Watumishi wezi, waliokosa uaminifu

Watumishi wezi, waliokosa uaminifu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
373,018
Reaction score
864,149
Karama na vipawa ni tunu mtu atunukiwazo bure na Mungu, hadai hata senti moja na si wote wanajaaliwa kuvipata, bali Mungu huwapa wale aliowachagua ili wakautumikie ulimwengu kwa niaba yake karama na vipawa si vitu unaweza kwenda shule ukavisomea na kufaulu kwanza hakuna shule za namna hiyo Mungu anatambua uwepo na kazi zifanywazo na hawa manabii na mitume, ni yeye mwenyewe ndio kawakirimia vipawa na karama ili wakautumikie ulimwengu,kawapa bure kwenye maandiko matakatifu kuna mstari unasema 'nimewapa bure toeni bure' kawapa vipawa na karama za kuhubiri, kuponya , kuhuisha, kufufua na kutenda miujiza mingi.

Kawapa bure kabisa.Lakini ni Mungu huyu huyu anayetuasa kuwa tusiwaamini hawa pamoja na kufanya miujuza yote hiyo tena kwa jina lake! Unatambua ni kwanini?Ni kwasababu si watumishi waaminifu ni watumishi wezi waliopewa bure ili wakauponye ulimwengu lakini wao wanatoza fedha na kujilimbikizia mali na utajiri huku wakiishi maisha ya starehe na anasa nyingi Mungu anaona na hesabu ya matendo yao itakuwa siku ya kiama kile kinachopatikana kwenye huduma wazitoazo walipaswa wakirudishe kwa Mungu kwa njia kusaidia ulimwengu kwa kujenga vituo vya watoto yatima wajane na wasiokuwa na makazi, kwa kujenga vituo vya afya na hospitali kwa kusaidia kwenye nyanja za elimu lishe na upatanishi, nk.

Lakini ndugu zangu hawa wanatenda tofauti wanatanua kwa kushindana kumiliki mali nyingi wanashindana kuvaa wanashindana kuendesha magari ya kifahari zikiwemo ndege na vyombo vya majini wanashindana kwa kila kitu huu ni wizi huku ni kukosa uaminifu.Mungu anaona na anaona kweli jinsi waumini maskini wanavyozidi kukamuliwa kila kukicha huku akaunti za manabii zikizidi kuvimbiwa mihela.

GOD IS WATCHING!
 
What they say Is not what they do
What they do Is not always true
They preach water and drink wine
...... I better watch them
(By Them Mushrooms)
^^
 
What they say Is not what they do
What they do Is not always true
They preach water and drink wine
...... I better watch them
(By Them Mushrooms)
^^

At least babu wa Loliondo alikuwa tofauti, alitoza mia tano tuu na katika hiyo akachukua mia mbili tuu, hakufanya matangazo kwenye media wala kwenye billboards lakini habari zake zilifika mbali na maelfu walienda kwake...huu ni mfano wa uchaji kwa Mungu
 
1449922556875.jpg
What they say Is not what they do
What they do Is not always true
They preach water and drink wine
...... I better watch them
(By Them Mushrooms)
^^

1449922545097.jpg
 
1449922959377.jpg gulf stream thamani yake USD million 601449922996826.jpg huyu yeye kaamua kuanzisha na biashara kabisa
 
Kazi ya Mungu ni Nazi ya kujitolea na malipo hutoa yeye...lakini kwa uchoyo na ubinafsi hujikusanyia hata visivyo vyake hii ni laana kubwa
 
Ufafanuzi watumishi wa Mungu hawazuiliwi kuwa na miladi kadha wa kadha.Siyo dhambi mfano Ibrahim alikuwa na utajili mkubwa ukisoma biblia. Sadaka ni kitu kitakatifu kwa Mungu hawawezi tumia wakapona bila kibali cha Mungu.Hawo wote ulio wataja hapo juu wengine wakulima wakubwa kama tb Joshua na wengine biashara zao binafsi.Nadhani nime eleweka.
 
Kwanza niharakishe kutamka hapa kwamba HAKUNA kiumbe yeyote (mwanadamu akiwemo) mbinguni na ardhini awezaye kufufua wafu.Ni Mwenyezi Mungu PEKEE ndiye mwenye uwezo huo wa kuhuisha na kufisha.
Pili;hawa wanaojiita manabii pamoja kwamba hawajatuweka wazi Mungu yupi kawapa unabii,lakini pia hawajatuambia ni Mungu yupi aliyewaambia kila 'nabii' aanzishe kanisa lake na kwa nini utaratibu wa ibada ufanane.
Tatu,Mungu kakataza kujilimbikizia mali,je wao wanapingana na Mungu?
Nne,ukiacha kuhudumu kanisa ambayo ni 'utumishi wa Mungu' kuna shughuli gani HALALI wanazofanya mpaka wanakua matajiri kupindukia?
Maswali haya wanajiuliza wale wenye KUFIKIRI KULIKO KAWAIDA,lakini wale nawapa pole wale WANAOFIKIRI KAWAIDA.
 
Ufafanuzi watumishi wa Mungu hawazuiliwi kuwa na miladi kadha wa kadha.Siyo dhambi mfano Ibrahim alikuwa na utajili mkubwa ukisoma biblia. Sadaka ni kitu kitakatifu kwa Mungu hawawezi tumia wakapona bila kibali cha Mungu.Hawo wote ulio wataja hapo juu wengine wakulima wakubwa kama tb Joshua na wengine biashara zao binafsi.Nadhani nime eleweka.

Tofautisha na nilichoandika hapa, si kila mmoja asemaye Mungu anamaanisha Mungu mkuu lakini mtumishi unakuwa na mradi ya nini? Kama ni kwa ajili ya jamii sawa, lakini kama kinachopatika chote unakificha bank umeungua
 
Kwanza niharakishe kutamka hapa kwamba HAKUNA kiumbe yeyote (mwanadamu akiwemo) mbinguni na ardhini awezaye kufufua wafu.Ni Mwenyezi Mungu PEKEE ndiye mwenye uwezo huo wa kuhuisha na kufisha.
Pili;hawa wanaojiita manabii pamoja kwamba hawajatuweka wazi Mungu yupi kawapa unabii,lakini pia hawajatuambia ni Mungu yupi aliyewaambia kila 'nabii' aanzishe kanisa lake na kwa nini utaratibu wa ibada ufanane.
Tatu,Mungu kakataza kujilimbikizia mali,je wao wanapingana na Mungu?
Nne,ukiacha kuhudumu kanisa ambayo ni 'utumishi wa Mungu' kuna shughuli gani HALALI wanazofanya mpaka wanakua matajiri kupindukia?
Maswali haya wanajiuliza wale wenye KUFIKIRI KULIKO KAWAIDA,lakini wale nawapa pole wale WANAOFIKIRI KAWAIDA.

Jamaa leo wananuka hela baada ya ibada za Christmas lakini sijamuona hata mmoja akiwaongoza waumini wake wakatoe sadaka muhimbili ocean road au kwingineko
 
Back
Top Bottom