Sangamwalogesha
JF-Expert Member
- Mar 10, 2025
- 2,144
- 1,300
Mh. Waziri hongera kwa jinsi unavyomsaidia Rais wetu kwa uchapakazi wako uliotukuka. Watanzania tumekushuhudia unavyofanya kazi usiku na mchana kusaidia watanzania dhidi ya madhila ya ukatili wa aina mbalimbali.
Mwezi uliopita niliandika kupitia jukwaa hili vitendo vya ovyo vilivyokuwa vinadhulumu haki za watoto wetu. Nililalamikia kitendo cha wanafunzi wa shule ya msingi Kimandafu kusahihishiana mitihani. Kiukweli ni kitendo cha ovyo kinachoharibu ubora wa elimu kwani unakuta maswali mengine hayajasahihishwa, maksi imekosewa kujumlishwa n.k.
Pia soma > Meru: Hii tabia ya wanafunzi kusahihisha mitihani ya wanafunzi wenzao ndio competence-based education?
Nashukuru serikali kesho yake walienda wadhibiti ubora kutokana na ukweli kuwa serikali yetu ni sikivu. Cha kushangaza baada ya taarifa ile na hatua iliyochukuliwa mwl. Mkuu badala ashukuru na kuwachukulia hatua walimu wahusika alianza kutafuta mwanafunzi/wanafunzi waliotoa taarifa ile, sasa kwa akili ya kawaida kuna mwanafunzi wa shule ya msingi anaweza kuja kuandika humu?
Ndipo akaanza kuwanyanyasa watoto wa familia moja akihisi mzazi wao ndiye aliyeandika thread niliyoandika mimi. Mtoto moja alikuwa anafanya usafi ktk ofisi yake akamwondoa ofisini kwake, sijui kuna priviledge gani kufanya usafi ofisi ya mwl. Mkuu, labda kumnyanyasa tu kisaikolojia.
Kuna mtoto mwingine mdogo ana kama miaka 8 huyu ndiyo amemnyanyasa kwa kushirikiana na walimu wake, mtoto mdogo kama huyu anaitwa ofisi ya walimu wote anahojiwa vitu vya kipuuzi, anasimangwa, mtoto ambaye hata hawezi kujieleza ukamwelewa.
Mara wamwambie apeleke shuleni karatasi zake za test zilizopita, mara wachunguze madaftari yake, mara maksi aliyopata 44/50 anarekodiwa 11/50. Huyu mtoto alikuja kuugua ghafla sijui ni unyanyasaji ule. Kumbuka ni mtoto wa miaka minane(8), just an innocent child. Kisa thread iliyoandika humu JF, kwanza huu mwl. Mkuu ajue yeye ni kiongozi, ni public figure Rais anaandikwa yeye asiandikwe akifanya uzembe ye ni nani?
Yule mama ni katili tena kwa watoto wadogo wa chini ya miaka 10. Habari kwamba wanafunzi wa darasa la 6 na la 7 kuwa wanasahihisha mitihani ya madarasa ya chini ni siri? Anachukulia wazazi wote kwamba hawawezi kupitia kazi za watoto wao na kugundua makosa? Hii ni dharau kwa wazazi.
Huyu mama hapendi watoto wadogo ushahidi ni vyakula anavyowapikia, watoto wanalishwa makukuru, makande yasiyokobolewa wakati shule za jirani zenye wanafunzi zaidi ya 1300 wanapikiwa vizuri, mahindi yanakobolewa, pili kuna mama moja mzungu anaitwa Birgita anasambazaga unga wa lishe, choroko na vitu vingine ktk baadhi ya shule zilizo ktk Halmashauri ya Wilaya ya Meru, huyu mwl. Mkuu wa shule ya msingi Kimandafu yeye hugawana vyakula hivi na walimu wenzake watoto wa watanzania wakilishwa makukuru, huu ni udhalimu na ukatili wa haki za hawa watoto.
