Waziri Kangi Lugola jitathmini

Waziri Kangi Lugola jitathmini

Tairi bovu

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2017
Posts
3,063
Reaction score
2,986
Mheshimiwa Kangi Lugola wewe ni mtu mzima kiumri na mtu mkubwa sana kimadaraka katika nchi hii. ( naibu waziri) . Kitendo chako ulichofanya bungeni cha kuulizwa swali na mbunge tena swali sensitive linalohusu climate change na badala ya kujibu swali wewe unaleta utani wa kuingiza mambo ya HAJI MANARA NI UTOTO NA UPOTEZAJI MUDA wa hali ya juu sana.

Tunajua mmekataza bunge live ili mkandamize haki zetu za kidemokrasia lakini tunajua unyeti wa mahali hapo ulipo. Kwanini uache kujibu swali la mbunge na badala yake unaingiza mambo ya Simba na Yanga?

Jitathimini mkuu
 
Kisa kumtaja Haji Manara.Kuna mizaha mingi sana inafanyika bungeni siyo leo tu . Na wakati mwingine hata spika hufanya mzaha.Au kwa kuwa leo ni Simba ?
 
Kisa kumtaja Haji Manara.Kuna mizaha mingi sana inafanyika bungeni siyo leo tu . Na wakati mwingine hata spika hufanya mzaha.Au kwa kuwa leo ni Simba ?
uliona na kusikia nature ya swali na alivyojibu?
 
Kisa kumtaja Haji Manara.Kuna mizaha mingi sana inafanyika bungeni siyo leo tu . Na wakati mwingine hata spika hufanya mzaha.Au kwa kuwa leo ni Simba ?

Spika uwa anachomekea ila sio kujibu swali kuhusu CLIMATE CHANGE kwa kuchanganya utani ndani yake. Mfano, angeweza kusema ilo kabla ya kuanza jibu swali kwa kuipongeza Simba na kuipiga vijembe Yanga kama ilivyo kawaida ya washabiki wa hizi timu mbili. Lakini kuchanganya CLIMATE CHANGE na usemaji wa Manara ni kuishushia heshima taaluma ya mazingira na yeye mwenyewe.
 
Kajibu kimzaha sana maswali ya wabunge!
hivi sifa za kuwa wazir ni kuwa kama lugola? huyu aliingia na kofia wakati wenzake wanajadil escrow yeye anafanya mzaha. kaonwa kawa wazir bado analeta mzaha. mlinga alileta mzaha kwa mnyika. yani watu/ mnyika anauliza mambo ya msingi yye dogo anaomba mwongozo juu ya mavazi. wakati mwingine unajiuliza na kuhisi labda mtu huelewi vizuri . kwamba na mlinga nae ni graduate? ghhhhh
 
Kumlaumu mtu mwenye uwezo mdogo wa kufikiri kwa kushindwa kujibu swali linalohitaji weledi wa jambo ni sawa na kumuonea tu!..unapaswa kumwonea huruma tu,ndio kikomo cha uwezo wake!
 
Sababu alizowahi kuzitoa Mbowe wakati wa kupokea fisadi sugu kugombea urais zilikuwa zipi??

Sababu za wanacdm kuruhusu mwenyekiti wa maisha ndani ya cdm ni zipi???

Demokrasia msiyoifanya ndani ya cdm mnataka muipate wapi
 
Kajibu kimzaha sana maswali ya wabunge!
Myonge mnyongeni lkn haki yske mpeni. Naibu eaziri alisema ametoa sgizo kwa halmashauri kuwa wavamizi waondolewe. Kuhusu simba na yanga hata spika Ndugai alikwishafanya utani bungeni kwa hiyo utani usio na madhara ruksa.
 
Back
Top Bottom