fally ipupa akapambanishwe na akina felix wazekwa huko,huyu werrason yupo level za akina gola,olomide na JB Mpiana.
 
Hakika haujamndea haki Noel Ngiama Makanda 'Werrason' kwa kumlinganisha na bwana mdogo Fally Ipupa....

Kiukweli Werrason sio size ya Fally Ipupa,Werrason size yake ni Jean-Bedel Mpiana, Adolphe Dominguez, Paschal Poba, Felix Wazekwa, Charles Antoine 'Koffi Olomide' na wengine..Kumbuka kwamba Werrason ni mmojawapo wa waanzilishi wa bendi machahari ya Wenge Musica BCBG ambayo waliianzisha mwaka 1981 na imetamba mpaka iliposambaratika mwaka 1997...Pia kumbuka kwamba Werrason ni mtunzi wa nyimbo ambazo miaka nenda rudi haziishi utamu/hazichuji...Nyimbo kama Kala Yi Boeing,Solola Bien, Force D'Intervention Rapide, Opearation Dragon, Kibuisa Mpimpa na bila kuvisahau vibao vitamu vilivyopo kwenye albamu yake ya Techno Malewa Suit En Fin....Kwa ujumla Werrason na Fally Ipupa ni sawa na Mbingu na Ardhi mkuu ama Yanga na Barca.......

Fally Ipupa yeye size yake(wa kuwalinganisha/kuwapambanisha naye) ni akina Ferre Gola, Bill Clinton Kalodji ,Montana Kamengana wengine....Kumbuka kwamba Fally ni bwa'mdogo ambaye ameibuliwa na Le Grand Mopao Charles Antoine Koffi Ollomide ambapo alikuwa ni mmojawapo wa wanamuzii waliounda Quartier Latin International(ambayo ilianza tangu mwaka 1986 na bwana mdogo Fally amejiunga mwaka 1999)...Alikuwa akiimba na vijana kama Montana Kamenga,Geco Mpela, Ferre Gola(baadae alihamia kwa Werrason).......Hii inaonesha ni jinsi gani Fally alivyo bwana mdogo kwa Koffi kimuziki na kiumri na pia kuheshimika kimataifa....
 
Hakika haujamndea haki Noel Ngiama Makanda 'Werrason' kwa kumlinganisha na bwana mdogo Fally Ipupa....

Kiukweli Werrason sio size ya Fally Ipupa,Werrason size yake ni Jean-Bedel Mpiana, Adolphe Dominguez, Paschal Poba, Felix Wazekwa, Charles Antoine 'Koffi Olomide' na wengine..Kumbuka kwamba Werrason ni mmojawapo wa waanzilishi wa bendi machahari ya Wenge Musica BCBG ambayo waliianzisha mwaka 1981 na imetamba mpaka iliposambaratika mwaka 1997...Pia kumbuka kwamba Werrason ni mtunzi wa nyimbo ambazo miaka nenda rudi haziishi utamu/hazichuji...Nyimbo kama Kala Yi Boeing,Solola Bien, Force D'Intervention Rapide, Opearation Dragon, Kibuisa Mpimpa na bila kuvisahau vibao vitamu vilivyopo kwenye albamu yake ya Techno Malewa Suit En Fin....Kwa ujumla Werrason na Fally Ipupa ni sawa na Mbingu na Ardhi mkuu ama Yanga na Barca.......

Fally Ipupa yeye size yake(wa kuwalinganisha/kuwapambanisha naye) ni akina Ferre Gola, Bill Clinton Kalodji ,Montana Kamengana wengine....Kumbuka kwamba Fally ni bwa'mdogo ambaye ameibuliwa na Le Grand Mopao Charles Antoine Koffi Ollomide ambapo alikuwa ni mmojawapo wa wanamuzii waliounda Quartier Latin International(ambayo ilianza tangu mwaka 1986 na bwana mdogo Fally amejiunga mwaka 1999)...Alikuwa akiimba na vijana kama Montana Kamenga,Geco Mpela, Ferre Gola(baadae alihamia kwa Werrason).......Hii inaonesha ni jinsi gani Fally alivyo bwana mdogo kwa Koffi kimuziki na kiumri na pia kuheshimika kimataifa....

Mkuu nakubaliana na wewe kabisa lakini Fally Ipupa kwa sasa nae kidogo anakuja kuja na wapo baadhi ya watu wanamuona yupo juu.

Koffi kwa sasa ni kama kafulia vile, kuna kibao kimoja Cindy alikiimba ndiyo nakiona kimenyanyua kidogo. Kesho nitaweka link yake.
 
Hakika haujamndea haki Noel Ngiama Makanda 'Werrason' kwa kumlinganisha na bwana mdogo Fally Ipupa....

Kiukweli Werrason sio size ya Fally Ipupa,Werrason size yake ni Jean-Bedel Mpiana, Adolphe Dominguez, Paschal Poba, Felix Wazekwa, Charles Antoine 'Koffi Olomide' na wengine..Kumbuka kwamba Werrason ni mmojawapo wa waanzilishi wa bendi machahari ya Wenge Musica BCBG ambayo waliianzisha mwaka 1981 na imetamba mpaka iliposambaratika mwaka 1997...Pia kumbuka kwamba Werrason ni mtunzi wa nyimbo ambazo miaka nenda rudi haziishi utamu/hazichuji...Nyimbo kama Kala Yi Boeing,Solola Bien, Force D'Intervention Rapide, Opearation Dragon, Kibuisa Mpimpa na bila kuvisahau vibao vitamu vilivyopo kwenye albamu yake ya Techno Malewa Suit En Fin....Kwa ujumla Werrason na Fally Ipupa ni sawa na Mbingu na Ardhi mkuu ama Yanga na Barca.......

