Waziri wa Elimu tunahitaji msaada wako

kichwa2020

New Member
Feb 21, 2020
1
3
Kumetokea tatizo kubwa kwa wamiliki wa shule binafsi Jijini Dar es Salaam mfano Royal Elite Primary School, Anazak Primary School etc kulazimisha watoto wa shule za msingi darasa la mitihani namaanisha darasa la nne na darasa la saba kukaa boarding bila ya ridhaa ya wazazi. Inakuwa ni bila ya ridhaa ya wazazi kwa sababu mazingira unayowekewa na mwenye shule unajikuta huna uwezo wa kukataa hata kama hautaki mtoto wako akae boarding.

Kwanza mwaka wa mtihani hauwezi kumuhamisha mtoto maana anakuwa ameisha sajiliwa na hii taarifa ya kukaa boarding unapewa akiingia tu darasa hilo la mtihani. Pili muda ambao wanataka umlete mtoto shule na muda wa kumchukua unakuwa ni mgumu kuweza kufanya hivyo.

Wanataka watoto wa darasa la mtihani kuanza masomo saa kumi na mbili asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni. Hivyo umlete mtoto shuleni kabla ya saa kumi na mbili asubuhi na umfuate shuleni baada ya saa kumi na mbili jioni. Hii haiko sawa kabisa kwa sababu mwanzo unampeleka mtoto kwenye shule hii hapakuwepo makubaliano ya kwamba mtoto atakaa boarding darasa la nne au la saba.

Shule hizi zinafanya hivi kwa manufaa yao binafsi na huku zikimuumiza mtoto. Kwanza wanawakalilisha watoto masomo ili waweze kupata A nyingi ambazo zitaonyesha shule ina ufaulu wa juu na hii inawasaidia wenye shule kupata wanafunzi wengi na fedha zaidi.

Vile vile kuwaweka boarding watoto, shule inapata fedha zaidi maana mzazi unalipia hiyo huduma ya boarding. Hii haiku sawa maana mtoto wa darasa la nne kuwa darasani masaa 12 sio vizuri kwa afya yake na uwezo wake wa kujifunza ni mdogo sana kwa umri huo.

Wazazi hatutaki hizo A za kuumiza akili ya mtoto. Mtoto wa miaka 8 na 9 ana muda wake kiafya wa kupumzika na madhala yake tunaweza tusiyaone sasa lakini baadae ni makubwa sana.

Kuna wazazi wanaotaka watoto wao wakae boarding ni sawa lakini kuna wengine hatutaki lakini unalazimishwa na masharti tunayowekewa na mwenye shule. Ingekuwa vizuri kama shule imesajiliwa kama boarding na mzazi tangu mwanzo anajua hilo na anakubaliana nalo ila hali haiko hivyo. Vilevile unakuta shule in matron mmoja wakuangalia watoto zaidi ya mia (100) ambao miaka yao ni kati ya 8 na 9.

Wengine hata namna ya kuangalia usafi wao bado. Matron mwenyewe hana mafunzo yoyote ya kuangalia watoto unakuta ni ndugu wa mwenye shule amepewa tu kazi ya umatron. Hakuna nurse wa kuangalia hawa watoto, mtoto akiumwa matron amepewa maelekezo ampe tu Panadol au akikohoa apewe kofta. Watoto hawa ni wadogo kwa umri haifai tuwatesa kwa ajili ya manufaa ya wenye shule.

Mwenye shule anacho angalia ni kupata pesa na kupata wanafunzi wengi tu. Waziri tusaidie utoe mwongozo kwenye hili. Muda wa kuanza masomo shule za msingi uwe unajulikana ni saa ngapi na unaisha saa ngapi ili kuondoa watu wenye tamaa kutuumizia watoto.
 
WHEN IT COMES TO EDUCATION ESPECIALLY IN THIS ERA, IT IS MUCH BETTER MY KIDS TO SPENT DAY AND NIGHTS IN SCHOOL RATHER THAN AT HOME, BECAUSE AT HOME THE ENVIRONMENT AT HOME IS NOT CONDUCIVE TO MY KIDS TO STUDY AND READ THEIR BOOKS.

I WANT MY KIDS TO BE BOOKWORMS HASWA TENA HASWA WHEN IT COMES TO EDUCATION...HATA KAMA ANA MIAKA 3 AKAE TU BOARDING.
 
Mtoto lazima apate muda wa kupumzika na kucheza.
WHEN IT COMES TO EDUCATION ESPECIALLY IN THIS ERA, IT IS MUCH BETTER MY KIDS TO SPENT DAY AND NIGHTS IN SCHOOL RATHER THAN AT HOME, BECAUSE AT HOME THE ENVIRONMENT AT HOME IS NOT CONDUCIVE TO MY KIDS TO STUDY AND READ THEIR BOOKS. I WANT MY KIDS TO BE BOOKWORMS HASWA TENA HASWA WHEN IT COMES TO EDUCATION...HATA KAMA ANA MIAKA 3 AKAE TU BOARDING.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kitu nachukia kama hii

Mtoto wa darasa la nne kukaa boarding

Tena kwa lazima......

Qizara iingilie kati hizi shuke zinazolaImisha.

Chanzo hapa ni kutafuta muda zaidi wa kuwakaririsha watoto tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Foji cheti cha hospital kwamba mtoto anahitaji clinic kila siku.
 
Hujasoma bweni ndugu, kwa sasa bweni si mahala salama kwa watoto..
WHEN IT COMES TO EDUCATION ESPECIALLY IN THIS ERA, IT IS MUCH BETTER MY KIDS TO SPENT DAY AND NIGHTS IN SCHOOL RATHER THAN AT HOME, BECAUSE AT HOME THE ENVIRONMENT AT HOME IS NOT CONDUCIVE TO MY KIDS TO STUDY AND READ THEIR BOOKS.

