Whitesmith
JF-Expert Member
- Aug 12, 2017
- 454
- 635
Habari GT.
WAZANZIBARI SASA WACHAGUE KATI YA;
1: CCM iliyoachwa na Mh. Karume
2: ACT waliyoachiwa na Mh Seif
3: No Reform no Election inayohubiriwa na CHADEMA.
Ama hakika kama kuna jambo ambalo CCM walikuwa wanalitafuta ni utulivu wa uchaguzi Zanzibar hasa hasa Pemba. Kitendo cha ACT wazalendo kushiriki uchaguzi bila reforms inaipa CCM utulivu Zanzibar, kwa hakikisho hilo CCM hataacha kuwapa fadhili ACT kwenye baadhi ya majimbo huku Bara. Hii inatokana na joto Kali wanayopata kutoka CHADEMA.
Kwa kuwa ACT na CCM washamalizana, ni wazi sasa Wazanzibari Pemba na Unguja wako Chama kimoja, inaonekana ni kama CCM imebaini namna pekee yakuwalambisha asali wasumbufu huko Zanzibar ni kupitia Serikali ya Umoja wa Kitaifa huku ikihakikisha wanabaki kuwa chini yao kwa kuwapa makamu wa Rais wa pili asiye na meno na baraza kivuli lisilo na meno, hii ndo njia ambayo CCM inalambisha asali wasumbufu wakisiasa Zanzibar.
Kwa kuwa Bara ilikuwa chini ya Giza la biashara ya kisiasa chini ya FAM na wajanja wachache, ni wazi kuwa Mungu ameamua tofauti sasa biashara imeingia mchanga na mabadiliko yanadaiwa kwa nguvu kupitia CHADEMA. Kwa kuwa msimamo wa Lissu na CHADEMA kuhusu Muungano uko wazi. Sasa Wazanzibari wana machaguo matatu kupata mamlaka yao kamili, ni ama;
1: CCM iliyoachwa na Mh. Karume
2: ACT waliyoachiwa na Mh Seif
3: No Reform no Election inayohubiriwa na CHADEMA.
WAZANZIBARI pia wanaweza kusema acha hili lipite maana nchi iko chini ya Wazanzibari wenzao. Iko wazi kwa sasa msimamo wowote wa Wazanzibari utahesabiwa na kupigwa Chapa kwa muhuri wa moto.
Mtazamo wangu:
Kama ACT wasinge sign CCM leo ingekuwa inahangaika kuwaita wote mezani, wanajua moto wa Wazanzibari na nguvu kuwa ya Dola ingepelekwa Zanzibar. Ni wazi sasa Watanganyika lazima wapite kwenye tanuru la moto walilopitia Wazanzibari miaka yote angalu kupata serikali ya Umoja wakitaifa.
Nashuka Jamvini niwatakie Dominika Njema
WAZANZIBARI SASA WACHAGUE KATI YA;
1: CCM iliyoachwa na Mh. Karume
2: ACT waliyoachiwa na Mh Seif
3: No Reform no Election inayohubiriwa na CHADEMA.
Ama hakika kama kuna jambo ambalo CCM walikuwa wanalitafuta ni utulivu wa uchaguzi Zanzibar hasa hasa Pemba. Kitendo cha ACT wazalendo kushiriki uchaguzi bila reforms inaipa CCM utulivu Zanzibar, kwa hakikisho hilo CCM hataacha kuwapa fadhili ACT kwenye baadhi ya majimbo huku Bara. Hii inatokana na joto Kali wanayopata kutoka CHADEMA.
Kwa kuwa ACT na CCM washamalizana, ni wazi sasa Wazanzibari Pemba na Unguja wako Chama kimoja, inaonekana ni kama CCM imebaini namna pekee yakuwalambisha asali wasumbufu huko Zanzibar ni kupitia Serikali ya Umoja wa Kitaifa huku ikihakikisha wanabaki kuwa chini yao kwa kuwapa makamu wa Rais wa pili asiye na meno na baraza kivuli lisilo na meno, hii ndo njia ambayo CCM inalambisha asali wasumbufu wakisiasa Zanzibar.
Kwa kuwa Bara ilikuwa chini ya Giza la biashara ya kisiasa chini ya FAM na wajanja wachache, ni wazi kuwa Mungu ameamua tofauti sasa biashara imeingia mchanga na mabadiliko yanadaiwa kwa nguvu kupitia CHADEMA. Kwa kuwa msimamo wa Lissu na CHADEMA kuhusu Muungano uko wazi. Sasa Wazanzibari wana machaguo matatu kupata mamlaka yao kamili, ni ama;
1: CCM iliyoachwa na Mh. Karume
2: ACT waliyoachiwa na Mh Seif
3: No Reform no Election inayohubiriwa na CHADEMA.
WAZANZIBARI pia wanaweza kusema acha hili lipite maana nchi iko chini ya Wazanzibari wenzao. Iko wazi kwa sasa msimamo wowote wa Wazanzibari utahesabiwa na kupigwa Chapa kwa muhuri wa moto.
Mtazamo wangu:
Kama ACT wasinge sign CCM leo ingekuwa inahangaika kuwaita wote mezani, wanajua moto wa Wazanzibari na nguvu kuwa ya Dola ingepelekwa Zanzibar. Ni wazi sasa Watanganyika lazima wapite kwenye tanuru la moto walilopitia Wazanzibari miaka yote angalu kupata serikali ya Umoja wakitaifa.
Nashuka Jamvini niwatakie Dominika Njema