Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,770
- 1,173
- ๐๐๐ผ๐ฎ ๐บ๐ฎ๐ฎ๐ด๐ถ๐๐ผ ๐ธ๐๐ฎ ๐ช๐ถ๐๐ฎ๐ฟ๐ฎ ๐๐ฎ ๐๐ณ๐๐ฎ, ๐ ๐ฆ๐ ๐ป๐ฎ ๐ต๐ผ๐๐ฝ๐ถ๐๐ฎ๐น๐ถ ๐๐ผ๐๐ฒ ๐ป๐ฐ๐ต๐ถ๐ป๐ถ
- ๐ช๐ฎ๐ด๐ผ๐ป๐ท๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ถ๐ฝ๐ผ๐ป๐ด๐ฒ๐๐ฎ ๐ฆ๐ฒ๐ฟ๐ถ๐ธ๐ฎ๐น๐ถ ๐ธ๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฏ๐ผ๐ฟ๐ฒ๐๐ต๐ฎ ๐ต๐๐ฑ๐๐บ๐ฎ ๐๐ฎ ๐ฎ๐ณ๐๐ฎ
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.
Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. โ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.โ
Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.
Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. โUjauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.โ
Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi.
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.
โTunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri kama tupo hospitali za private (binafsi).โ Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.
-
- ๐ช๐ฎ๐ด๐ผ๐ป๐ท๐๐ฎ ๐๐ฎ๐ถ๐ฝ๐ผ๐ป๐ด๐ฒ๐๐ฎ ๐ฆ๐ฒ๐ฟ๐ถ๐ธ๐ฎ๐น๐ถ ๐ธ๐๐ฎ ๐ธ๐๐ฏ๐ผ๐ฟ๐ฒ๐๐ต๐ฎ ๐ต๐๐ฑ๐๐บ๐ฎ ๐๐ฎ ๐ฎ๐ณ๐๐ฎ
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.
Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. โ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.โ
Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.
Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. โUjauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.โ
Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi.
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.
โTunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri kama tupo hospitali za private (binafsi).โ Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.
-