Fally Ipupa yeye size yake(wa kuwalinganisha/kuwapambanisha naye) ni akina Ferre Gola, Bill Clinton Kalodji ,Montana Kamengana wengine....Kumbuka kwamba Fally ni bwa'mdogo ambaye ameibuliwa na Le Grand Mopao Charles Antoine Koffi Ollomide ambapo alikuwa ni mmojawapo wa wanamuzii waliounda Quartier Latin International(ambayo ilianza tangu mwaka 1986 na bwana mdogo Fally amejiunga mwaka 1999)...Alikuwa akiimba na vijana kama Montana Kamenga,Geco Mpela, Ferre Gola(baadae alihamia kwa Werrason).......Hii inaonesha ni jinsi gani Fally alivyo bwana mdogo kwa Koffi kimuziki na kiumri na pia kuheshimika kimataifa....

Mkuu umeiweka kama nilivyotaka kusema ...
Tena hata Bill Clinton na Tutu Kalodji sio size yake bado, sema tu ho majembe nyota zao ni za kawaida pia ni ma team player...
Fally Ipupa anaangukia huko kwa akina Ferre Golla na wakina CNN ( yule repa wa Koffi baada ya kuondoka wale Quatterettin ya wakina Suzuki) amerap kwenye ile nyimbo ya Artentant (nismehe matamshi ila kama ni mfutiliaji wa Koffi najua umeipata hiyo nyimbo)....

Nasikitika kusema inapokuja kwenye bolingo Fally Ipupa kwangu anapata marks za chini sana....

Ahsante mkuu kwa kunipa hizo kumbukumbu za wakongwe.
 
... mie hapa nasikiliza Orchestra VEVE kibao kinaitwa yanini. huu mziki wa Kavasha ni mtamu ajabu! Akina Fally Ipupa dah just cant comment!! lkn ukiwa na time sikiliza mziki wa akina Verckys, Kiamangwana mateta, Mombasa vata, Nzaya Nzayadio! oh roho inataka kuniruka hapa nikikumbuka enzi za Kavasha!
 
Tunachanganya mambo hapa..........kuna swala la ukongwe na kuna swala la nani anafanya vizuri kwa sasa

Kwa ukongwe wa sikunyingi na kutunga nyimbo nyingi zilizofanya vizuro ofkozi Ngiama Makanda ataukuwa juu
Swala la nani anafanya vizuri kwa sasa ni debatable

Kwa maoni yangu Fally Ipupa yupo vizuri zaidi kwa sasa, Fally ana management iiliyokwenda shule na anaangalia zaidi masoko ya kimataifa zaidi ya Condo na Paris
Fally anakubalika zaidi hata nje ya Congo hasa baada ya kufanya makolabo ya kufa mtu almost all over the world.
Fally yupo flexible ku adapt aina mbali mbali za musiki kama alivyokuwa Papa Wemba tofauti na Werrason aliyejikita kwenye bolingo original na kumfanya akubalike zaidi Congo na nchi zinazopenda miziki ya kikongo tu.
Fally anakubalika zaidi na kizazi kipya cha dot com

Lakini hii yote haiondoi ubora na umahiri wa Werrason isipokuwa kwa sasa Fally Ipupa ni zaidi.....maoni ynagu tu
 
Tunachanganya mambo hapa..........kuna swala la ukongwe na kuna swala la nani anafanya vizuri kwa sasa

Kwa ukongwe wa sikunyingi na kutunga nyimbo nyingi zilizofanya vizuro ofkozi Ngiama Makanda ataukuwa juu
Swala la nani anafanya vizuri kwa sasa ni debatable

Kwa maoni yangu Fally Ipupa yupo vizuri zaidi kwa sasa, Fally ana management iiliyokwenda shule na anaangalia zaidi masoko ya kimataifa zaidi ya Condo na Paris
Fally anakubalika zaidi hata nje ya Congo hasa baada ya kufanya makolabo ya kufa mtu almost all over the world.
Fally yupo flexible ku adapt aina mbali mbali za musiki kama alivyokuwa Papa Wemba tofauti na Werrason aliyejikita kwenye bolingo original na kumfanya akubalike zaidi Congo na nchi zinazopenda miziki ya kikongo tu.
Fally anakubalika zaidi na kizazi kipya cha dot com

Lakini hii yote haiondoi ubora na umahiri wa Werrason isipokuwa kwa sasa Fally Ipupa ni zaidi.....maoni ynagu tu

Nakubali uchambuzi wako sana tu,
 
Nakubali uchambuzi wako sana tu,

Narudia tena, Fally ipupa anapiga makelele jukwaani, Werason anaimba kwa ustadi mkubwa, hata kama huelewi lugha anayotumia, ustadi wa sauti yake utakuburudisha.
Werason usipime!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom