Waume wapendeni wanawake.

Waume wapendeni wanawake.

happiness win

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
2,461
Reaction score
1,394
Tunaelewa kwamba mke ametoka katika ubavu wa mume. Hakutoka katika nyayo ili adharauliwe na kukandamizwa wala hakutoka katika kichwa ili mwanamume ajisifu kuwa yeye ana akili sana; bali ametoka ubavuni ili akumbatiwe na kulindwa, kumbuka ametoka ubavu wa kushoto ulio karibu na moyo ili apendwe, aheshimiwe na kuthaminiwa.

Kwa kuwa ubavu haujanyooka sawa sawa mke pia ana mapungufu, lakini asinyooshwe kwa nguvu atavunjika, akanywe kwa upole na upendo naye atasikia.

Mke ana ana akili, huruma, hisia na akifanyiwa yote hayo huwa kitu chema, tofauti na hivyo unamharibu na kuondoa lengo la Mungu kukuumbia msaidizi. Kumbuka mwanamke akiharibika hutaweza kumrudisha katika hali halisi aliyoumbwa nayo utaishia kuona mwanamke ni kiumbe hatari kisichostahili kuishi duniani.

Mambo haya yote yanaanza toka mwanamke anapozaliwa, apendwe, alindwe na atunzwe. Wapende dada zako/binti zako hadi watakapokuwa wake za watu na hadi kifo.
 
Mashairi mazuri sana ila mimi huwa sijui vizuri kama upendo ni matokeo ya akili zetu au ni nguvu inayotoka nje inachochea vitu tulivyoumbwa navyo. Huwa naona mtu anapenda kweli kweli kiasi kuwa hawezi kula, mambo yake mengi hayaendi. Lakini baada ya muda anasema nafikiri nilikuwa sipendi sijui nilichokuwa nimefanyiwa.
 
Ni wanaume wachache sana wenye moyo mgumu mbele ya wanawake. Ukiona mwanamke anapata shida kwa mume wake, ni sababu ya VIBURI, GUBU na KUTOJIHESHIMU kwa wanawake hao.

Virukanjia wengi sana wamejibadili majina siku hizi wote wanajiita wake, lkn wamepinda na ndio wanaishia kwenye vibano. Mwanamke anayejitambua na kuzijua silaha zake siku zote atapendwa na mumewe. Ukitanua mbavu lazima uchapike
 
Umenena vyema sana happiness win. Lakini hiyo isiwe sababu ya baadhi yao ku-misbehave, wanapaswa nao kuheshimu, kupenda nk. Upendo uwe niwa pande zote mbili vinginevyo hali bado itakuwa mbaya kwenye mahusiano. Ila ujumbe tumeupokea.
 
Ni wanaume wachache sana wenye moyo mgumu mbele ya wanawake. Ukiona mwanamke anapata shida kwa mume wake, ni sababu ya VIBURI, GUBU na KUTOJIHESHIMU kwa wanawake hao.

Virukanjia wengi sana wamejibadili majina siku hizi wote wanajiita wake, lkn wamepinda na ndio wanaishia kwenye vibano. Mwanamke anayejitambua na kuzijua silaha zake siku zote atapendwa na mumewe. Ukitanua mbavu lazima uchapike

Tabia zote mbaya ulizozitaja zinatokana na malezi wanayoyapata wanawake toka siku ya kwanza kuingia duniani. Ile anazaliwa tu Baba anasema "umezaa toto la kike, shida tupu", malezi yatakayoendelea baada ya hapo si ya upendo tena, unadhani nini kitatokea... ndio hizo tabia. Ndio maana nikasema Wababa, wakaka, wapendeni wanawake, yaani kuanzia dada zenu hadi wake zenu. Wanawake ni viumbe vya kulelewa kwa tahadhari.
 
Tunaelewa kwamba mke ametoka katika ubavu wa mume. Hakutoka katika nyayo ili adharauliwe na kukandamizwa wala hakutoka katika kichwa ili mwanamume ajisifu kuwa yeye ana akili sana; bali ametoka ubavuni ili akumbatiwe na kulindwa, kumbuka ametoka ubavu wa kushoto ulio karibu na moyo ili apendwe, aheshimiwe na kuthaminiwa.

Kwa kuwa ubavu haujanyooka sawa sawa mke pia ana mapungufu, lakini asinyooshwe kwa nguvu atavunjika, akanywe kwa upole na upendo naye atasikia.

