Watoto wa vigogo wamepenyezwa Mizani - Magufuli

babalao 2

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
5,398
3,243
Waziri wa ujenzi mh. Magufuli amebainisha ya kuwa mara nyingi akituma timu zake kufanya ukaguzi katika mizani huwa zinarudi bila majibu mazuri kufuatia kukutana na majina ya watoto wa vigogo na hivyo kutishika.
Alizidi kusema kuwa watoto hao walipenya eneo hilo la mizani kwa kuwa wataweza kula hela za Watanzania kwa rushwa hivyo akatoa agizo wote watakao bainika wafukuzwe hata kama ni 10 kwa siku ili kuwapunguza.
Pia aliwataka watumishi kuwajibika kila mtu kwa nafasi yake na kwa uaminifu. Aliyasema hayo mjini Dodoma.
Habari inapatikana ktk gazeti la habari leo.
Hawa watoto wakijadiliwa watu wengi huona kama wanaonewa kumbe wanapenyezwa au kubebwa tu.
 
Sasa yeye kama Waziri kwanini asichukue hatua ya kuwafukuza kazi badala ya kulalamika!? Yeye mpaka kuweza kulalama ina maana ameona kuna ushahidi wa kutosha kutoa malalamiko yake hadharani? Je amechukua hatua zipi hadi sasa kupambana na hao watoto wa vigogo!?
 
Binafsi namkubali sana huyu Mwana CC! Pengine the system haimpi mamlaka kamili ya kufanya anachostahili pale wzaran
 
Huyu Mh. Waziri naye Mlalamiishi, looh. Kama anaweza kutishia kumfukuza Regional Manager wa Tanroads kule Simiyu kuwa barabara isipokamilika ndani ya siku 30, anashindwaje kuwaondoa hao watoto wa vigogo kama walijipenyeza bila kufuata taratibu za ajira? Aaache porojo afanye kazi. Halafu ndo watu wanampigia chapuo kuwa anafaa kuwa mkulu, m.a.a.v.i!!!
 
Sasa yeye kama Waziri kwanini asichukue hatua ya kuwafukuza kazi badala ya kulalamika!? Yeye mpaka kuweza kulalama ina maana ameona kuna ushahidi wa kutosha kutoa malalamiko yake hadharani? Je amechukua hatua zipi hadi sasa kupambana na hao watoto wa vigogo!?

Mkuu naona kweli ni vichekesho, yeye ndio incharge wa wizara kama anaona hao watu ni tatizo kwanini asichukue hatua? kwani ni lazima wakae mizani hao watoto wa vigogo, na ni nani amewapeleka huko bila idhini ya wakuu wa wizara.
Naona kuna maswali mengi ya kumuuliza Magufuli. Inawezekana kuwa anatafura umaarufu kupitia magazeti. Nadhani kwanza angeanza na kazi ya kuwaadhibu wanaoshindwa kufanya kazi kwa kuwaogopa watoto wa vigogo.
 
Hovyo tu, ndo leo anajua kuna watoto wa vigogo.
cheap popularity anaipenda sana!
anajifanya mjuvi wa kukariri kms za barabara halafu anataka kutuaminisha kuwa watotovigogo ndo amestukia leo!
nyambaf zake!
 
Ama kweli ukitaka kuona watu wanafiki wala usipate shida,nenda nyinyiemu kamata mtawala yeyote,huyu mzee kama ni mpenda haki awataje hao watoto si kuendeleza mipasho kama mwenyekiti wake.
 
Na Masoud Masasi,

Waziri wa Ujenzi Dr John Magufuli amesema watendaji wengi katika mizani ni wala rushwa na hawastahili kuwepo kazini.


Hayo ameyaeleza jana mjini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kabla yakuweka jiwe la msingi la Ofisi ya Wakala wa Ujenzi Tanzania TBA.


Amesema watumishi hao wala rushwa ni watoto wa vigogo ambao hutumia simu kuwasiliana na wasafirishaji wa mizigo kabla ya gari husika kufika katika mizani na kuruhusiwa.


kutokana na hali hiyo amesema hivi sasa watendaji katika maeneo ya mizani hawaruhusiwi kuwa na simu na yeyote atakayebainika kuwa na simu kazini atafukuzwa kazi.


Aidha ametoa maagizo kwa wakala wa Barabara nchini TANROADS kutangaza hadharani pale wanapotaka kupata watumishi wa wakala huo wakiwemo wa mizani nia ya kufanya hivyo ni kupata watumishi wenye sifa na ambao wanaweza kuchukuliwa hatua kikamilifu kulingana na taratibu.


Dr Maghufuli amesema Kutokana na hali hiyo ya rushwa barabara nyingi zimekuwa zikiharibika kutokana na uzito wa mizigo inayopitishwa huku watu katika mizani wakiwepo.


Amewataka mameneja wa TANROADS wa Mikoa kuendelea kufukuza watendaji wala rushwa katika mizani hiyo siku hadi siku ili kupunguza tatizo la rushwa lililopo.


