Waziri wa TAMISEMI, Selemani Jafo: Kwa kasi hii, Watu watakuja nchini kujifunza Utendaji kazi wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
View attachment 845756

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. Selemani Jafo, akiwa anaongea kwenye kipindi cha Tunatekeleza cha TBC, saa 6 mchana, amesifia kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuibadilisha Tanzania kuelekea katika uchumi wa kati na kwamba kwa kasi hiyo, "Watu watakuja kujifunza juu ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano."
Jafo alitoa takwimu kadhaa zinazoonyesha mabadiliko makubwa yaliyofanywa ndani ya kipindi kifupi tangu Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli iingie madarakani mwaka 2015. Baadhi ya mambo aliyoongelea kwenye sekta za Afya na Elimu ni yafuatayo:
  • Sekta ya Afya: Tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961 hadi mwaka 2015, kulikuwepo Vituo vya Afya 515, kati ya hivyo, vinavyotoa huduma za upasuaji 115 pekee lakini ndani ya miaka miwili na nusu, Vituo vya huduma ya upasuaji vimeongezeka na kufikia 204, sawa na ujenzi wa vituo 89 ndani ya miaka miwili pekee. Alisema kuwa, wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani, kulikuwepo hospitali 72 pekee katika jumla ya Halmashauri 184 nchini lakini ndani ya Bajeti ya mwaka huu wa 2018/2019 pekee, Serikali itajenga hospitali 63 huku Vituo vya afya 67 vikiwa vinajengwa Nchi nzima.
  • Elimu Msingi Bila Malipo: Kumekuwepo kasi kubwa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, maabara na madawati kwa ajili ya kukidhi ongezeko kubwa la wanafunzi. Alitolea mfano wa Shule ya Msingi Maji Matitu, jijini Dar es Salaam, iliyokuwa imepanga mwaka 2017 kusajili (maotea) wanafunzi 260 lakini ilijikuta ikisajili wanafunzi 1026!! Vilevile, upatikanaji wa vitabu umeongezeka kutoka wanafunzi 8 kwa kitabu hadi wanafunzi 3 kwa kitabu.
Waziri Jafo aliongelea pia jitihada za Serikali katika Sera ya viwanda kwa kila Mkoa, ujenzi wa barabara chini ya TARURA, pamoja na miradi ya maji, shule etc.

Waziri aliwakumbusha Wakurugenzi wa Halmashauri juu ya wajibu wao katika kuharakisha maendeleo kwenye maeneo yao na "kuwaonya Wakurugenzi wasioendana na kasi ya Serikali wasione ajabu wakiondolewa kwenye nafasi zao na wasitafute mchawi kuwa, sijui wamerogwa bali ni utendaji kazi wao."
Jafo alidai kuondolewa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Kigoma Mjini, Pangani na Nkasi ni kutokana na kutoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Jafo akiwa kwenye Kikao na Wadau wa Elimu nchini jijini Mwanza, mwaka 2017, alitabiri mabadiliko makubwa katika performance ya shule za Serikali kulinganisha na za binafsi kwa sababu ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali kwa shule zake, ikiwemo kujenga maabara za sayansi, kuondoa ada, kusambaza vitabu, kutengeneza madawati, kuongeza vyumba vya madarasa na kuajiri walimu wengi mpaka kufikia mahitaji ya walimu wa Arts kutosheleza kabisa. Aliwaambia wadau kuwa, ana uhakika ni shule chache tu za binafsi zitabakia kutokana na maboresho hayo makubwa yakiwemo ya kukarabati shule kongwe. Matokeo ya Kidato cha VI mwaka 2018, ni mwanzo tu wa "changing of guard" kati ya shule za umma dhidi ya za binafsi.

Mnyonge mnyongeni haki yake mwachie. Iliyokwishayafanya ni mengi mno kwenye sekta ya elimu na afya, wote tunaona.
 
