ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,650
Natumaini wote mu wazima wa afya njema. Mie mzima kama jiwe nadunda maisha kwa raha zangu.
Nimewaza sana kulingana na hali ya maisha ya sasa na jinsi mambo yanavyendelea kubadilika nikaona ngoja niwaulize ili nijue ni kwa kiasi gani mambo yakienda na kubadilika. Issue ni kwamba baadhi ya wazazi walikuwa na tabia ya kuwalisha watoto wadogo chakula walichokuwa hawawezi kutafuna kwa kukitafuna kwanza wenyewe na kisha kukitema chakula hicho na kuwalisha watoto wao. Hili lilifanywa kwa baadhi ya vyakula km mahindi, mihogo au viazi vya kuchoma. Binafsi nilishaona baba yangu akiwafanyia hivyo wajuu zake-watoto wa dada zangu- ambao wengi wao sasa ni watu wazima wenye watoto. Ninachokiongelea hapa ni kama vile ndege anavyolisha makinda yake kwenye kiota.
Hilo ni moja, suala la pili nalo nimeona tuliongelee ni hili la wazazi kunyonya kamasi kutoka kwenye pua za mtoto, hasa iilipotokea mtoto alikuwa anasumbuliwa na mafua/makamasi na inakuwa vigumu kuyadhibiti. Wazazi wa zamani walikuwa wanaweka midomo kwenye pua ya mtoto na kuvuta kamasi kwa mtindo wa kunyonya kisha alitema nje. Ikumbukwe mengi ya haya yalikuwa yakitokea kati ya mwanzoni na mwishoni mwa miaka ya 70.
Inawezekaa likawa ni jambo geni miongoni mwa wengi wetu humu jamvini lakini nahisi wapo ambao waesikia au kuona haya mambo mawili nilioyaongelea.
Sasa naomba niwaulize wanaJF wenzangu, kama hukuwahi kuona au kusikia, hebu jiulize kama wewe unaweza kulifanya hilo sasa hivi? Ni wangapi kati yetu hasa wanaume, umeshawahi walau kumsafisha mwanao aliyejisaidia haja kubwa kama sio kumuita msaidizi wa nyumbani aje amsafishe mwanao? Na je kwa mtazamo wako unadhani wazazi walipokuwa wakifanya haya kwa watoto/wajukuu wao ilikuwa ni ulimbukeni wa kutojua madhara ya matendo haya au ilikuwa ishara ya upendo kwa vizazi vyao hivyo?
Tafakari na toa maoni yako!
Alamsiki.
Nimewaza sana kulingana na hali ya maisha ya sasa na jinsi mambo yanavyendelea kubadilika nikaona ngoja niwaulize ili nijue ni kwa kiasi gani mambo yakienda na kubadilika. Issue ni kwamba baadhi ya wazazi walikuwa na tabia ya kuwalisha watoto wadogo chakula walichokuwa hawawezi kutafuna kwa kukitafuna kwanza wenyewe na kisha kukitema chakula hicho na kuwalisha watoto wao. Hili lilifanywa kwa baadhi ya vyakula km mahindi, mihogo au viazi vya kuchoma. Binafsi nilishaona baba yangu akiwafanyia hivyo wajuu zake-watoto wa dada zangu- ambao wengi wao sasa ni watu wazima wenye watoto. Ninachokiongelea hapa ni kama vile ndege anavyolisha makinda yake kwenye kiota.
Hilo ni moja, suala la pili nalo nimeona tuliongelee ni hili la wazazi kunyonya kamasi kutoka kwenye pua za mtoto, hasa iilipotokea mtoto alikuwa anasumbuliwa na mafua/makamasi na inakuwa vigumu kuyadhibiti. Wazazi wa zamani walikuwa wanaweka midomo kwenye pua ya mtoto na kuvuta kamasi kwa mtindo wa kunyonya kisha alitema nje. Ikumbukwe mengi ya haya yalikuwa yakitokea kati ya mwanzoni na mwishoni mwa miaka ya 70.
Inawezekaa likawa ni jambo geni miongoni mwa wengi wetu humu jamvini lakini nahisi wapo ambao waesikia au kuona haya mambo mawili nilioyaongelea.
Sasa naomba niwaulize wanaJF wenzangu, kama hukuwahi kuona au kusikia, hebu jiulize kama wewe unaweza kulifanya hilo sasa hivi? Ni wangapi kati yetu hasa wanaume, umeshawahi walau kumsafisha mwanao aliyejisaidia haja kubwa kama sio kumuita msaidizi wa nyumbani aje amsafishe mwanao? Na je kwa mtazamo wako unadhani wazazi walipokuwa wakifanya haya kwa watoto/wajukuu wao ilikuwa ni ulimbukeni wa kutojua madhara ya matendo haya au ilikuwa ishara ya upendo kwa vizazi vyao hivyo?
Tafakari na toa maoni yako!
Alamsiki.