Mkuu umenena kweli. Maana sio kila atakayekuwa hapo kijijini ni mkazi wa kijiji hicho. Na hata kama ni mkazi wa kijiji hicho, sidhani kama ni sahihi kila kijiji kuwa na sheria yake (hasa zinazohusiana na uhuru wa mtu mmoja mmoja).
Tunaweza tukaishangilia hii, lakini kesho tukasikia kijiji kingine wakasema ni marufuku kusuka nywele, wengine ni marufuku kupaka kucha rangi, wengine ni marufuku kusikiliza miziki ya aina fulani nk.
Kweli kabisa mkuu wangu. Hakuna watu wavunjaji haki za binadamu ktk maeneo ya vijijini na watu masikini kama vikundi haramu vya aina hiyo vikijiita watetezi wa mila ama dini!