Ila kwenye demokrasia tumefeli hii biashara ya inayoendelea ya chaguzi za marudio kila leo eti kisa watu "wanajiuzulu" hapa hawana la kujifunza. Kuvunja katiba kwa kuzuia shughuli halali na kuweka mipaka ya watu kutembea na kuongea au kutoa mawazo sehemu yoyote wakati katiba inaruhusu hapa inabidi watupe pole
 
Nauliza hiyo maji matitu baada ya kutoka wanafunzi 200 mpaka 1000 kuna waalimu wameongezwa. Kuongezeka wanafunzi sio kazi ya serikali kuprovide resources ndo kazi ya serikali je wameprovide?
 
Adakabra tu hizi. Kwa miaka 50+ ya uhuru bado mtu anajadili suala la vituo vya afya huku wagonjwa wakipelekwa India! Anajadili suala la ujenzi wa madarasa na vitabu kwa uwiano wa 1:3 huku tulipo ni hakuna kabisa kwani ni 1:160. Ningekuwa mwandishi ningemuuliza kazi ya sensa ni nini hasa hizi za watoto wanaotarajia kujiunga na darasa la kwanza zinazofanyika kila mwaka! Mbona maji safi hakuzungumzia? Au yametosheleza?
Bado nchi ina safari ndefu isiyohitaji data bali utekelezaji na ugawaji wa huduma za jamii kwa kasi!
 
DEMOCRASIA NI NINI? WASIBORESHE HUDUMA ZA KIJAMII ILA DEMOCRASIA
Kama akili kama hizi kazi kubwa sana tunayo!!ni nchi ngapi duniani zenye kuendeshwa ki dikiteta zimepiga maendeleo makubwa?kulinganisha na zile zenye demokrasia ya kweli??kama sio kuficha mapungufu yao na upigaji!!kama unapeleka maendeleo unahofia nini wwtu kuhoji pale kwenye shida!!!ni suala la muda tu,miaka zaidi ya 50,kiongozi anakuja sifia vituo vya afya,matundu ya vyoo wakati toka uhuru ni hao hao ndio wameongoza nchi na kutufikisha hapa leo mtu anataka sifa?!!wakati ni vitu ambavyo vingefanyika miaka ya 1970's!!!!eti ndio vision 2020-2025 uchumi wa kati ni ndotooo
 
View attachment 845756

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. Selemani Jafo, akiwa anaongea kwenye kipindi cha Tunatekeleza cha TBC, saa 6 mchana, amesifia kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuibadilisha Tanzania kuelekea katika uchumi wa kati na kwamba kwa kasi hiyo, "Watu watakuja kujifunza juu ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano."
Jafo alitoa takwimu kadhaa zinazoonyesha mabadiliko makubwa yaliyofanywa ndani ya kipindi kifupi tangu Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli iingie madarakani mwaka 2015. Baadhi ya mambo aliyoongelea kwenye sekta za Afya na Elimu ni yafuatayo:
  • Sekta ya Afya: Tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961 hadi mwaka 2015, kulikuwepo Vituo vya Afya 515, kati ya hivyo, vinavyotoa huduma za upasuaji 115 pekee lakini ndani ya miaka miwili na nusu, Vituo vya huduma ya upasuaji vimeongezeka na kufikia 204, sawa na ujenzi wa vituo 89 ndani ya miaka miwili pekee. Alisema kuwa, wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani, kulikuwepo hospitali 72 pekee katika jumla ya Halmashauri 184 nchini lakini ndani ya Bajeti ya mwaka huu wa 2018/2019 pekee, Serikali itajenga hospitali 63 huku Vituo vya afya 67 vikiwa vinajengwa Nchi nzima.
  • Elimu Msingi Bila Malipo: Kumekuwepo kasi kubwa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, maabara na madawati kwa ajili ya kukidhi ongezeko kubwa la wanafunzi. Alitolea mfano wa Shule ya Msingi Maji Matitu, jijini Dar es Salaam, iliyokuwa imepanga mwaka 2017 kusajili (maotea) wanafunzi 260 lakini ilijikuta ikisajili wanafunzi 1026!! Vilevile, upatikanaji wa vitabu umeongezeka kutoka wanafunzi 8 kwa kitabu hadi wanafunzi 3 kwa kitabu.
Waziri Jafo aliongelea pia jitihada za Serikali katika Sera ya viwanda kwa kila Mkoa, ujenzi wa barabara chini ya TARURA, pamoja na miradi ya maji, shule etc.

