We NEED a Way Foward ASAP!

Bramo

JF-Expert Member
Oct 21, 2009
13,160
10,007
Tunahitaj Muongozo ama kwa haraka iwezekanavyo, nini tunafanya, dalili zote zinaonesha Magamba wanataka kuupitisha ule Muswada na Mkwe.re atausaini fasta uwe sheria, Jaman tunahitaj Muongozo, Tuko Tayar kwa lolote, who is taking the lead, CDM? Jukwaa la Katiba Please please Please.

A way foward ,inahitajika AS SOOON AS POSIBLE
 
Licha ya watu na makundi mbali mbali kuupinga muswada wa marekebisho ya Katiba usisomwe kwa mara ya pili na ya tau na kisha kuanza kujadiliwa, jana tarehe 14 Nov 2011, muswada huo ulisomwa kwa mara ya pili na ya tatu na kuanza kujadiliwa.

Kwa jinsi Spika alivyoendesha mjadala huo ni dhahiri kuwa yalikuwepo maandalizi ya makakati mzito baina ya vyama vitatu vya CCM, CUF na TLP kwa kuwatumia wasemaji wao mahiri Mhe A Kilango, Mhe Khalfan na Mhe A Mrema; wasemaji hawa wote walilenga kutuma ujumbe kwa wananchi kuukubali mchakato unaopendekezwa, na kujiepusha na mambo waliyoyaita ni vuruga na uvunjifu wa amani.

Kama ilivyotarajiwa wabunge wa CDM waliandika historia tena kwa kutoka nje ya bunge kupinga uchakachuaji wa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya. Aidha msemaji wa kambi ya upinzani Mhe Tundu Lissu alitia fora kwa kufichua namna CCM kwa kushirikiana na CUF na vyama vingine vidogo ilivyokusudia kuuza utu na haki za watanganyika kwa muswada huu kuipatia Zbar, Rais wa Zabar na wawakilishi wa Zbar madaraka makubwa ya kujadili hata mambo hata yasiyo ya muungano.

Jambo la kutia faraja idadi ya wabunge waliomua kutoka nje kupinga ubabe wa Spika iliongezeka na kuhusisha pia wabunge wa vyama vingine.

Kwa kuwa wawakilishi wetu wameshatimiza wajibu wao licha ya upungufu wao, sisi wapenda mabadiliko tufanye nini ili kuokoa muswada huu ili hatimaye Tanzania iweze kupata Katiba mpya iliyo bora?
 
Back
Top Bottom