Wenye Nyumba/Vyumba vya kukodisha msiogope

Wenye Nyumba/Vyumba vya kukodisha msiogope

jebs2002

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2008
Posts
11,021
Reaction score
10,683
Wenye nyumba/vyumba/viwanja/frames za kukodisha, msiogope maswala ya wapangaji wenu kulipa kodi kila mwezi, hasa kama dola imetamka hivyo, na wanadai watakuja na mfumo utakaowalinda wapangaji na wapangishaji, kama ni hivyo basi hatuoni tatizo, hasa kama mikataba yenu itatamka wazi vipengele vyote kuhusu upangishaji wa hiyo sehemu.

Kuna kodi ya miezi 2 au 3 itatolewa kama Deposit, na kodi ya mwezi mmoja juu.
Hii "Deposit" tuikumbuke ni kwa ajili ya kukulinda mwenye boma kama kutakuwa na uharibifu wa aina yoyote pale kwako, na kama hela itabakia basi itatumika kama kodi ya mwezi au ile miezi michache aliyokaa mteja wako bila kulipa kodi..

Twajijuwa raia, mwanzoni mwa hii mikataba lazima kutatokea tafrani nyingi tu, polisi na mahakama ya ardhi n.k. Hasa za wateja ambawo hawajalipa kodi zao kwa muda unaohitajiwa na kusababisha kodi kulundikana, na kuwa vigumu kulipa, dola imesema itatunga sheria za kukulinda wewe mwenye boma hili swala litakapotokea..

Nahisi dola pia itaweka sheria za wewe mwenye boma kumpa notisi ya muda fulani mfupi mteja wako endapo utakuwa hujaridhika na kiwango anacholipa kwa mwezi kwa muda huo..

Pia kutokana na mikataba hii mifupi, tutegemee utakuwa ukibadilisha wateja kukicha, kwa bei uitakayo wewe mwenye boma..

Tunategemea pia mpangishaji atapata uhuru wa kuhamia nyumba mpya kila baada ya miezi michache, sababu mikataba sasa itakuwa mifupi..

Yaonekana hii sheria ikija itawanufaisha na kufedhehesha pande zote 2, ni nzuri, kwani siyo lazima tena kwa mwenye boma na mpangaji kuzoena kama zamani..
Yawezekana hii sheria imeletwa kupunguza rushwa na ufisadi makazini petu, tukumbuke hata wale wanaopangisha vimada sasa yawezekana tena...

Wenye nyumba, tuikubali hii sheria ikija, nina uhakika itasaidia pande zote 2, hasa hasa kwenu wenye maboma..

Au?
 
Azam TV - MIZANI YA WIKI (19/11/2017): Lukuvi kuhusu kuwabana wanaotoza ... via YouTube
 
KUHUSU WAZIRI WANYUMBA NA MAKAZI KUWAOMBA WENYENYUMBA KUPANGISHA KWAMWEZI MMOJA MMOJA JE KUNAWEZA KUWAPA UNAFUU WAPANGAJI AU NDO KUNAWEZA KUWAPA MAISHA MAGUMU ZAIDI?
 
mimi naona kila mwenye nyumba aweke makubaliano na wapangaji wake ndio maana kuna mikataba.maana kuna wapa ngaji wengine wanapenda kulipa kila baada ya miezi 6 au 3 au 2.kulingana na kipato chake anachokipata.kuweka mwezi 1 alipe hapo kuwapa lawama wenye nyumba maana kuna wapangaji wengine ni wasumbufu kwerikweri,hawaishiwi visingizio mara mwezi huu mambo yamekwenda hovyo yaani hawaishiwi visingizio.naona hapo wameongelea upande mmoja.sasa na mimi mwenye nyumba mwezi ukifika mpangaji pesa hana nimfukuze kwenye chumba changu,hilo hawaja ongelea.tatizo huwa wanakulupuka sana,jambokama hili ni la kukaa chini kuangalia nini tatizo nakupata suluhisho ambalo alito muumiza mpangaji wala mwenyenyumba.
 
mimi naona kila mwenye nyumba aweke makubaliano na wapangaji wake ndio maana kuna mikataba.maana kuna wapa ngaji wengine wanapenda kulipa kila baada ya miezi 6 au 3 au 2.kulingana na kipato chake anachokipata.kuweka mwezi 1 alipe hapo kuwapa lawama wenye nyumba maana kuna wapangaji wengine ni wasumbufu kwerikweri,hawaishiwi visingizio mara mwezi huu mambo yamekwenda hovyo yaani hawaishiwi visingizio.naona hapo wameongelea upande mmoja.sasa na mimi mwenye nyumba mwezi ukifika mpangaji pesa hana nimfukuze kwenye chumba changu,hilo hawaja ongelea.tatizo huwa wanakulupuka sana,jambokama hili ni la kukaa chini kuangalia nini tatizo nakupata suluhisho ambalo alito muumiza mpangaji wala mwenyenyumba.
Unavyosema mkuu nayo yapo kwenye taarifa ya Mh. Lukuvi..
Kwamba mteja akitaka kulipa miezi 6, 12, 36 hazuiwi, ila kama kama anataka kulipa kwa mwezi baada ya kutoa DEPOSIT ya miezi 3 basi wewe kama mwenye nyumba mfikirie, kifupi ni marufuku kusema unakodisha nyumba kuanzia miezi 6 na kuendelea..
Mkataba kati ya wewe na mteja wanadai hawataingilia...
Ila wewe mwenye nyumba hujashinikizwa hela gani utamtoza mpangaji wako, kwa kweli nilipinga sana hili mwanzoni, ila kama dola imeshinikiza, sisi ni nani wa kulikataa, tena tununue na EFD mashine kabisa, ili iwe biashara rasmi, kwamba kila ukipokea kodi, toa risiti ya EFD, biashara yako ya "Real Estate" inakuwa rasmi, mpe ya Kaisari na wewe ubaki na yako, yawezekana..
Uzuri wa hii system mkuu, kama kanyumba ulikuwa wakodisha kwa laki 3, sasa waweza fanya hata laki 5!
Poa tu, tutafika...
 
Unavyosema mkuu nayo yapo kwenye taarifa ya Mh. Lukuvi..
Kwamba mteja akitaka kulipa miezi 6, 12, 36 hazuiwi, ila kama kama anataka kulipa kwa mwezi baada ya kutoa DEPOSIT ya miezi 3 basi wewe kama mwenye nyumba mfikirie, kifupi ni marufuku kusema unakodisha nyumba kuanzia miezi 6 na kuendelea..
Mkataba kati ya wewe na mteja wanadai hawataingilia...
Ila wewe mwenye nyumba hujashinikizwa hela gani utamtoza mpangaji wako, kwa kweli nilipinga sana hili mwanzoni, ila kama dola imeshinikiza, sisi ni nani wa kulikataa, tena tununue na EFD mashine kabisa, ili iwe biashara rasmi, kwamba kila ukipokea kodi, toa risiti ya EFD, biashara yako ya "Real Estate" inakuwa rasmi, mpe ya Kaisari na wewe ubaki na yako, yawezekana..
Uzuri wa hii system mkuu, kama kanyumba ulikuwa wakodisha kwa laki 3, sasa waweza fanya hata laki 5!
Poa tu, tutafika...
kwer mkuu kwa mpango huo wapangaji ndio watakiona chamoto.
 
Back
Top Bottom