Waziri Mkuu afunguka TBC kuhusu mabomu Arusha

Waziri Mkuu afunguka TBC kuhusu mabomu Arusha

Gubuntu

Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
19
Reaction score
2
Nilipita jf na kuona wadau Jf mlivopata hasira kuhusu bunge leo kupigwa kapuni, sasa nampata Pinda Live TBC RADIO anafunguka na mwana wa mkulima kwa nia njema anasema epusha siasa ktk suala la Arusha
 
Haki itapatika na hakuna usanii wowote tuwe na imani vyombo vilivyo shiriki kuchunguza ni madhubuti na uoongozi wa FBI ni wakuaminika; Lakini at the mean timu TUENDELEE na shughuli zetu za kujenga Taifa.
 
akiwa na maana kuwa lililotokea arusha halihusiani na siasa? Sasa linahusiana na nini? Wamesema halihusiani na dini. Hebu hao fbi wamalize mapema kwani hawa ndugu wanatuchanganya vichwa
 
Haki itapatika na hakuna usanii wowote tuwe na imani vyombo vilivyo shiriki kuchunguza ni madhubuti na uoongozi wa FBI ni wakuaminika; Lakini at the mean timu TUENDELEE na shughuli zetu za kujenga Taifa.

Hapo nilipobold pananipa mashaka sana hususan uliposema hakuna usanii, ngoja nikuulize swali moja, tangu vuguvugu za milipuko ya mobomu, kuchomwa kwa majengo ya ibada na kuuwawa kwa baadhi ya viongozi wa dini, kuna mtu yeyote yule ambaye aliwahi kukamatwa na kutiwa hatiani kisha kuhukumiwa?

Nauunga mkono hoja yako ya kuendelea na shughuli za kujenga Taifa, ila niwakumbushe tu binafsi siamini na sintaamini huu uongozi kama uko makini mpaka nisikie wahusika halisi wamekamatwa na kuhukumiwa pasipo kificho au usanii wowote ule.

Na pia tunapoendelea na shughuli za kujenga taifa, tusibweteke, tufumbue macho kama wenzetu wa Kenya au Marekani. Raia yoyote ambaye hatumfahamu maeneo tunayoishi ni vyema kuwa naye makini, pengine na kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama (we have to play our part, hata kama hawatarespond on time) maana hatujui nani baina yetu anaweza kutushambulia. Ni vyema tukawa zaidi ya makini.
 
Naogopa kwenda kanisani....misikiti yenyewe iko salama
 
Hapo nilipobold pananipa mashaka sana hususan uliposema hakuna usanii, ngoja nikuulize swali moja, tangu vuguvugu za milipuko ya mobomu, kuchomwa kwa majengo ya ibada na kuuwawa kwa baadhi ya viongozi wa dini, kuna mtu yeyote yule ambaye aliwahi kukamatwa na kutiwa hatiani kisha kuhukumiwa?

Nauunga mkono hoja yako ya kuendelea na shughuli za kujenga Taifa, ila niwakumbushe tu binafsi siamini na sintaamini huu uongozi kama uko makini mpaka nisikie wahusika halisi wamekamatwa na kuhukumiwa pasipo kificho au usanii wowote ule.

Na pia tunapoendelea na shughuli za kujenga taifa, tusibweteke, tufumbue macho kama wenzetu wa Kenya au Marekani. Raia yoyote ambaye hatumfahamu maeneo tunayoishi ni vyema kuwa naye makini, pengine na kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama (we have to play our part, hata kama hawatarespond on time) maana hatujui nani baina yetu anaweza kutushambulia. Ni vyema tukawa zaidi ya makini.

Bw. HP nashukuru kupokea tambulisho lenye utata, Kwakuwa nina amini Ulimwengu kwa sasa ni mdogo Ujue kuwa tokeo hili na jambo hili limishafika majuu yaani kwa ICC na Human rights pamoja na wa Vaticans ambao walikuwepo na kuguswa na hofu juu ya balaa hili, sasa hao wamesha weka taswira na maelezo yote juu ya meza wana subiri matokeo tuu , ILI WAANZE kazi... nakuondoa shaka zaidi hakuna kigogo wa aina yote kukimbia " wapo wakuwamulika ". hata kama itachukuwa miaka lakini lazima atafikishwa kujibu mashitaka aliyoficha au kufunika.!! Pia maBalozi wapo kama mashuhuda hapa.
Nina kubaliana nawe kuhusu kuwa MAKINI na kushirikiana kikweli ili tulinde masilahi ya jamii. Bravo and Blessings kwa waTZ.
 
Naogopa kwenda kanisani....misikiti yenyewe iko salama

Uongozi dhaifu wa baba mwanaAsha umelifanya Taifa la Tanzania kuweza kuingiliwa kwa urahisi sana[ easily penetrated]. Imekuwa hivyo kwasababu ya mgawanyiko wa wananchi kwa misingi ya dini na hata makabila yao ambao huko nyuma haukuwepo.

Maadui wa nchi hii wakiwemo majirani zetu watatumia udhaifu wa kugawanyika kwa wananchi hasa kwa misingi ya dini kutuchonganisha kwa kufanya vitendo vya kiharamia kama vile kulipua mabomu kati yetu ili tufarakane sisi kwa sisis ili hali vitendo hivi vikifadhiliwa na watu wa nje!!

