Wazanzibar-muungano imekula kwenu

i pad3

JF-Expert Member
Mar 16, 2012
1,518
378
hawa jamaa wapemba waliopo madarakani(ccm) hawataki kabisa muungano uvujike, wanajua ukivunjika itakuwa imekula kwao
[h=1]Balozi Seif akoromea wapinga muungano Zanzibar[/h] Written by Mrfroasty (Ufundi) // 10/04/2012 // Habari // 1 Comment

balozi_seif_kiduni-564x272.jpg

  • Azitaka taasisi za kiislamu kuacha kujadili muungano mara moja!
Salma Said,
Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekusudia kutoa muongozo maalumu na msimamo wake juu ya suala la utoaji wa maoni katika kupatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “kwa kuzingatia umuhimu wa suala hilo la katiba mpya, Chama cha Mapinduzi kinakusudia kutoa muongozo maalum utaowawezesha Wanachama wa CCM kuutumia ili kuweza kuelezea msimamo wao” alisema Balozi Seif.
Balozi Seif ameyasema hayo juzi katika nyakati tofauti wakati akizungumza na wanachama wa CCM wa Kitope, Matetema na Upenja katika ziara yake ya kugawa vifaa mbali mbali vya ujenzi na mashuleni ikiwemo shule ya Kinduni.
Akielezea msimamo thabiti wa Chama Cha Mapinduzi hadi sasa Balozi Seif ambaye ni Mwakilishi wa Jimbo la Kitope alisema ni Muungano wa serikali mbili na wanaopita kutoa ushawishi kutokana na faida zake zimeonekana katika kipindi cha miaka 48, na kasoro zilizokuwapo isiwe kisingizio cha kutaka kuvunjika.
Mwakilishi huyo alisema wanaotaka serikali tatu hawajazuiwa kutoa maoni yao, lakini sio jambo la busara kwa vikundi hivyo kutumia majukwaa ya dini na mabaraza ya Katiba kutoa vitisho kwa wenye mawazo ya kuipinga dhana hiyo.
Aidha amewakemea viongozi wa dini wenye kuendesha mihadhara ya kuzungumzia suala la Muungano na kuwataka waache kufanya hivyo mara moja kwani wanawababaisha wananchi wa Zanzibar katika suala hilo.
Makamu huyo wa pili ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM alisema wakati wananchi wanataka kuelekea kwenye machakato wa katiba mpya tayari kuna vikundi vinavyojipa madaraka ya kuwasemea Wazanzibari na kutoa maoni dhidi ya Muungano jambo ambalo linatakiwa kuachwa.
Alisema wazanzibari wenyewe ndio wenye kujua mustakbali wa hatima yao na sio kutolewa maoni kwa niaba yao kwani wakati ukifika wa kutoa maoni wananchi watajitokeza na kusema wanachotaka juu ya sualazima la Muungano uliyopo.
Katika siku za hivi karibuni jumuiya za kidini zimekuwa zikifanya mihadhara mijini na mashamba kuelezea namna ya kutoa maoni katika mchakato wa katiba mpya utakapofika ambapo baadhi ya wananchi husema hawataki Muungano kitendo ambacho kimeonekana kumkera Balozi Seif.
Balozi Seif alisema wakati huu wa demokrasia si wakati tena wa kundi moja kulisemea au kuliamulia kundi jengine, hivyo suala la Muungano litaamuliwa na wananchi wenyewe wakati wa kukusanya maoni ya katiba mpya ya Tanzania na si wakati wa kupewana vitisho wala wananchi kuamrishwa mambo yenye maslahi yao .
Aliwataka wanachama wa Chama Cha Mapinduzi kuwa macho na kuwa makini zaidi kutokana na vikundi hivyo kwa kuzingatia kwamba vikundi hivyo havijatumwa na mtu yeyote hufanya hivyo bali ni utashi wao wa binafsi ndio unaowapelekea kufanya hivyo.
“Msikubali kubabaishwa na vikundi hivi ni utashi wao wenyewe” alisema Balozi Seif na kuongeza kwamba.
“Vikundi hivyo vinapita kufanya mihadhara na wanasema wametumwa na wazanzibari kwani wamekutana nao lini na wapi wakazungumza hayo? ni maoni yao wasiwasingizie wazanzibari na Wazanzibari wasiotaka hilo watatoa maoni yao katika Tume iliyoundwa ya kukusanya maoni na sio kupitia majukwaa kama hayo”, alisema Balozi Seif.
