Watu watano muhimu katika maisha yako

Watu watano muhimu katika maisha yako

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,529
Reaction score
21,530
Screenshot_20241111_161531_Google.jpg


Huyu ni mtu ambaye anakusaidia wakati yeye mwenyewe anataka msaada,yani kuna watu ambao wao wenyewe hali zao ni za mashaka lakini bado wana moyo wa kutoa,kama wewe ni mmoja wapo ubarikiwe sana

Mtu ambaye anawapuuza watu wengine kwa ajili yako,yani watu wengine wanampa maneno ya uchochezi au fitina juu yako lakini bado anaziba masikio na bado yupo na wewe,big up sana kwa boss wangu mpya licha ya kwamba boss wangu wa zamani alitia fitina juu yangu,lkn my new boss kwakuwa ananijua vyema ameniamini na tunapambana pamoja

Mtu ambaye anakupa mda kusikiliza shida zako,yupo tayar mda wowote kukusikiliza bila kuchoka,na anatunza siri zako

Mtu ambaye haonyeshi kuchoka kwa tabia zako mbaya,pamoja na tabia zako mbovu lkn yupo pamoja na wewe

Na mtu ambaye anaonyesha dhahiri furaha yake kwako

Namalizia kwa kusema maisha hayakupi mtu mmoja mara mbili

Kwa nyuzi za motivation basi usikose kunisoma,nipo kwa ajili yako


Ni hayo tu!
 
Huyu ni mtu ambaye anakusaidia wakati yeye mwenyewe anataka msaada,yani kuna watu ambao wao wenyewe hali zao ni za mashaka lakini bado wana moyo wa kutoa,kama wewe ni mmoja wapo ubarikiwe sana

Mtu ambaye anawapuuza watu wengine kwa ajili yako,yani watu wengine wanampa maneno ya uchochezi au fitina juu yako lakini bado anaziba masikio na bado yupo na wewe,big up sana kwa boss wangu mpya licha ya kwamba boss wangu wa zamani alitia fitina juu yangu,lkn my new boss kwakuwa ananijua vyema ameniamini na tunapambana pamoja

Mtu ambaye anakupa mda kusikiliza shida zako,yupo tayar mda wowote kukusikiliza bila kuchoka,na anatunza siri zako
Inayapa maisha thamani ukiishi au kukutana na watu kama hawa. Mungu awabariki sana.
 
Back
Top Bottom