Watu waliosomea hisabati!!

Watu waliosomea hisabati!!

tindikalikali

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2011
Posts
4,854
Reaction score
1,139
Hivi ni kweli kwamba watu waliosoma maths kwa angalau ngazi ya kidato cha 5 na 6 wana uwezo mkubwa wa kufikiri na kuchanganua mambo ukilinganisha na wale waliosoma masomo ya Art kama Kiswahili!?
 
Sio Kweli mbona Lipumba hawezi kuchanganua mambo!!!!?
 
Hivi ni kweli kwamba watu waliosoma maths kwa angalau ngazi ya kidato cha 5 na 6 wana uwezo mkubwa wa kufikiri na kuchanganua mambo ukilinganisha na wale waliosoma masomo ya Art kama Kiswahili!?


Linganisha mburula fisadi Lowasa na Dr.Pombe Magufuli!
 
uwezo wa mtu hutokana na IQ sio craming za elimu duni ya tz
 
Ni kweli kabisa. Vijana waliochukua PCM, PCB hata ukiwapeleka kusoma masomo ya arts, uhasibu ndiyo wanaoongoza. Hesabu ni kitu muhimu sana katika maisha ya binadamu. Kama una mtoto umzuie kusoma HGL;, HKL n.k.
 
Hili halina ubishi. akili ya binadamu hupanuka na kukua pale ambapo binadamu anajifunza mambo mageni na pale anapotumia ufikiri katika kufumbua majibu kwa changamoto zinazomkabili. hatubezi masomo ya arts wala lugha ni masomo muhimu kama yalivyo mengine kinachotofautisha tu ni uwezo wa kukabili masomo lugha unaanza kuionge hata bila kwenda shule lugha mtu akiamua kuibobea hata bila wa kumuelekeza mtu anajua ni ngumu sana mtu asijue matumizi ya lugha hata kijujuu juu ila kuna hesabu tunafundishwa na kuzifahamu bila kujua matumizi yake au madhumuni ya kujifunza ila waliobobea wanakwambia hakuna hesabu ambayo haina matumizi kwa maisha ya hesabu
 
Sio Kweli mbona Lipumba hawezi kuchanganua mambo!!!!?

PCM, PGM, CBM na EGM wanasoma Pure mathematics lakini ECA wanasoma hesabu za kawaida... kwa hvo LIPUMBA hajagusa hesab za advance!!
 
PCM, PGM, CBM na EGM wanasoma Pure mathematics lakini ECA wanasoma hesabu za kawaida... kwa hvo LIPUMBA hajagusa hesab za advance!!

ebooo nyie ndio mnafanya nchi hii iendelee kuwa maskini
 
Basi tuamini kuwa kwa kuwa wazungu wote wamesoma sana hesabu ndo maana wana uwezo mkubwa wa kufikiri
 
Hesabu ndio msingi wa kila kitu, kama ulichelewa jitahidi hata mwanao asichukie hii hazina.
 
unajua kuna mambo mengine ni ujinga sana eti
linakuja swali

x + 20=40 halafu wananiambia nitafute x wakati x naiona

huu ujinga ndio maana hesabu ilinishinda
 
Ni kweli, mbali na kuchanganua mambo hata unapoongea nao na kuwauliza maswali huwa wanatoa majibu kwa haraka sana bila kujali jibu ni sahihi au sio sahihi.
 
ni kweli PCM,PCB, PGM wanapeta sana kwenye maisha hasa kutusua maisha hata kama magumu yanaenda vizuri tu
 
Back
Top Bottom