DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
WAUMINI wa Dini ya Kiislamu wameshauriwa kutoshiriki maandamano yanayohamasishwa kwenye mitandao ya kijamii yaliyopangwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu, na badala yake wajitokeze kupiga kura kwa amani katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe hiyo.
Wito huo ulitolewa jana Oktoba 4,2025 na Shehe wa Msikiti wa Mtambani, Wilaya ya Kinondoni mkoa wa Dar es salaam,Shabani Pembe wakati wa Kongamano la Kuombea Uchaguzi, Amani na Dua ya Nchi lililofanyika jijini Dar es Salaam.
“Hakuna muislamu yeyote atakayeingia barabarani kuandamana. Atakayeingia barabarani Oktoba 29 atakutana na mambo yasiyoridhisha na kuipa familia yake shida. Wanaohamasisha maandamano hawapo nchini, hivyo ni heri mkapige kura badala ya kuandamana,” amesema Shehe Pembe.
Chanzo: Habari Leo
Wito huo ulitolewa jana Oktoba 4,2025 na Shehe wa Msikiti wa Mtambani, Wilaya ya Kinondoni mkoa wa Dar es salaam,Shabani Pembe wakati wa Kongamano la Kuombea Uchaguzi, Amani na Dua ya Nchi lililofanyika jijini Dar es Salaam.
“Hakuna muislamu yeyote atakayeingia barabarani kuandamana. Atakayeingia barabarani Oktoba 29 atakutana na mambo yasiyoridhisha na kuipa familia yake shida. Wanaohamasisha maandamano hawapo nchini, hivyo ni heri mkapige kura badala ya kuandamana,” amesema Shehe Pembe.