Waziri wa Fedha: Nchi inapita kwenye kipindi kigumu, wafadhili wamepunguza misaada

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Serikali yakiri misaada imepungua.

=======

Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Phillip Mpango amesema nchi inapita kwenye kipindi kigumu kidogo kutokana na wafadhili kupungua kutoa misaada.

Kufuatia hali hiyo, amewataka wanaokusanya mapato kuhakikisha wanasimamia kwa nguvu zote ukusanyaji mapato.

Dk.Mpango ametoa kauli hiyo leo katika Mkutano kati ya Wizara hiyo na Watoa huduma za Serikali katika kukusanya mapato uliofanyika Jijini hapa.

Amesema nchi inapitia katika kipindi kigumu kutokana na wafadhili kupunguza kutoa misaada na wanaotoa misaada pia imekuwa na masharti mengi ya hovyo.

Ameelezwa miongoni mwa masharti hayo ambayo wafadhili wamekuwa wakiyatamka bila aibu kuwa ni wanaopokea misaada hiyo wakubali tabia ya ushoga kitu ambacho nchi haiwezi kukubaliana na masharti hayo.
MY TAKE:

1. Kwanini serikali inataja sharti moja tu la ushoga na kuacha masharti mengine yenye tija kama utawala bora, kufifia kwa demokrasia nchini, wanafunzi wanaopata mimba, sheria ya takwimu, kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na ukiukwaji wa haki za binadamu?

2. Kama misaada imepungua kwanini tunalazimisha kuendesha miradi mingi mikubwa kwa wakati mmoja.

CHANZO: Mpango: "Nchi inapita kwenye kipindi kigumu"
 
Huyu naye keshaanza kutulisha visivyostahili!

Sijawahi kutokumuamini mwalimu wangu kwa lolote walilonifundisha kwani hawafundishi uongo! Lakini leo mwalimu mbobevu na mchungaji anachagua maneno ya kunifunza na kuyaacha yale ya msingi!

Nasikitika kwa kweli kwani hakuna msaada duniani wenye sharti moja tu. Ayataje masharti yote tuyachuje wenyewe! Anavyotubagulia ayatakayo haipendezi. Aseme na masharti mengine yote.
 
Hilo la ushoga wameliona ni kama sababu muhimu kwa sababu kuna baadhi ya wananchi tunajifanya tumekolewa na dini alizozileta huyo huyo mzungu.

Ila karibia barua zote kutoka nchi zilizomkazia mkuu wetu zinataja sababu nyingi sana ikiwemo hizo ambazo hawazimention wakuu wetu kwenye speech zao.
 
"serikali yangu inapesa"

Haya zile za stiglers zichezeshwe ziingie kwenye matumizi tmya sirikali halafu hayo mambo ya stiglerz tutajua huko huko mbele kwa mbele..

Tuombe Mungu isije tukaambiwa "jamani kwa sasa hatuna hela kwaajili ya uchaguzi tukusanyekusanye kwanza miaka mitatu ndo tufanye uchaguzi".

Unatunisha msuli wakati upaja mdogo.
 
Mmhhh yaani ushoga ndio imekuwa kichaka cha kujifichia. Lakini tuulizane. Mbona hata kabla ya ushoga bado walikuwa wanajitoa au hapo sababu ilikuwa ni nini?

Nakumbuka speech ya aliyekuwa waziri wa viwanda pale bungeni. Kuna mambo aliyaongea kama kodi na ajira mpya... naamini hiyo speech ndio ilikuwa sababu ya yeye kutumbuliwa...
 
"serikali yangu inapesa"

Haya zile za stiglers zichezeshwe ziingie kwenye matumizi tmya sirikali halafu hayo mambo ya stiglerz tutajua huko huko mbele kwa mbele..

Tuombe Mungu isije tukaambiwa "jamani kwa sasa hatuna hela kwaajili ya uchaguzi tukusanyekusanye kwanza miaka mitatu ndo tufanye uchaguzi".

Unatunisha msuli wakati upaja mdogo.
😁😁😁
 
Ushoga ni sehemu ndogo tu ya swala kubwa la ukiukwaji wa hali za binadamu ktk Utawala huu.

Ili kuhalalisha udhalimu wao wanasingizia ushoga wakati tunajua kuwa wapo viongozi waandamizi ambao ni mashoga.

Hawataki kuongelea udikteta uchwara wa ushamba wa wafuasi wa kagame
 
Serikali yakiri misaada imepungua.

Waziri wa Fedha na Mipango Dr. Phillip Mpango amesema nchi inapita kwenye kipindi kigumu kidogo kutokana na wafadhili kupungua kutoa misaada.

Kufuatia hali hiyo amewataka wanaokusanya mapato kuhakikisha wanasimamia kwa nguvu zote ukusanyaji wa mapato.

"Nchi inapita kwenye kipindi kigumu kidogo kutokana na wafadhili kupungua kutoa misaada na wanaotoa misaada pia imekuwa na masharti mengi ya hovyo".

Dr. Mpango ametoa kauli hiyo leo kwenye mkutano wa wizara hiyo na watoa huduma wa serikali katika kukusanya mapato uliofanyika jijini.

Ameelezwa miongoni mwa masharti ambayo wafadhili wamekuwa wakiyatamka bila aibu kuwa wanaopokea misaada hiyo wakubali tabia ya ushoga kitu ambacho nchi yetu haiwezi kukubali.

MY TAKE:

Kwanini serikali inataja sharti moja tu la ushoga na kuacha masharti mengine yenye manufaa kama utawala bora, kufifia kwa demokrasia nchini, wanafunzi wanaopata mimba, sheria ya takwimu, kuzuia mikutano ya vyama vya siasa na ukiukwaji wa haki za binadamu?

Mpango: "Nchi inapita kwenye kipindi kigumu"
Kwani ni lini wafadhili waliongeza misaada!
 
Back
Top Bottom