Akitoa masikitiko yake Balozi Seif alisema serikali haiwezi kuvumilia matusi wanaotukanwa viongozi wa ngazi za juu katika mikutano au mihadhara inayofanyika kwa kuzingatia baadhi ya wanaofanya mihadhara hiyo huvuka mipaka na kuwatukana matusi ya nguoni viongozi wa ngazi za juu.
“Hali hiyo inasikitisha kuona baadhi ya viongozi hao wamekuwa wakiwavunjia heshima viongozi wa nchi kwa kuwatukana matusi ya nguoni jambo hili serikali haiwezi kulivumilia kabisa” alisema Balozi Seif kauli ambayo tayari ilishatolewa na umoja wa vijana wa CCM Zanzibar hivi karibuni.
Alisema kinachosikitisha zaidi kuona wengi wa viongozi hao baada ya kuja kwa serikali ya Umoja wa Kitaifa walikuwa ni vinara wanaoiombea Zanzibar kudumisha amani, lakini hivi sasa wamekuwa wakitumia majukwaa hayo kuanzisha vitendo vitavyosababisha kuvunjika kwa amani.
Alisema jambo la msingi ni kuona hivi sasa wanajiandaa kushiriki kwa wingi katika mchakato wa kutoa maoni ya kuiwezesha Tanzania kupata Katiba mpya isiokuwa na mizengwe wala ubabaishaji.
Aidha Balozi Seif, aliwaataka wanachama hao kuhakikisha uchaguzi za ndani ya Chama nazo wanazifanya kwa kuzingatia kupata viongozi bora wataokiwezesha chama kupata ushindi katika uchaguzi Mkuu ujao.
Mapema Balozi Seif, aliwataka wanafunzi katika Skuli ya Upenja kuona wanajibidiisha kusoma zaidi na kuacha mchezo utaowasababishia kufanya vibaya katika masomo yao .
Balozi Seif, katika ziara hiyo aliukabidhi uongozi wa skuli hiyo mabati zaidi ya 100 kwa ajili ya kujenga majengo mawili ya madarasa mapya ya skuli hiyo huku Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali iliahidi kugharamia umalizikaji wa majengo hayo kabla ya bajeti mpya kuingia.
Wakati huo huo Mke wa Makamu wa Pili wa Rais Mama Asha Seif Iddi, akitoa nasaha zake kwa wanafunzi wa skuli hiyo alisema uongozi wa Jimbo hilo utaendelea kuwa pamoja na wananchi wa Jimbo hilo kwa kuwapa misaada mbali mbali itayoweza kulifanya jimbo hilo kuwa na maendeleo zaidi.
Jumla ya Wanafunzi 244 waliofaulu mitihani yao ya kuingia Mchepuo, Darasa la 11 na la 12 kwa mwaka 2012 wamekabidhiwa sare, Baskeli 13 kwa wale walioingia Darasa la 13 na Baskeli 7 kwa Walimu Wakuu wa Skuli saba za Jimbo la Kitope.
Tukio hilo limekwenda sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Nd. Vuai Ali Vuai Kukabidhiwa Baskeli tatu kwa Walimu wa Skuli ya Msingi ya Kidagoni Jimbo la Nungwi kufuatia ahadi ya Balozi Seif aliyoitoa wakati wa ziara yake mkoa wa Kaskazini Unguja Mapema mwezi machi Mwaka huu.
Gharama za zawadi zote hizo zinakadiriwa kufikia shilingi milioni sita na laki tano { 6,500,000/-}.
Mapema Mkurugenzi wa Utumishi na Uendeshaji wizaya ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Vuai Ali amempongeza Mbunge wa Jimbo la Kitope kwa juhudi zake zilizopelekea Wanafunzi wote wa Jimbo hilo kusoma katika Vikalio.
Vuai alisema lengo la baadaye la Wizara ya Elimu Mafunzo ya Amali Zanzibar ni kuwa na Mkondo mmoja tu wa Masomo kwa Skuli zote Unguja na Pemba.
Kwenye Hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Ndugu Vuai Ali Vuai katika kuhamasisha kutanzua uhaba wa Madarasa ya kusomea alishawishi mchango wa papo kwa papo uliopelekea walioshuhudia hafla hiyo kutoa ahadi ya kuchangia Ujenzi wa Jengo jengine la Skuli ya Kinduni.
Mchango huo wa papo kwa papo umezalisha ahadi za matofali 3,000 gari za Mchanga na Fedha Taslimu kutoka kwa Maafisa na Viongozi wa Sekta tofauti wakati Mke wa Mbunge wa Jimbo hilo Mama Asha Suleiman Iddi akaahidi kuchangia gharama zote za Ujenzi wa Msingi wa Jengo hilo pamoja na Saruji yake
 
Back
Top Bottom