Haitoshi kila mtihani shule hii ni wa kulipia, mitihani mingine kila mtihani unafikia sh. 4000. Mtihani wa juzi wa terminal umelipiwa, anatumia kamati ya shule kwa maslahi yake, dhana ya elimu bila malipo iko wapi?
Huyu na kamati yake wako juu ya Rais wa nchi hii? Afanye upuuzi na uzembe wake halafu anakuja kutishia watoto wetu wadogo waliodhulumiwa haki zao kwanini? Hii kiburi anaitoa wapi, pale Halmashauri nani analinda huu uovu, huu uchafu?
Huyu mama aache kutishia watoto wetu, atimize wajibu wake, hii ni shule ya umma siyo ya babake, na ingekuwa ya babake angewabembeleza watoto wetu, ila kwasababu ni ya serikali anaona watoto wale hawana haki.
Mh. Waziri watoto wanaosoma shule za serikali imefika sehemu wanachukuliwa kama raia daraja la pili, hii haikubaliki. Mh. Gwajima sina ugomvi wala kisa na huyo mwl na kimsingi hanifahamu, kama mtanzania na kama binadamu sipendi uonevu, unyanyasaji, ukatili hasa kwa watoto wadogo malaika tu ambao bwana wetu Yesu kristo alisema acheni watoto wadodo waje kwangu maana ufalme wa Mungu ni wao.
Sasa anatokea mtu moja kwa ushetani wake anawanyanyasa, anawatesa kisaikolojia, ingilia kati mheshimiwa uwasaidie watoto wetu dhidi ya madhila haya. Kuna shule ya jirani, yule mwl. Mkuu wake anawapenda wanafunzi wake, watoto chakula ni kizuri, msaada mama Birgita wote wanapewa watoto hakuna mwalimu anausogelea.
Juzi kawaelekeza walimu wake kuwatendea haki wanafunzi hasa ktk mitihani yao ya wiki iliyopita. Serikali iwe inafanya vetting ya kutosha mwl. Mkuu wa shule ya msingi sifa kuu iwe upendo kwa watoto hasa wadogo maana siku hizi wanapelekwa watoto mpaka wa miaka 3, mtoto km huyu anaweza kula makande hayajakobolewa na akashiba?
Mwezi uliopita niliandika kupitia jukwaa hili vitendo vya ovyo vilivyokuwa vinadhulumu haki za watoto wetu. Nililalamikia kitendo cha wanafunzi wa shule ya msingi Kimandafu kusahihishiana mitihani. Kiukweli ni kitendo cha ovyo kinachoharibu ubora wa elimu kwani unakuta maswali mengine hayajasahihishwa, maksi imekosewa kujumlishwa n.k.
Pia soma > Meru: Hii tabia ya wanafunzi kusahihisha mitihani ya wanafunzi wenzao ndio competence-based education?
Nashukuru serikali kesho yake walienda wadhibiti ubora kutokana na ukweli kuwa serikali yetu ni sikivu. Cha kushangaza baada ya taarifa ile na hatua iliyochukuliwa mwl. Mkuu badala ashukuru na kuwachukulia hatua walimu wahusika alianza kutafuta mwanafunzi/wanafunzi waliotoa taarifa ile, sasa kwa akili ya kawaida kuna mwanafunzi wa shule ya msingi anaweza kuja kuandika humu?
Ndipo akaanza kuwanyanyasa watoto wa familia moja akihisi mzazi wao ndiye aliyeandika thread niliyoandika mimi. Mtoto moja alikuwa anafanya usafi ktk ofisi yake akamwondoa ofisini kwake, sijui kuna priviledge gani kufanya usafi ofisi ya mwl. Mkuu, labda kumnyanyasa tu kisaikolojia.
Kuna mtoto mwingine mdogo ana kama miaka 8 huyu ndiyo amemnyanyasa kwa kushirikiana na walimu wake, mtoto mdogo kama huyu anaitwa ofisi ya walimu wote anahojiwa vitu vya kipuuzi, anasimangwa, mtoto ambaye hata hawezi kujieleza ukamwelewa.
