Waziri Muhongo ni muongo?

Waziri Muhongo ni muongo?

mwinukai

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2011
Posts
1,447
Reaction score
630
Licha ya kusema bungeni kuwa suala la mgao wa umeme ni HALIKUBALIKI lakini sas naona limeanza kukubalika kutokana na mgao wa umeme ambao hautangazwi bila shaka ni kwa lengo la kuficha aibu, Je mgao wa umeme kurudi kinyemela hii haimanishi kuwa WAZIRI MUHONGO NI MUONGO?
 
Mafisadi wanamhujumu ili aonekane muongo. Usicheze na wenye pesa!!!!!
 
Wanafanya kila hila kumuhujumu ili aonekane hafai; laki kwa vile tumemtanguliza MUNGU watashindwa tu!!
 
Licha ya kusema bungeni kuwa suala la mgao wa umeme ni HALIKUBALIKI lakini sas naona limeanza kukubalika kutokana na mgao wa umeme ambao hautangazwi bila shaka ni kwa lengo la kuficha aibu, Je mgao wa umeme kurudi kinyemela hii haimanishi kuwa WAZIRI MUHONGO NI MUONGO?

wewe ndo mwoongo tumuache proff afanye kazi yake umeme kukatika ni miundombinu mibovu tuuu!
KUMBUKENI MLIKOTOKA BANA, MWAKA JANA KAMA LEO HII MGAO NI MKUBWA SANA!
 
Acha post za kinafiki! Mpeni prof nafasi afanye kazi.

Bila shaka magamba yamemzunguka aonekane hafai, ingawa amejimbanua tayari kuwa ana uchungu na wananchi.

Mtu huyu, ni sawa ni yule aliyeomba akumbukwe katika ufalme ujao.

Prof, wakikuboa, rudi kafundishe. Utaitendea vema nchi yako kwa kusimama imara. Utakumbukwa.
 
Waongo ni Mhando, Mboma, wenye mikataba isiyo na tija kwa Taifa (Symbion) na majenereta yao pamoja na mafisadi walionyimwa tenda ya kuuzia Tanesco mafuta kwa bei ya juu maana kama tuna uwezo wa kufua umeme kuliko hitaji la Taifa, mgao utakubalikaje? Sisi tunakubali kukatika umeme (kwa muda mfupi tu) kabla ya marekebisho kutokana na miundo-mbinu chakavu lakini hatukubali migao. Ukikubali mgao hukosi miongoni mwa makundi tajwa hapo juu au wafaidika na mfumo huo! Wizara ikishindwa kuwakabili kwa hujuma zenu, nguvu ya umma itawaonyesha adabu na majenereta yenu mliyorithishana toka Richmond!
 
Toa upuuzi hapa. Inamaana serikali inazidiwa nguvu na mafisadi, basi si bora tuwape nchi watuongoze wao.

Mkuu serikali yako inayongozwa na legelege JK ni serikali DHAIFU, wala hauitaji kupigwa fimbo ili uelewe... Wanachojua viongozi wako ni lini anatakiwa aende kubadili damu...
 
Mkuu serikali yako inayongozwa na legelege JK ni serikali DHAIFU, wala hauitaji kupigwa fimbo ili uelewe... Wanachojua viongozi wako ni lini anatakiwa aende kubadili damu...

Kwa maana hiyo KPI ya Muhongo usitegemee kuwa bora ktk mazingira ya mambo LEGELEGE!
 
Haitakuwa ajabu kwa Muhongo kuwa mwongo maana ni bonge la TISS!!

Moja wapo ya sifa ya kuwa TISS, ni lazima uwe mwongo. Mwanagalie JK, Kikula wa UDOM, n.k.
 
Toa upuuzi hapa. Inamaana serikali inazidiwa nguvu na mafisadi, basi si bora tuwape nchi watuongoze wao.
Unaweza kufikisha ujumbe bila hata kutukana. Hili la mafisadi kuwa na nguvu kuliko serikali ya kikwete halina ubishi kwani hata Pinda aliwahi kukiri hivyo.
 
Unaweza kufikisha ujumbe bila hata kutukana. Hili la mafisadi kuwa na nguvu kuliko serikali ya kikwete halina ubishi kwani hata Pinda aliwahi kukiri hivyo.

Nimetukana wapi? Hii sio serikali ya kikwete ni serikali yetu, Kikwete ni mtu mdogo sana kwenye serikali yetu, kama tukiamua hata leo hawezi kuitwa rais tena, kwa hiyo mnapotokea na kutoa maneno ya kufedhehesha namna hii mimi binafsi ninachukia sana.