Waziri aliwakumbusha Wakurugenzi wa Halmashauri juu ya wajibu wao katika kuharakisha maendeleo kwenye maeneo yao na "kuwaonya Wakurugenzi wasioendana na kasi ya Serikali wasione ajabu wakiondolewa kwenye nafasi zao na wasitafute mchawi kuwa, sijui wamerogwa bali ni utendaji kazi wao."
Jafo alidai kuondolewa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Kigoma Mjini, Pangani na Nkasi ni kutokana na kutoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Jafo akiwa kwenye Kikao na Wadau wa Elimu nchini jijini Mwanza, mwaka 2017, alitabiri mabadiliko makubwa katika performance ya shule za Serikali kulinganisha na za binafsi kwa sababu ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali kwa shule zake, ikiwemo kujenga maabara za sayansi, kuondoa ada, kusambaza vitabu, kutengeneza madawati, kuongeza vyumba vya madarasa na kuajiri walimu wengi mpaka kufikia mahitaji ya walimu wa Arts kutosheleza kabisa. Aliwaambia wadau kuwa, ana uhakika ni shule chache tu za binafsi zitabakia kutokana na maboresho hayo makubwa yakiwemo ya kukarabati shule kongwe. Matokeo ya Kidato cha VI mwaka 2018, ni mwanzo tu wa "changing of guard" kati ya shule za umma dhidi ya za binafsi.

Mnyonge mnyongeni haki yake mwachie. Iliyokwishayafanya ni mengi mno kwenye sekta ya elimu na afya, wote tunaona.
Huu uchumi wa kati Objective yake ni nini? Ni nani walengwaa wa uchumi wa kati? Kama ni watanzani, waziri na serikali yake wanajidanganya. Wananchi hawajahamasishwa. Wananchi hawashirikishwi. Wananchi wamejaa manung'uniko na simanzi mioyoni. Wananchi wana maisha magumu sana. Nachelea Mheshimiwa Jaffo kana anasomaga makala zetu atambue kuwa, uchumi wa kati ni ndoto ya viongozi wa Tanzania. Ndoto yao ingekamilika kama pangekuwa na uongozi thabiti kuliko utawala. Maana kwenye utawala **** bwana na mtwana. Watanzania tumebakia watwana kwenye nchi yetu. Kazi ya mtwana no kupokea amri ya bwana wake. Mtwana anafanya kazi kwa kusimamiwa, na kama msimamizi kaondoka, ile kazi haifanyiki kwa kuwa ni kazi ya Bwana.
 