Mke ana ana akili, huruma, hisia na akifanyiwa yote hayo huwa kitu chema, tofauti na hivyo unamharibu na kuondoa lengo la Mungu kukuumbia msaidizi. Kumbuka mwanamke akiharibika hutaweza kumrudisha katika hali halisi aliyoumbwa nayo utaishia kuona mwanamke ni kiumbe hatari kisichostahili kuishi duniani.

Mambo haya yote yanaanza toka mwanamke anapozaliwa, apendwe, alindwe na atunzwe. Wapende dada zako/binti zako hadi watakapokuwa wake za watu na hadi kifo.

Sasa unamaanisha demu au ndo nini sasa!

Dada, binti na wanawake ni vitu tafauti!
Usinchanganye.

Adam mwenyewe alipobananishwa si akaropoka
"si ni huyu mwanamke ulionipa!"
 
Umenena vyema sana happiness win. Lakini hiyo isiwe sababu ya baadhi yao ku-misbehave, wanapaswa nao kuheshimu, kupenda nk. Upendo uwe niwa pande zote mbili vinginevyo hali bado itakuwa mbaya kwenye mahusiano. Ila ujumbe tumeupokea.

Asante kwa kupokea ujumbe, wapende wanao wote na dada zako (ila hapa naongelea wa kike). Toka tumboni hadi wanazaliwa na kukua hadi kuolewa kama wangelelewa kwa upendo nao wangejifunza kupenda, kuheshimu na kuthamini wengine.
 
Sasa unamaanisha demu au ndo nini sasa!

Dada, binti na wanawake ni vitu tafauti!
Usinchanganye.

Adam mwenyewe alipobananishwa si akaropoka
"si ni huyu mwanamke ulionipa!"

nimeongelea wanawake, nikasema wanapaswa kupewa upendo toka wakiwa tumboni. Hivyo mwanao wa kike, dada yako, na baadae mkeo au demu wako kama unavyoita.
 
Tunaelewa kwamba mke ametoka katika ubavu wa mume. Hakutoka katika nyayo ili adharauliwe na kukandamizwa wala hakutoka katika kichwa ili mwanamume ajisifu kuwa yeye ana akili sana; bali ametoka ubavuni ili akumbatiwe na kulindwa, kumbuka ametoka ubavu wa kushoto ulio karibu na moyo ili apendwe, aheshimiwe na kuthaminiwa.

Kwa kuwa ubavu haujanyooka sawa sawa mke pia ana mapungufu, lakini asinyooshwe kwa nguvu atavunjika, akanywe kwa upole na upendo naye atasikia.

Mke ana ana akili, huruma, hisia na akifanyiwa yote hayo huwa kitu chema, tofauti na hivyo unamharibu na kuondoa lengo la Mungu kukuumbia msaidizi. Kumbuka mwanamke akiharibika hutaweza kumrudisha katika hali halisi aliyoumbwa nayo utaishia kuona mwanamke ni kiumbe hatari kisichostahili kuishi duniani.

Mambo haya yote yanaanza toka mwanamke anapozaliwa, apendwe, alindwe na atunzwe. Wapende dada zako/binti zako hadi watakapokuwa wake za watu na hadi kifo.

Iko poa, ila umesahau kitu kimoja kwa wanawake, ambacho ni "wanawake watiini waume zenu".
 
Iko poa, ila umesahau kitu kimoja kwa wanawake, ambacho ni "wanawake watiini waume zenu".

Ni kweli Biblia inasema hivyo. Lakini Utii kwa mtu asiyekupenda unakuwa na walakini tena unakuwa wa kuigiza tu kwa muda mwishoni dharau huchukuwa nafasi. Ukisoma vizuri Neno hilo lilianza na ENYI WANAUME WAPENDENI WAKE ZENU...
 
Tabia zote mbaya ulizozitaja zinatokana na malezi wanayoyapata wanawake toka siku ya kwanza kuingia duniani. Ile anazaliwa tu Baba anasema "umezaa toto la kike, shida tupu", malezi yatakayoendelea baada ya hapo si ya upendo tena, unadhani nini kitatokea... ndio hizo tabia. Ndio maana nikasema Wababa, wakaka, wapendeni wanawake, yaani kuanzia dada zenu hadi wake zenu. Wanawake ni viumbe vya kulelewa kwa tahadhari.

