Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,968
- 20,120
Waziri wa Fedha wa Russia leo ameupinga mpango wa Waziri Mkuu Vladimir Putin wa kumfanya Rais Dmitry Medvedev kuwa waziri mkuu wake iwapo atarudi tena Kremlin - Ikulu ya Russia,kwa kusema kwamba hatoitumikia serikali mpya.
Wawekezaji wa kigeni wamekuwa na wasi wasi na dharao hiyo ya Alexei Kudrin baada ya Putin kutangaza kwamba atagombea urais katika uchaguzi wa mwezi Machi mwakani ambao utaufikisha utawaka wake hadi mwka 2024.
Kudrin ambaye ni mshirika wa Putin amekuwa na tamaa ya kuwa waziri mkuu na amesema amekuwa na tafauti zake na Medvedev ambaye hivi sasa itabidi aonyeshe uwezo wake atakapokuwa waziri mkuu baada ya kulazimishwa na Putin kuachana na ndoto yake ya kuwa rais kwa kipindi cha pili.
Kudrin mwenye umri wa miaka 50 amesema hajioni kuwemo katika serikali mpya, kauli yake hiyo ameitowa mjini Washington Marekani ambapo amekuwa akikutana na watengeza sera wa kimataifa.***
Wawekezaji wa kigeni wamekuwa na wasi wasi na dharao hiyo ya Alexei Kudrin baada ya Putin kutangaza kwamba atagombea urais katika uchaguzi wa mwezi Machi mwakani ambao utaufikisha utawaka wake hadi mwka 2024.
Kudrin ambaye ni mshirika wa Putin amekuwa na tamaa ya kuwa waziri mkuu na amesema amekuwa na tafauti zake na Medvedev ambaye hivi sasa itabidi aonyeshe uwezo wake atakapokuwa waziri mkuu baada ya kulazimishwa na Putin kuachana na ndoto yake ya kuwa rais kwa kipindi cha pili.
Kudrin mwenye umri wa miaka 50 amesema hajioni kuwemo katika serikali mpya, kauli yake hiyo ameitowa mjini Washington Marekani ambapo amekuwa akikutana na watengeza sera wa kimataifa.***