View attachment 845756

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. Selemani Jafo, akiwa anaongea kwenye kipindi cha Tunatekeleza cha TBC, saa 6 mchana, amesifia kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuibadilisha Tanzania kuelekea katika uchumi wa kati na kwamba kwa kasi hiyo, "Watu watakuja kujifunza juu ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano."
Jafo alitoa takwimu kadhaa zinazoonyesha mabadiliko makubwa yaliyofanywa ndani ya kipindi kifupi tangu Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli iingie madarakani mwaka 2015. Baadhi ya mambo aliyoongelea kwenye sekta za Afya na Elimu ni yafuatayo:
  • Sekta ya Afya: Tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961 hadi mwaka 2015, kulikuwepo Vituo vya Afya 515, kati ya hivyo, vinavyotoa huduma za upasuaji 115 pekee lakini ndani ya miaka miwili na nusu, Vituo vya huduma ya upasuaji vimeongezeka na kufikia 204, sawa na ujenzi wa vituo 89 ndani ya miaka miwili pekee. Alisema kuwa, wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani, kulikuwepo hospitali 72 pekee katika jumla ya Halmashauri 184 nchini lakini ndani ya Bajeti ya mwaka huu wa 2018/2019 pekee, Serikali itajenga hospitali 63 huku Vituo vya afya 67 vikiwa vinajengwa Nchi nzima.
  • Elimu Msingi Bila Malipo: Kumekuwepo kasi kubwa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, maabara na madawati kwa ajili ya kukidhi ongezeko kubwa la wanafunzi. Alitolea mfano wa Shule ya Msingi Maji Matitu, jijini Dar es Salaam, iliyokuwa imepanga mwaka 2017 kusajili (maotea) wanafunzi 260 lakini ilijikuta ikisajili wanafunzi 1026!! Vilevile, upatikanaji wa vitabu umeongezeka kutoka wanafunzi 8 kwa kitabu hadi wanafunzi 3 kwa kitabu.
Waziri Jafo aliongelea pia jitihada za Serikali katika Sera ya viwanda kwa kila Mkoa, ujenzi wa barabara chini ya TARURA, pamoja na miradi ya maji, shule etc.

Waziri aliwakumbusha Wakurugenzi wa Halmashauri juu ya wajibu wao katika kuharakisha maendeleo kwenye maeneo yao na "kuwaonya Wakurugenzi wasioendana na kasi ya Serikali wasione ajabu wakiondolewa kwenye nafasi zao na wasitafute mchawi kuwa, sijui wamerogwa bali ni utendaji kazi wao."
Jafo alidai kuondolewa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Kigoma Mjini, Pangani na Nkasi ni kutokana na kutoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Jafo akiwa kwenye Kikao na Wadau wa Elimu nchini jijini Mwanza, mwaka 2017, alitabiri mabadiliko makubwa katika performance ya shule za Serikali kulinganisha na za binafsi kwa sababu ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali kwa shule zake, ikiwemo kujenga maabara za sayansi, kuondoa ada, kusambaza vitabu, kutengeneza madawati, kuongeza vyumba vya madarasa na kuajiri walimu wengi mpaka kufikia mahitaji ya walimu wa Arts kutosheleza kabisa. Aliwaambia wadau kuwa, ana uhakika ni shule chache tu za binafsi zitabakia kutokana na maboresho hayo makubwa yakiwemo ya kukarabati shule kongwe. Matokeo ya Kidato cha VI mwaka 2018, ni mwanzo tu wa "changing of guard" kati ya shule za umma dhidi ya za binafsi.

Mnyonge mnyongeni haki yake mwachie. Iliyokwishayafanya ni mengi mno kwenye sekta ya elimu na afya, wote tunaona.

Ni utendaji kazi upi USIOINUA uchumi mtu atakuja kujifunza?
 
