Wbunge wote wapewe wafundishwe Sheria

ebrah

JF-Expert Member
Oct 9, 2010
396
50
Salaam wana JF,
Jamani mimi nimekuwa nikiangalia vikao mbalimbali vya Bunge Letu, kugundua Mapungufu Mengi yanayohusiana na mabo ya sheria na Jinsi ya kutafsiri sheria, tatizo ambalo limepelekea nchi Yetu kuwa na sheria nyingi mbovu na zenye kuwabana wanyonge na zisizo tuonyesha mwanga a Maendeleo wanachi, kwani tinafahamu kuwa BUNGE ndo chombo kikuu kinachuhusika na utungaji na marekebishombalimbali ya sheria.
Jambo hili Lipo wazi kwani ukiangalia tofauti za michango inayotolewa bungeni utagundua, hasa kipindi Hiki ambacho wabunge wengi wa upinzani wamesomea Sheria, na hii ndio sababu tunaona mabadiliko makubwa sana bungeni siku za hivi karibuni kwani mambo mengi ya liyokuwa yanafichwa huko nyuma sasa hivi yanawekwa wazi, na matokeo yake wabunge wa Magamba wameishia kukubali hoja hata kamahawazikubali.

Kutokana na hali hii, niwazi kuwa ufinyu wa wa uelewa wa masuala ya sheria unasababisha mapungufu mengi katika kupitia na kusimamia kanuni mbalimbali za Bunge na hii inasababisha vitu vingi kupitishwa bila kuwa na vigezo.

Kwa nini sasa usianzishwe utaratibu wa kuwapa wabunge wote Elimu ya Sheria kwqa kifupi ili kuwezesha kuchangia na kutunga sheria zenye mshiko kwa watanzania?
 
Back
Top Bottom