Ukifuatilia msingi za wanaosema Muhongo anafanywa nini sijui na mafisadi utagundua kwamba wanatembea na hoja ile ile ya Kikwete ni imara ila mawaziri wake ndio wanamuangusha, waziri mzima mambo yaliyo ndani ya mamlaka yake yanahujumiwa vipi na mtu wa namna yoyote ile? Kama ni hujuma wanahujumiana wao kwa wao, ccm wanatuhujumu watanzania, hakuna fisadi asiye mwanaccm nchini hii, kwa kifupi uwezo mzima wa ccm kusimamia serikali umedhoofika sana, hatuhutaji kusikia kisingizio chochote kile, na matusi ni haki yao washenzi hawa.
 
Nimetukana wapi? Hii sio serikali ya kikwete ni serikali yetu, Kikwete ni mtu mdogo sana kwenye serikali yetu, kama tukiamua hata leo hawezi kuitwa rais tena, kwa hiyo mnapotokea na kutoa maneno ya kufedhehesha namna hii mimi binafsi ninachukia sana.

Ukifuatilia msingi za wanaosema Muhongo anafanywa nini sijui na mafisadi utagundua kwamba wanatembea na hoja ile ile ya Kikwete ni imara ila mawaziri wake ndio wanamuangusha, waziri mzima mambo yaliyo ndani ya mamlaka yake yanahujumiwa vipi na mtu wa namna yoyote ile? Kama ni hujuma wanahujumiana wao kwa wao, ccm wanatuhujumu watanzania, hakuna fisadi asiye mwanaccm nchini hii, kwa kifupi uwezo mzima wa ccm kusimamia serikali umedhoofika sana, hatuhutaji kusikia kisingizio chochote kile, na matusi ni haki yao washenzi hawa.

Mkuu, upo sahihi na wala hujatukana mtu, hiyo ndo lugha pekee iliyobaki ya kuwaambia hawa MAFISADI, MAJAMBAZI na WANYANG'ANYI wanaliibia taifa la Tanzania mchana kweupe huku viyoyozi vikiwapepea. kwa kweli mkuu hawa ccm ni WASHENZI, sio kuwatukana ila ndo sifa wanayostahili. we ngoja kiama chao kinakaribia, ngoja tuwaamshe wananchi waamke wajue umuhimu wa KULINDA KURA.
 
duara ni lile lile ukijichanganya na wachafu utachafuka tu !
Prof. Endelea na style yako SHOKA 1 MBUYU CHINI.
 
Toa upuuzi hapa. Inamaana serikali inazidiwa nguvu na mafisadi, basi si bora tuwape nchi watuongoze wao.

Sanagarara elewa kwamba mafisadi wapo ndani ya serikali pia na serikali kwa namna moja inawatetea! Kama hawana nguvu mbona serikali imeshindwa kuchukua hatua kuhusu vitendo vingi vya kifisadi km richmond, rada, EPA, deep green, meremeta nk? Ndugu ushauri wa bureee funguka!!!!!
 
Mkuu serikali yako inayongozwa na legelege JK ni serikali DHAIFU, wala hauitaji kupigwa fimbo ili uelewe... Wanachojua viongozi wako ni lini anatakiwa aende kubadili damu...

Kumbuka kiraja mkubwa wao aliwahi kusema mjengoni hatari ya hawa watu
 
Tusianze kumlaumu Prof Muhogo bali kumpa moyo. Kubadilisha mfumo uliokuwepo kwa zaidi ya miaka hamsini ni kazi kubwa. Tumpe muda angalau mwaka mmoja tuone. Bila shaka tutaridhishwa na kazi yake kama mafisadi hawatamhujumu.
Mbona serikali imeshindwa kutakeleza kauli mbiu yake ya Maisha bora kwa kila mtanzania kwa takribani miaka saba sasa? Watanzania tuache tabia ya kulalama na kunyooshea wengine vidole bila sababu za msingi.
 
....[/QUOTE]

Hakuna kitu kama hicho, serikali ndio imejisalimisha kwa mafisadi kwa maslahi binafsi ya viongozi, na sio kweli kwamba mafisadi wameizidi nguvu serikali, unataka kuniambia mafisadi wanaweza wakasema mchakato wa uandikaji katiba mpya usitishwe na ukasitishwa?

Na kama kweli unataka tukae hapa tufunguane kwamba mafisadi wameishinda serikali kuna mantiki gani sasa ya kutaka kukiondoa chama cha mapinduzi kuingoza serikali yetu.

sisi ndio serikali, watu tuliowapa dhamana ya kuiongoza serikali wametusaliti, alafu sielewi ni kitu gani kinawasukuma watu kutoa kauli zinazowatenganisha mafisadi na CCM, naona kama kuna hoja mfu inaota mizizi hapa.
 
wengi hamuelewi kinachoendelea mnaongea siasa tu kama za prof. muhongo muongo, bila kuwekeza kwenye uzalishaji wa umeme zaidi mgao upo pale pale, kwa hali ilivyo mgao hauepukiki subirini muone, watanzania manadanganyika kirahisi sana.
 
Back
Top Bottom