View attachment 845756

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mh. Selemani Jafo, akiwa anaongea kwenye kipindi cha Tunatekeleza cha TBC, saa 6 mchana, amesifia kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuibadilisha Tanzania kuelekea katika uchumi wa kati na kwamba kwa kasi hiyo, "Watu watakuja kujifunza juu ya utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano."
Jafo alitoa takwimu kadhaa zinazoonyesha mabadiliko makubwa yaliyofanywa ndani ya kipindi kifupi tangu Serikali ya Awamu ya Tano, chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli iingie madarakani mwaka 2015. Baadhi ya mambo aliyoongelea kwenye sekta za Afya na Elimu ni yafuatayo:
  • Sekta ya Afya: Tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961 hadi mwaka 2015, kulikuwepo Vituo vya Afya 515, kati ya hivyo, vinavyotoa huduma za upasuaji 115 pekee lakini ndani ya miaka miwili na nusu, Vituo vya huduma ya upasuaji vimeongezeka na kufikia 204, sawa na ujenzi wa vituo 89 ndani ya miaka miwili pekee. Alisema kuwa, wakati Serikali ya Awamu ya Tano inaingia madarakani, kulikuwepo hospitali 72 pekee katika jumla ya Halmashauri 184 nchini lakini ndani ya Bajeti ya mwaka huu wa 2018/2019 pekee, Serikali itajenga hospitali 63 huku Vituo vya afya 67 vikiwa vinajengwa Nchi nzima.
  • Elimu Msingi Bila Malipo: Kumekuwepo kasi kubwa ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, maabara na madawati kwa ajili ya kukidhi ongezeko kubwa la wanafunzi. Alitolea mfano wa Shule ya Msingi Maji Matitu, jijini Dar es Salaam, iliyokuwa imepanga mwaka 2017 kusajili (maotea) wanafunzi 260 lakini ilijikuta ikisajili wanafunzi 1026!! Vilevile, upatikanaji wa vitabu umeongezeka kutoka wanafunzi 8 kwa kitabu hadi wanafunzi 3 kwa kitabu.
Waziri Jafo aliongelea pia jitihada za Serikali katika Sera ya viwanda kwa kila Mkoa, ujenzi wa barabara chini ya TARURA, pamoja na miradi ya maji, shule etc.

Waziri aliwakumbusha Wakurugenzi wa Halmashauri juu ya wajibu wao katika kuharakisha maendeleo kwenye maeneo yao na "kuwaonya Wakurugenzi wasioendana na kasi ya Serikali wasione ajabu wakiondolewa kwenye nafasi zao na wasitafute mchawi kuwa, sijui wamerogwa bali ni utendaji kazi wao."
Jafo alidai kuondolewa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Kigoma Mjini, Pangani na Nkasi ni kutokana na kutoendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Jafo akiwa kwenye Kikao na Wadau wa Elimu nchini jijini Mwanza, mwaka 2017, alitabiri mabadiliko makubwa katika performance ya shule za Serikali kulinganisha na za binafsi kwa sababu ya maboresho makubwa yaliyofanywa na Serikali kwa shule zake, ikiwemo kujenga maabara za sayansi, kuondoa ada, kusambaza vitabu, kutengeneza madawati, kuongeza vyumba vya madarasa na kuajiri walimu wengi mpaka kufikia mahitaji ya walimu wa Arts kutosheleza kabisa. Aliwaambia wadau kuwa, ana uhakika ni shule chache tu za binafsi zitabakia kutokana na maboresho hayo makubwa yakiwemo ya kukarabati shule kongwe. Matokeo ya Kidato cha VI mwaka 2018, ni mwanzo tu wa "changing of guard" kati ya shule za umma dhidi ya za binafsi.

Mnyonge mnyongeni haki yake mwachie. Iliyokwishayafanya ni mengi mno kwenye sekta ya elimu na afya, wote tunaona.
Cha kujivunia kitu gani ambacho kitakuwa mfano kwa watu wa mataifa wanje waje wajifunze kwetu ni kipi? JE wangekuwa wanatulipia mahari kama Libya ingekuwaje? usipende sasa kusifiwa kwani mwisho wake ni kubri na kujiona Mungu mtu kwa vitu ambavyo kichwa wala miguu. Hata ukifanya ni sawa kwani ni haki yako ya kikatiba kutoa huduma kwa wapigakura wako ambao walikuchagua kipindi cha uchaguzi.
 
Yaani nchi zingine wake wajifunze kutoka kwetu , maajabu haya maana Havana wa Kenya baada sakata la kuchomwa vifaranga ,alisema kuna kiongozi hafai hata kuwa mwenyekiti wa kijiji .
 
Waje kujifunza kazi ya kuzuia Siasa wakati Katiba na Sheria zetu zinaruhusu...basi sawa!!
 
Back
Top Bottom