Mara wamwambie apeleke shuleni karatasi zake za test zilizopita, mara wachunguze madaftari yake, mara maksi aliyopata 44/50 anarekodiwa 11/50. Huyu mtoto alikuja kuugua ghafla sijui ni unyanyasaji ule. Kumbuka ni mtoto wa miaka minane(8), just an innocent child. Kisa thread iliyoandika humu JF, kwanza huu mwl. Mkuu ajue yeye ni kiongozi, ni public figure Rais anaandikwa yeye asiandikwe akifanya uzembe ye ni nani?
Yule mama ni katili tena kwa watoto wadogo wa chini ya miaka 10. Habari kwamba wanafunzi wa darasa la 6 na la 7 kuwa wanasahihisha mitihani ya madarasa ya chini ni siri? Anachukulia wazazi wote kwamba hawawezi kupitia kazi za watoto wao na kugundua makosa? Hii ni dharau kwa wazazi.
Huyu mama hapendi watoto wadogo ushahidi ni vyakula anavyowapikia, watoto wanalishwa makukuru, makande yasiyokobolewa wakati shule za jirani zenye wanafunzi zaidi ya 1300 wanapikiwa vizuri, mahindi yanakobolewa, pili kuna mama moja mzungu anaitwa Birgita anasambazaga unga wa lishe, choroko na vitu vingine ktk baadhi ya shule zilizo ktk Halmashauri ya Wilaya ya Meru, huyu mwl. Mkuu wa shule ya msingi Kimandafu yeye hugawana vyakula hivi na walimu wenzake watoto wa watanzania wakilishwa makukuru, huu ni udhalimu na ukatili wa haki za hawa watoto.
Haitoshi kila mtihani shule hii ni wa kulipia, mitihani mingine kila mtihani unafikia sh. 4000. Mtihani wa juzi wa terminal umelipiwa, anatumia kamati ya shule kwa maslahi yake, dhana ya elimu bila malipo iko wapi?
Huyu na kamati yake wako juu ya Rais wa nchi hii? Afanye upuuzi na uzembe wake halafu anakuja kutishia watoto wetu wadogo waliodhulumiwa haki zao kwanini? Hii kiburi anaitoa wapi, pale Halmashauri nani analinda huu uovu, huu uchafu?
Huyu mama aache kutishia watoto wetu, atimize wajibu wake, hii ni shule ya umma siyo ya babake, na ingekuwa ya babake angewabembeleza watoto wetu, ila kwasababu ni ya serikali anaona watoto wale hawana haki.
Mh. Waziri watoto wanaosoma shule za serikali imefika sehemu wanachukuliwa kama raia daraja la pili, hii haikubaliki. Mh. Gwajima sina ugomvi wala kisa na huyo mwl na kimsingi hanifahamu, kama mtanzania na kama binadamu sipendi uonevu, unyanyasaji, ukatili hasa kwa watoto wadogo malaika tu ambao bwana wetu Yesu kristo alisema acheni watoto wadodo waje kwangu maana ufalme wa Mungu ni wao.
Sasa anatokea mtu moja kwa ushetani wake anawanyanyasa, anawatesa kisaikolojia, ingilia kati mheshimiwa uwasaidie watoto wetu dhidi ya madhila haya. Kuna shule ya jirani, yule mwl. Mkuu wake anawapenda wanafunzi wake, watoto chakula ni kizuri, msaada mama Birgita wote wanapewa watoto hakuna mwalimu anausogelea.
Juzi kawaelekeza walimu wake kuwatendea haki wanafunzi hasa ktk mitihani yao ya wiki iliyopita. Serikali iwe inafanya vetting ya kutosha mwl. Mkuu wa shule ya msingi sifa kuu iwe upendo kwa watoto hasa wadogo maana siku hizi wanapelekwa watoto mpaka wa miaka 3, mtoto km huyu anaweza kula makande hayajakobolewa na akashiba?