Wazanzibari kuitolea kauli rasimu leo

Nipo njiani wakuu naelekea uwanjani nikifika kibandamaiti habari zote nitakupeni hapa pamoja tunaweza.
 
Picha tafadhali. Bado mkutano kuanza au? Usiingie mitini mleta mada
 
Jamani watanganyika na wazanzibar tuungane pamoja kuikataa rasimu ya akina ccm na wachumia tumbo wote kama kina Sita na kina Chenge, kina Seif Rashid na wenzao.
 

Kwenye rasimu ya warioba tatu zinaafadhali kwa wazanzibar,kwenye rasimu ya sita na chenge ni bora mkataba kwa wazanzibar hakuna 2 wala 3,zanzibar kwanza.
 
ngoja tusubiri na huko tena kama wataiba. maana akidi yenyewe bungeni ni ya magumashi maana hata wale ambao hawakupiga kuwa wanaonekana kwenye list ya waliopiga kura tena ya ndio.
 

Hapana haitatuchanganya mkuu kama wamemwaga mboga wacha wamwage ugali mkataba hauchakachuliki ni mahakama za kimataifa ndio zitakazo simamia mkataba mkuu hii ni fundisho zuri mzee warioba aliwatahadharisha juu ya hili suala wakawa vichwa maji jeuri dawa yake kiburi
 
Wasaka tonge wote wanajifanya kumsahau Mwal. Nyerere na Tanganyika yetu. kwani historia ipo wazi ukirudi nyuma kidogo miaka ya tisini wakati wa mchakato wa mfumo mpya wa vyama vingi bila busara za mwalimu na mheshimiwa Walioba kulazimisha mambo yangekua kama miaka ya sabin kurudi. Tuikatae rasimu
 
Mkutano wa hadhara wa Chama cha Wananchi - CUF, eneo la Kibandamaiti, Zanzibar

[video]https://www.facebook.com/video.php?v=864839710201362&se t=vb.160894643929209&type=2&th eater[/video]
 
Sasa hiki ndio nini? Hatuhitaji video tunahitaji live streaming.
 
Chuchu FM kwa kupitia Masafa ya FM hata Dar inafika ila si kwaubora sanaaaa ila unaweza ukatumia stream yao ukawapata popote pale duniani
Mkuu, hiyo stream nimeipata lakini ni muziki tu uliopo tena wa DRC na sasa ni saa kumi na dakika ishirini na tano jioni mbona.
 

Nadhani ni kinyume cha hivyo. Umetaja sifa zote za waliopiga kura za ndio! Ulikuwa unamaanisha hivyo?
 
Updates.......
Sasa Wazanzibar wanatangaza rasmi "ni vita wanaitaka nchi yao"
Seif ndo anaingia umati umezizima
 
Updates.......
WanaCCM wamefurika kwenye mkutano na wanahamasika sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…