BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Wazalishaji wa pedi waitupia lawama serikali https://www.jamiiforums.com/index.p...ikali&format=pdf&option=com_content&Itemid=57https://www.jamiiforums.com/index.p...nt&print=1&page=&option=com_content&Itemid=57https://www.jamiiforums.com/index.p...hbGkmb3B0aW9uPWNvbV9jb250ZW50Jkl0ZW1pZD01Nw==
Friday, 29 January 2010 06:35
Na Edmund Mihale
Majira
MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Kays Hygene inayotengeneza pedi aina ya Jessy, Bi. Khadija Simba ameitupia lawama serikali kwa kushindwa kusimamia bidhaa zinazotengenezwa na viwanda vya hapa nchini, hali inayosababisha nchi kuwa dampo la kuuzia bidhaa bandia.
Kauli hiyo imekuja siku mbili baada ya polisi kukamata pedi bandia aina ya Always zenye thamani ya sh. milioni 60 zilizokuwa zikisafirishwa kwenda mikoani.
Akizungumza na Majira ofisi kwake Dar es Salaam jana, Bi. Simba alisema Watanzania wengi wamekata tamaa katika kuanzisha viwanda, hivyo wameamua kuwa wachuuzi wa bidhaa za nje husasni katika nchi ya China kutokana na unafuu wa bei zake.
"Kuna udhaifu mkubwa kwa watendaji wa serikali na sisi wenyewe katika kusimamia wawekezaji wa ndani kwa kuwa tumekosa uzalendo wa kuipenda nchi yetu," alisema Bi. Simba.
Alisema serikali kushindwa kuteteta viwanda vya hapa nchini ni sawa na kuwamilikisha wageni uchumi na kuwacha wazawa mkono matupu, hali ambayo ni hatari kwa taifa la leo na vizazi vijavyo.
Alisema watendaji wengi wa serikali na wafanyabishara wasio na mapenzi na nchi yao, wamekuwa wakiangalia maslahi ya sasa bila kujali ya kesho na vizazi vijavyo kwa kuingiza bidhaa ambazo ni hatari kwa Watanzania kutokana na kusababisha magonjwa yasiyopona.
Wakati lawama hizo zikitolewa, taarifa za kitaalamu kuhusu bidhaa hizo bandia zinasema kuwa zinasababisha madhara makubwa kwa akina mama, yakiwamo magonjwa ya fangasi na maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI).
Friday, 29 January 2010 06:35
Na Edmund Mihale
Majira
MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Kays Hygene inayotengeneza pedi aina ya Jessy, Bi. Khadija Simba ameitupia lawama serikali kwa kushindwa kusimamia bidhaa zinazotengenezwa na viwanda vya hapa nchini, hali inayosababisha nchi kuwa dampo la kuuzia bidhaa bandia.
Kauli hiyo imekuja siku mbili baada ya polisi kukamata pedi bandia aina ya Always zenye thamani ya sh. milioni 60 zilizokuwa zikisafirishwa kwenda mikoani.
Akizungumza na Majira ofisi kwake Dar es Salaam jana, Bi. Simba alisema Watanzania wengi wamekata tamaa katika kuanzisha viwanda, hivyo wameamua kuwa wachuuzi wa bidhaa za nje husasni katika nchi ya China kutokana na unafuu wa bei zake.
"Kuna udhaifu mkubwa kwa watendaji wa serikali na sisi wenyewe katika kusimamia wawekezaji wa ndani kwa kuwa tumekosa uzalendo wa kuipenda nchi yetu," alisema Bi. Simba.
Alisema serikali kushindwa kuteteta viwanda vya hapa nchini ni sawa na kuwamilikisha wageni uchumi na kuwacha wazawa mkono matupu, hali ambayo ni hatari kwa taifa la leo na vizazi vijavyo.
Alisema watendaji wengi wa serikali na wafanyabishara wasio na mapenzi na nchi yao, wamekuwa wakiangalia maslahi ya sasa bila kujali ya kesho na vizazi vijavyo kwa kuingiza bidhaa ambazo ni hatari kwa Watanzania kutokana na kusababisha magonjwa yasiyopona.
Wakati lawama hizo zikitolewa, taarifa za kitaalamu kuhusu bidhaa hizo bandia zinasema kuwa zinasababisha madhara makubwa kwa akina mama, yakiwamo magonjwa ya fangasi na maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI).