Watu wanampenda Magufuli kama Magufuli

Watu wanampenda Magufuli kama Magufuli

mdetichia

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2015
Posts
5,292
Reaction score
2,172
Ndugu wanabodi naomba nimuambie ndugu January Makamba kutokana na kujiaminisha kuwa CCM kwa sasa imeanza kupumua kutokana na utendaji wa Rais Magufuli.

Mimi nikiwa kama mwananchi wa kawaida na muumini wa UKAWA namwambia pasna shaka kuwa huku mitaani watu sio wameanza kuipenda CCM baada kupoteza mvuto la hasha kwa sasa wananchi wanachokiamini na kukikubali ni utendaji wake na Magufuli kama alivyo lakini chama kama chama cha mapinduzi bado sana maana ni kuwa hata hao waliojifanya wana CCM kindaki ndaki wapo wapi leo kumpongeza Rais wetu Magufuli mtu wa watu ?

Hembu tuacheni unafiki utawala uliokuwepo ulikuwa chini ya CCM hata kama walikuwa wakifuata sheria kwanini hawakuyafanya haya anayoyafanya leo Dr Magufuli? UKWELI utabaki kuwa ukweli watu wanampenda Magufuli kama Magufuli na serikali yake atakayoiamini na kuiunda serikali kwanza CCM baadae.
 
Mkuu uzi wako hauna chembe ya unafiki..
Kwa wana CCM, huo ndio ukweli MCHUNGU..!!!
 
leo magufuli akisema anahama ccm na kuunda chama chake atapata kura nyingi sana
 
Mkuu uzi wako hauna chembe ya unafiki..
Kwa wana CCM, huo ndio ukweli MCHUNGU..!!!


Umenena!!! maana tangu ameanza kazi wanachama, wakereketwa na wafurukutwa wote kimya, ni kama wamepigwa bumbuwazi, hawajui jamaa anafikiria nini maana anayoyafanya hakuna hata mmoja wao alipata kufikiria kuyafanya au hata kutabiri kuwa ipo siku yatafanyika, to be honest ni kwamba chama kimenyang'anywa nguo
 
Uko sawa. Mimi nilishawahi kusema sina tatizo na Magufuli, nna tatizo na ccm inayomchukia Magufuli kwa sababu anabana mpaka peneti! Bado tatizo langu ni ccm na sema jamani ccm ndiyo tatizo la nchi hii! Magufuli kwenye kampeni zake hakuwahi kujinadi kiccm bali alijinadi kivyakevyake akijua ccm haipendwi na haitakiwi! Sasa tusubiri tuone iwapo wana ccm watamfunga spped governor au atawaweza ccm?
 
Nafikiri akikabidhiwa na chama , watu watarudisha imani zaidi kwa CCM

Hivyo CCM hawana budi kumtumia vizur kurudisha legacy yao iliyopotezwa na mkwere
 
Ndugu wanabodi naomba nimuambie ndugu January Makamba kutokana na kujiaminisha kuwa CCM kwa sasa imeanza kupumua kutokana na utendaji wa Rais Magufuli.

Mimi nikiwa kama mwananchi wa kawaida na muumini wa UKAWA namwambia pasna shaka kuwa huku mitaani watu sio wameanza kuipenda CCM baada kupoteza mvuto la hasha kwa sasa wananchi wanachokiamini na kukikubali ni utendaji wake na Magufuli kama alivyo lakini chama kama chama cha mapinduzi bado sana maana ni kuwa hata hao waliojifanya wana CCM kindaki ndaki wapo wapi leo kumpongeza Rais wetu Magufuli mtu wa watu ?

Hembu tuacheni unafiki utawala uliokuwepo ulikuwa chini ya CCM hata kama walikuwa wakifuata sheria kwanini hawakuyafanya haya anayoyafanya leo Dr Magufuli? UKWELI utabaki kuwa ukweli watu wanampenda Magufuli kama Magufuli na serikali yake atakayoiamini na kuiunda serikali kwanza CCM baadae.

Baniani mbaya kiatu chake dawa?
 
Uko sawa. Mimi nilishawahi kusema sina tatizo na Magufuli, nna tatizo na ccm inayomchukia Magufuli kwa sababu anabana mpaka peneti! Bado tatizo langu ni ccm na sema jamani ccm ndiyo tatizo la nchi hii! Magufuli kwenye kampeni zake hakuwahi kujinadi kiccm bali alijinadi kivyakevyake akijua ccm haipendwi na haitakiwi! Sasa tusubiri tuone iwapo wana ccm watamfunga spped governor au atawaweza ccm?

Patamu hapo?
 
Tatizo JF haliwi jukwaa la great thinkers tena,baadhi ya wana Jukwaa wanaamini kuwa Jakaya ni dhaifu kuliko ELN,na wengine wanaamini kuwa ELN ni mkweli kuliko Jakaya.Natofautiana nao sana.

Mwenyekiti wa kamati ya ushindi ya Ari mpya,nguvu mpya na kasi mpya alikuwa ELN. Katika timu yao walipima na kupata mchezaji mzuri kuliko wote wakampata JK.

Kama JK ni dhaifu aliyetuuzia mbuzi kwenye gunia ni ELN,kwangu mimi JK kwa manufaa ya nchi kafanya vizuri kuliko mzee wa kuzungusha mikono kwa hoja moja tu. Hakutaka lakini8 kakubali Rais wa Tanzania asipatikane tena kwa fedha za kijanjajanza zinazotoka kwa wahalifu wa ndani naa nje ya nchi ili watukaange kwa mafuta yetu wenyewe.

Ninakiri kuyaona madhaifu mengi ya JK lalini hayafuniki memea yake.Kama angengeng'ang'ania fedha zitumike kupata uongozi JPM asingekuwa alipo.

Ninajua kuwa nguvu iliyotumika kumweka kando Membe ELN alihusika ila wengi mnasahau kuwa ELN angeingia katika tano bora ya CCM ELN ndiye angekalia magogoni leo.

Tumpeni sifa yake Jakaya kuwa fedha za kihuni hazitatuchagulia rais tena.MUNGU wetu alifunika akili za wanadamu na Jakaya akatekeleza,tumempata rais wa hadhi tunayoitaka.

Waganga njaa na fedha za kijanja janja mjini wanalia na kuja na utoto ,ooh JPM hawezi kiingerza,ooh anayofanya hajengi mfumo,ooh hafuati sheria.

Matendo huzungumza kuliko maneno.Anathibitisha nguvu alizozotumia jukwaani kufanya" push up" inathibitika kwa vitendo. MUNGU anaipenda mno Tanzania ndiyo maana alitupa vyote tulivyonavyo hadi majirani wanaona gere tunavyovichezea. Tunaipenda Tanzania,tunampenda JPM. CCM,CDM,CUF vitapita TZ itakuwepo hadi aliyeiumba atakapokuja kuimaliza dunia nzima.

Ni muda wa kujenga TZ,siyo vyama.
 
Umenena!!! maana tangu ameanza kazi wanachama, wakereketwa na wafurukutwa wote kimya, ni kama wamepigwa bumbuwazi, hawajui jamaa anafikiria nini maana anayoyafanya hakuna hata mmoja wao alipata kufikiria kuyafanya au hata kutabiri kuwa ipo siku yatafanyika, to be honest ni kwamba chama kimenyang'anywa nguo

Siyo kweli chama kimenyang'anywa nguo!!! Ukweli ni kwamba CCM imefufuka na inaimalika sasa, baada ya kupata "uongozi bora" moja ya misingi/nguzo kuu ya maendekeo ya nchi, ikiwa ni pamoja na Ardhi, Watu na Siasa Safi. Hivi ndivyo CCM inaamini. Kiongozi Bora ni yule anayetambua na kuthamini "cheo ni dhamana". Rais Magufuli anatekeleza sera na ilani ya CCM kwa vitendo.

TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
Back
Top Bottom