8691jakigili
Senior Member
- Mar 30, 2012
- 178
- 67
Babu mmoja alimtembelea bibi katika mtaa wa pili ambaye wanasali wote. Alipofika mlangoni aligonga asipate jibu ila alisikia kishindo cha nyayo kilisikika mtu akitembea ndani ya nyumba. Babu huyo alipoona hakuna jibu kwa dakika kadhaa, akaamua kuondoka katika mji huo. Lakini akaacha ujumbe mlangoni: "Tazama, nasimama mlangoni nabisha..."(Ufunuo 3:20). Jumapili iliyofuatia bibi naye akajitokeza kanisani akiwa na karatasi mkononi. Alimpatia mzee mwenzake bila kumsemesha neno lolote. Ujumbe wa bibi ulisomeka: "Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa, kwa kuwa nalikuwa uchi, nikajificha"(Mwanzo 3:10).