Hivi mwanamke anayemjibu hovyo mume wake anakuwa alifundishwa na baba yake eti? Yapo mambo ambayo ni zao la ukuaji, lakini mengi wanafundisha wenyewe ukubwani.

Hapa JF kumejaa manungayembe yanataka kuolewa, at the same time ndoa imegeuka kuwa 'a business of equal shares' as if kuna kitu tunashindania. Hakuna cha kuwataka hawa wafanye hivi, wala wale wafanye vile, tukiufuata mpango wa Mungu hakuna wa kuijutia ndoa.
 
Hivi mwanamke anayemjibu hovyo mume wake anakuwa alifundishwa na baba yake eti? Yapo mambo ambayo ni zao la ukuaji, lakini mengi wanafundisha wenyewe ukubwani.

Hapa JF kumejaa manungayembe yanataka kuolewa, at the same time ndoa imegeuka kuwa 'a business of equal shares' as if kuna kitu tunashindania. Hakuna cha kuwataka hawa wafanye hivi, wala wale wafanye vile, tukiufuata mpango wa Mungu hakuna wa kuijutia ndoa.

Kwenye blue!! Mara nyingi tabia za mke mtukanaji hazianzii ukubwani. Huyu alishazoea matusi toka mdogo, inawezekana amekuwa kwa kutukanwa na kuona mama yake akitukanana na baba yake hivyo naye anakuwa mtukanaji na mgombanaji na mbabe katika ndoa. Kitu kidogo tu kitaibua mahasira na machungu ya maisha aliyoishi akiwa mdogo, au mateso aliyoyapata mama yake ambayo yeye aliyashuhudia; hali hii humfanya hata asiwe na heshima wala kuona umuhimu wa mumewe kwake.

Ni vizuri ukitaka kujua tabia za mwanamke unayemuoa nenda kaone mama yake anavyoishi na mumewe.
 
Asante kwa kupokea ujumbe, wapende wanao wote na dada zako (ila hapa naongelea wa kike). Toka tumboni hadi wanazaliwa na kukua hadi kuolewa kama wangelelewa kwa upendo nao wangejifunza kupenda, kuheshimu na kuthamini wengine.

Thanks, Wanangu wameshaolewa tayari sasa hivi nalea vijukuu.
 
sema ni wachache wajuayo haya yoote!!!

Nilikwenda Hospitali moja hapa jijini nikamkuta baba anatukana matusi kwa kuwa mkewe kazaa jike, watu walijazana kumsikiliza naye akatukana sana na kuwakashifu sana wanawake. Nilimhurumia huyo mtoto aliyezaliwa na kufikiri maisha yake yatakuwaje kama amepokelewa hivi, tena alikuwa anasisitiza "umenizalia baa medi, silitaki mie"
 
Ni kweli Biblia inasema hivyo. Lakini Utii kwa mtu asiyekupenda unakuwa na walakini tena unakuwa wa kuigiza tu kwa muda mwishoni dharau huchukuwa nafasi. Ukisoma vizuri Neno hilo lilianza na ENYI WANAUME WAPENDENI WAKE ZENU...

Ikiwa utaonesha utii kwa mtu yoyote ni lazima upendwe tu. Kinyume cha utii ni uasi na pia kumbuka uasi ndio dhambi ya kwanza kabisa iliyomwingia shetani hadi akakataa kumtii Mungu. Mungu aimpenda shetani lakini shetani hakujali kupendwa na Mungu na badala yake hakumtii Mungu.

Kwa kuliona hilo ndio maana Mungu amewatahadharisha wanaume kwa kuwaambia kuwa "Enyi wanaume ishini na wake zenu kwa akili" na pia maandiko hayo hayo yanasema mwanamke -------- ndio huivunja nyumba yake yeye mwenyewe.
 
Hapa JF kumejaa manungayembe yanataka kuolewa

Give me a break guy,unamanisha nini,kila anayetaka kuolewa ni nungayembe?au kutaka kuolewa ni dhambi?au kutokuolewa ni dhambi?For your information huku kuna wanawake wenye heshima zao kuliko hao unaofikiri wapo kanisani au msikitini i know some of them.

Kuna mtu haingii bar,hajichanganyi, kutoka kwake ni kazini na kanisani kuwa jf is not a justification of abusing us.

And being a man does not give you a right of talking whaever nasty you feel againsty women only because you can wake up in the morning and get married.
Life is vicious bro usitukane only because hatukuoni au ni kama vile unatujua

,
 
Back
Top Bottom