opportunist2012
Member
- Feb 8, 2012
- 92
- 8
Ninaunga mkono moja kwa moja maneno ya wazee wa CCM akina mzee Kitime,Kaduma na Butiku kuhusu mustakabali wa chama hiki tawala. Ni ukweli usiopingika chama hiki kinaenda kinyume na itikadi zaHayati Baba wa Taifa,mwalimu Julius K.nyerere.Chama hiki kila kukicha kinazidi kupoteza muelekeo.
Ufisadi na kila aina ya rushwa ndio msingi wa chama hiki.Huwezi kugombea ubunge mpaka uwe na pesa nyingi.Chama hiki kinafumbia macho vitendo vya ubaguzi.
Hali ya ubaguzi wanaofanyiwa walimu wasio wazawa manispaa ya Bukoba si ya kuvumiliwa hata kidogo.Viongozi wanaotokana na chama tawala wanawalinda baadhi ya wakuu wa shule zilizopo Bukoba na afisa elimu sekondari wa manispaa ya Bukoba kuwanyanyasa na kuwabagua walimu wasio wazawa.
Vitendo hivi vya ubaguzi viko waziwazi.Mkuu wa shule ya sekondari Kahororo ni kinara wa ubaguzi huu wa kiukabila.Hii si Tanzania aliyoihubiri Mwalimu Nyerere.Watanzania wanazidi kutokuwa na imani na CCM. Hali hii ikiendelea CCM itajichimbia kabuli lake mwenyewe.
Maneno ya Nnape Nnauye ni ya kutapatapa,eti maneno ya wazee wa CCM wameyapokea na wanayafanyia kazi.Muda wote kwa nini wasiyafanyie kazi mpaka hawa wazee waliojawa na busara watoe kauli kali dhidi ya mustakabali wa CCM.
Ufisadi na kila aina ya rushwa ndio msingi wa chama hiki.Huwezi kugombea ubunge mpaka uwe na pesa nyingi.Chama hiki kinafumbia macho vitendo vya ubaguzi.
Hali ya ubaguzi wanaofanyiwa walimu wasio wazawa manispaa ya Bukoba si ya kuvumiliwa hata kidogo.Viongozi wanaotokana na chama tawala wanawalinda baadhi ya wakuu wa shule zilizopo Bukoba na afisa elimu sekondari wa manispaa ya Bukoba kuwanyanyasa na kuwabagua walimu wasio wazawa.
Vitendo hivi vya ubaguzi viko waziwazi.Mkuu wa shule ya sekondari Kahororo ni kinara wa ubaguzi huu wa kiukabila.Hii si Tanzania aliyoihubiri Mwalimu Nyerere.Watanzania wanazidi kutokuwa na imani na CCM. Hali hii ikiendelea CCM itajichimbia kabuli lake mwenyewe.
Maneno ya Nnape Nnauye ni ya kutapatapa,eti maneno ya wazee wa CCM wameyapokea na wanayafanyia kazi.Muda wote kwa nini wasiyafanyie kazi mpaka hawa wazee waliojawa na busara watoe kauli kali dhidi ya mustakabali wa CCM.