Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,638
- 697,929
Waache wazeeke kwa upendo uleule waliokulea nao.
Waruhusu waongee na wasimulie hadithi tena na tena kwa subira na shauku ile ile waliyokusikiliza ukiwa mtoto. Waache wawe washindi, kwani mara nyingi walikuacha ushinde hata kama hukustahili ushindi .
Waache wafurahie marafiki zao, wazungumze na wajukuu zao... Waache wafurahie kuishi kati ya vitu ambavyo vimeambatana nao kwa muda mrefu, kwa sababu wanateseka wakati wanaona kuwa vipande vya maisha yao vimeng'olewa.
Waache wafanye makosa, kama ulivyofanya mara nyingi... Waache waishi na kujaribu kuwafurahia kwenye sehemu ya mwisho ya safari yao, kama vile walivyokushika mkono ulipoanza yako.
Wape support wafikie mwisho mwema! Watakuwa walinzi wako kiroho kwenye ulimwengu usioonekana watakapokuwa ni roho mautini nje ya mwili uharibikao..
Sent using Jamii Forums mobile app
Waruhusu waongee na wasimulie hadithi tena na tena kwa subira na shauku ile ile waliyokusikiliza ukiwa mtoto. Waache wawe washindi, kwani mara nyingi walikuacha ushinde hata kama hukustahili ushindi .
Waache wafurahie marafiki zao, wazungumze na wajukuu zao... Waache wafurahie kuishi kati ya vitu ambavyo vimeambatana nao kwa muda mrefu, kwa sababu wanateseka wakati wanaona kuwa vipande vya maisha yao vimeng'olewa.
Waache wafanye makosa, kama ulivyofanya mara nyingi... Waache waishi na kujaribu kuwafurahia kwenye sehemu ya mwisho ya safari yao, kama vile walivyokushika mkono ulipoanza yako.
Wape support wafikie mwisho mwema! Watakuwa walinzi wako kiroho kwenye ulimwengu usioonekana watakapokuwa ni roho mautini nje ya mwili uharibikao..
Sent using Jamii Forums mobile app