Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,277
- 105,480
Jambo baya popote linatakiwa kukemewa.Mimi sijasema Dar, ilishanitokea Heathrow, safari ingine uswisi mara kadhaa nikaacha kutumia swissair anyway watanzania tunakatabia ka kipuuzi kukandia vya kwetu
Leo nilikuwa naongea na rafiki yangu Nyani Ngabu , kakosea njia katumia airport mbaya kabisa ya New York ya La Guardia.
Nikamwambia kutumia airport ya La Guardia New York ni bora akapande ndege gerezani kisiwa cha Rikers.
Kwa hiyo sisi raia wa dunia tunasema ujinga tunapouona popote.
Juzi nilikuwa najibizana na Nyani Ngabu huyu huyu, nainanga demokrasia ya Marekani, naonesha mapungufu yake.
Kwa sababu kuna mtu aliiweka juu sana Marekani kama kigezo katika demokrasia.
Kwa hiyo, kwenye kundi la watu wanaoponda vya kwetu tu, simo.
Ila naponda ujinga dunia nzima, sijali kwetu au ugenini.
Na kwa vile wanasema "charity begins at home", nikianzia na kushikia bango nyumbani, hakuna ubaya.
Ndipo makaburi ya wahenga wangu yalipo hapo.