I WANT MY KIDS TO BE BOOKWORMS HASWA TENA HASWA WHEN IT COMES TO EDUCATION...HATA KAMA ANA MIAKA 3 AKAE TU BOARDING.

Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
 
Hujasoma bweni ndugu, kwa sasa bweni si mahala salama kwa watoto..


Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
Mazingira yanabadilika!

Bweni za watoto zina mazingira mazuri na salama tofauti na bweni zenu zile za kayumba school!

Usifananishe visivyofanana.
 
Kumetokea tatizo kubwa kwa wamiliki wa shule binafsi Jijini Dar es Salaam mfano Royal Elite Primary School, Anazak Primary School etc kulazimisha watoto wa shule za msingi darasa la mitihani namaanisha darasa la nne na darasa la saba kukaa boarding bila ya ridhaa ya wazazi. Inakuwa ni bila ya ridhaa ya wazazi kwa sababu mazingira unayowekewa na mwenye shule unajikuta huna uwezo wa kukataa hata kama hautaki mtoto wako akae boarding.

Kwanza mwaka wa mtihani hauwezi kumuhamisha mtoto maana anakuwa ameisha sajiliwa na hii taarifa ya kukaa boarding unapewa akiingia tu darasa hilo la mtihani. Pili muda ambao wanataka umlete mtoto shule na muda wa kumchukua unakuwa ni mgumu kuweza kufanya hivyo.

Wanataka watoto wa darasa la mtihani kuanza masomo saa kumi na mbili asubuhi mpaka saa kumi na mbili jioni. Hivyo umlete mtoto shuleni kabla ya saa kumi na mbili asubuhi na umfuate shuleni baada ya saa kumi na mbili jioni. Hii haiko sawa kabisa kwa sababu mwanzo unampeleka mtoto kwenye shule hii hapakuwepo makubaliano ya kwamba mtoto atakaa boarding darasa la nne au la saba.

Shule hizi zinafanya hivi kwa manufaa yao binafsi na huku zikimuumiza mtoto. Kwanza wanawakalilisha watoto masomo ili waweze kupata A nyingi ambazo zitaonyesha shule ina ufaulu wa juu na hii inawasaidia wenye shule kupata wanafunzi wengi na fedha zaidi.

Vile vile kuwaweka boarding watoto, shule inapata fedha zaidi maana mzazi unalipia hiyo huduma ya boarding. Hii haiku sawa maana mtoto wa darasa la nne kuwa darasani masaa 12 sio vizuri kwa afya yake na uwezo wake wa kujifunza ni mdogo sana kwa umri huo.

Wazazi hatutaki hizo A za kuumiza akili ya mtoto. Mtoto wa miaka 8 na 9 ana muda wake kiafya wa kupumzika na madhala yake tunaweza tusiyaone sasa lakini baadae ni makubwa sana.

Kuna wazazi wanaotaka watoto wao wakae boarding ni sawa lakini kuna wengine hatutaki lakini unalazimishwa na masharti tunayowekewa na mwenye shule. Ingekuwa vizuri kama shule imesajiliwa kama boarding na mzazi tangu mwanzo anajua hilo na anakubaliana nalo ila hali haiko hivyo. Vilevile unakuta shule in matron mmoja wakuangalia watoto zaidi ya mia (100) ambao miaka yao ni kati ya 8 na 9.

Wengine hata namna ya kuangalia usafi wao bado. Matron mwenyewe hana mafunzo yoyote ya kuangalia watoto unakuta ni ndugu wa mwenye shule amepewa tu kazi ya umatron. Hakuna nurse wa kuangalia hawa watoto, mtoto akiumwa matron amepewa maelekezo ampe tu Panadol au akikohoa apewe kofta. Watoto hawa ni wadogo kwa umri haifai tuwatesa kwa ajili ya manufaa ya wenye shule.

Mwenye shule anacho angalia ni kupata pesa na kupata wanafunzi wengi tu. Waziri tusaidie utoe mwongozo kwenye hili. Muda wa kuanza masomo shule za msingi uwe unajulikana ni saa ngapi na unaisha saa ngapi ili kuondoa watu wenye tamaa kutuumizia watoto.
Mkuu umeongea point sana. La ajabu Wizara ya Elimu inapata taarifa hizi lakini hawachukui hatua. Vilio hivi vya wazazi kuhusu shule kuamua kulazimisha watoto kukaa boarding bila sababuna kuwabebesha watoto mzigo wa takataka wanazoita elimu eti wanattafuta A's.

Sababu kubwa ni kutaka kuwaibia tu wazazi pesa huku wakiumiza watoto pia. Matokeo yake ni kutengeneza kizazi chenye akili za kukaririshwa kama robot kisicho na fikra binafi kwa sababu bongo zilikosa muda wa kukua na kupumzika hivyo zikadumaa.

Vilio hivi ni vingi na kwa kweli Wizara ya Elimu ndio inalea tatizo hili sugu. Bila shaka ni wanufaika namba moja au namba mbili.

Haiwezekana malalamiko mengi hivi yafumbiwe macho na kuziba masikio kama Wizara hawafaidiki kibinafsi.

Huu ni wakati mwakafaka kuchukua hatua ikiwa ni pamoja na kufuta ulazima wa boarding kwa Darasa la Nne na la Saba. Mzazi atakayependa kupeleka mtoto wake borading awe huru kufanya hivyo bila kuathiri wengine.

Mheshimiwa Rais wewe ni msikivu wa vilio vya wasio na sauti ninakuomba sasa wewe mweneywe uchukue hatua sitahiki kunusuru watoto na wazazi wa taifa hili.
 
Back
Top Bottom