Nchi za Uganda na Kenya mara tu zilipopeleka majeshi yake Somalia kukabiliana na Al Sabaab, mabomu yalilipuliwa mjini Nairobi na mjini Kamapala. Sisi juzi majeshi yetu yameelekea DRC kupambana na M23 je tukianza kuona mabomu yanalipuliwa nchini mwetu kama ilivyotokea kule Arusaha kuna haja ya sisi kumtafuta MCHAWI wetu?
 
Haki itapatika na hakuna usanii wowote tuwe na imani vyombo vilivyo shiriki kuchunguza ni madhubuti na uoongozi wa FBI ni wakuaminika; Lakini at the mean timu TUENDELEE na shughuli zetu za kujenga Taifa.

Kama Pinda mwenyewe alishaanza USANII kwa kumsingizia tena mbele ya BUNGE TUKUFU Kijana Victor Ambrose muandesha bodaboda kwamba ndiye aliyerusha bomu kanisani, huku akikwepa kutaja majina ya watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa na POLISI, kwanini basi Mtu huyu (Pinda) sisi tumuamini in the first place?!

Pinda katika kadhia hii ameshakosa credibility kauli yake haiwezi kuaminiwa kamwe na Mtanzania yeyote yule anayeshughulisha UBONGO wake!
 
Sijajua kwanini jambo linalowahusu waislamu kunakuwa na woga wa kuliweka wazi.
 
Sijajua kwanini jambo linalowahusu waislamu kunakuwa na woga wa kuliweka wazi.

mkuu wewe siunatumia id ya kificho kama unalijua vizuri liweke wazi wewe kwa sababu taarifa ya awali iliahatolewa na uchunguzi unaendelea sijui unataka uwazi gani.
 
akiwa na maana kuwa lililotokea arusha halihusiani na siasa? Sasa linahusiana na nini? Wamesema halihusiani na dini. Hebu hao fbi wamalize mapema kwani hawa ndugu wanatuchanganya vichwa

Wanajitahidi kujenga hoja ya kupotosha UDINI kwa vile wanajuwa kwamba wao ndio WAASISI wa UDINI. Wanajuwa Mh. Lema ana kila kitu kudhibitisha UDINI wao, hivyo lazima waanze kujenga HOJA MCHEPUKO ili kutu hadaa waTanganyika.

Bahati mbaya wamelewa madaraka na kuwa vipofu wa kila vituko wanavyo vifanya. Si umesikia na kuona Bungeni, anaye tukana matusi ya nguoni huitwa shujaa! Na anaye tetea maslahi ya waTanganyika huitwa Kichaa na Mchochezi!
 
Naogopa kwenda kanisani....misikiti yenyewe iko salama

Haha haa na uchungaji umeubwaga? Njoo twende tukatambike siye vimbangisye! Hizo imani zina wenyewe bana

_52566370_mudmen,wahgivalley.jpg
 
My friend! wacha kutoa Mapovu... uhamasishaji wa vurugu na uchu wa madaraka kwa njia mbali mbali ikiwepo ushirikishwaji wa nyumba za dini katika mambo ya kisiasa unatupeleka pabaya. Marekani na Kenya sio mifano Mizuri ya kufuata ...kwani hali si shwari katika nchi hizo kutokana na kugrade watu kutokana na races , Kabila na Dini zao... Finland, Sweden na Norway ni Nchi nzuri za kuigwa...
 
Nilipita jf na kuona wadau Jf mlivopata hasira kuhusu bunge leo kupigwa kapuni, sasa nampata Pinda Live TBC RADIO anafunguka na mwana wa mkulima kwa nia njema anasema epusha siasa ktk suala la Arusha

Hakuna anayeweza kufika huko lakini Hata nyerere alisema Maendeleo na amani vinaletwa na vitu 3 na akavitaja kuwa ni Siasa Safi, Uongozi bora na Raia wema. Sisi kwa tanzania bado nina imani kubwa sana na watanzania kuwa ni Raia wema ila katika sehemu hizo mbili zilizobaki nadhani ndio tatizo letu. Hata tufanye nini, Hata kwa kuwafungia watanzania mikutano ya Kisiasa kama hatuna uongozi bora na siasa safi (Ambazo haimanishi kutokuwa na mikutano ya kisiasa) Bado nchi hii tutaendelea kuthibitisha machafuko mengi.

Tena kama viongozi wetu ni wazalendo wa kutosha wangeweza kusema na kuthibitisha ubaya wa mikutano ya kisiasa kwa kusema wazi wakusanyika huwa wanafanya fujo au ni mtoa maada ndio huongea maneno ya kashafa kwa serikali na dawa yake ni Kuwasambaratisha wananchi waliokusanyika kwa mabomu ya machozi au ni kumkamata mtoa maada mchochezi.

Pia sipati picha itakuwaje kama ndio wanataka kupitisha sheria ya kuzuia mikutano ya kisiasa ambayo ndio silaha pekee iliyobaki nchini ya watanzania kuweza kufarijiwa na kuzungumza walionayo mioyoni mwao. Kwani wakikosa pa kuongelea hali ya kuwa wanaonewa hakuna haja hata ya research ni kwamba wataanza kufanya yale ya Mtwara na Lindi na Rufiji kwa wakulima na wafugaji. Na hapo viongozi wetu wa siasa watakuwa wamepata namna ya kuzuia machafuko nchini.
 
Back
Top Bottom