Nijuavyo ni kampuni ya serikali yenye jukumu la kujenga nyumba zenye gharama nafuu na kuwauzia watumishi wa serikali. Imeanzishwa kama miaka mitatu hivi iliyopita huku wawekezaji katika kampuni hiyo wakiwa ni mifuko ya jamii kama PPF, PSPF, GEPF, NSSF na pia NHC.
Baadhi ya miradi yake ni kama huo wa Magomeni jirani na kituo cha Usalama, nyumba zilizojengwa kule Bunju/Mabwepande jirani na mradi wa nyumba za Tanzania Buildings Agency (TBA) na pia viwanja walivyopewa waathirika wa mafuriko ya miaka kama mitano iliyopita au viwanjwa vilivyokuwa vikiuzwa hivi karibuni na halmashauri ya manispaa ya Kinondoni.