Aidha ameziomba kamati za ulinzi na usalama za mikoa kusaidia katika kuwafuatilia watumishi hao wa mizani kwani hata wakitumwa watu toka Ofisi za wakala kwenda kuwafuatilia wanashindwa kuwakamata kwa kuwa wao wanakuwa sehemu ya hao wala rushwa.
 
Sasa ANGALIA WALIVYOPANDIKIZA WATOTO WAO; Kweli Unadhani wataachia MADARAKA kiurahisi ?
Hakuna TUME HURU; Itabidi wawaalike EUROPEAN OBSERVERS; Or JIMMY CARTER a CARTER CENTER pia wanaangalia CHAGUZI za NCHI wakialikwa... Hii itakata MIRIJA Mingi ya VIFISADI UCHWARA...

 
Huyu nae akalale tu , hivi hawa mawaziri njaa wametoka wapi?Je anajua athari zake?Mara nyingi kwenye sheria wanashindwa wanaishia kulipa fidia.
 
Huyu nae akalale tu , hivi hawa mawaziri njaa wametoka wapi?Je anajua athari zake?Mara nyingi kwenye sheria wanashindwa wanaishia kulipa fidia.

Mkuu athari gani tena kwa kuwafukuza wala rushwa? Maana ya wala rushwa ni wale waliokamatwa au kudhibitika kufanya maamuzi yao bila kufuata utaratibu wa kazi.

Ni bahati mbaya watanzania nasi tunashirikiana na hawa watu waroho kuhujumu nchi yetu. Rushwa ya laki 9 inawafanya waruhusu gari linalopita na mzigo mkubwa na kuharibu barabara zetu njia nzima linakopita na kutugharimu mamilioni au mabilion kuzikarabati.

Nakumbuka nilikuwa kwenye basi tukafika mizani wakasema jamani sogea mbele, niliongoza abiria kugomea kitendo kile na nilikumbana na upinzani mkali sana japo tulifanikiwa na gari lilipigwa faini. Wengi wetu hatuelewi ni kwa kiwango gani uzembe huu unaligharimu taifa!


 
Anatwambia siye tufanyehe sasa? Jamaa kazoea kujipatia umaarufu tu kwenye vyombo vya habari, nilisha ona hamna kitu hapo tokea abomoe kituo cha mafuta kwa lazima kule Mwanza alafu yule mmiliki wa kile kituo akaja kulipwa mamilioni na serikali kama fidia.Jamaa ni mchemfu sana huyu watu hawajamjua tu
 
Mkuu athari gani tena kwa kuwafukuza wala rushwa? Maana ya wala rushwa ni wale waliokamatwa au kudhibitika kufanya maamuzi yao bila kufuata utaratibu wa kazi.

Ni bahati mbaya watanzania nasi tunashirikiana na hawa watu waroho kuhujumu nchi yetu. Rushwa ya laki 9 inawafanya waruhusu gari linalopita na mzigo mkubwa na kuharibu barabara zetu njia nzima linakopita na kutugharimu mamilioni au mabilion kuzikarabati.

Nakumbuka nilikuwa kwenye basi tukafika mizani wakasema jamani sogea mbele, niliongoza abiria kugomea kitendo kile na nilikumbana na upinzani mkali sana japo tulifanikiwa na gari lilipigwa faini. Wengi wetu hatuelewi ni kwa kiwango gani uzembe huu unaligharimu taifa!



Unajua mara nyingi huwafukuza kwa dhana kwa hiyo linapofikishwa kwenye sheria wanakwama.Kwanza aina ya mashahidi pia kutokuwa makini ktk kesi husika hupelekea serikali kulipa fidia au kuwarudisha kazi.Tatizo sio kuwafukuza bali wajipange namna ya kupata ufumbuzi juu ya hilo.
 
kiongozi inabidi ufanye kazi yako kwa mujibu wa sheria kwahiyo basi wala rushwa

1. inakubidi uwapeleke mahakamani na sio kulalamika huo ndio tunaita usanii

2.sheria gani ya nchi inayosema mfanyakazi afukuzwe kazi eti anamiliki cell phone??

3. kuwa mtoto wa kigogo is not an excuse km kakosea sheria inabidi zifuatwe na siyo kulalamika kwy gazeti.

4. kama wanapokea rushwa wawekee mtego kupitia madereva hao hao wa malori na uwakamate otherwise

unatulalamikia sisi tukusaidie nini sana sana tutakuona unajitafutia cheap popularity tu.
 
Sasa yeye kama Waziri kwanini asichukue hatua ya kuwafukuza kazi badala ya kulalamika!? Yeye mpaka kuweza kulalama ina maana ameona kuna ushahidi wa kutosha kutoa malalamiko yake hadharani? Je amechukua hatua zipi hadi sasa kupambana na hao watoto wa vigogo!?

Achukue hatua! Magufuli hawezi kuchukua hatua, atabaki kulalamika, ndio mfumo wao. Si unamsikia hata mheshimiwa Mkuu mwenyewe kwenye maslahi ya nchi badala ya kuchukua hatua ye analalamika! Hii ni serikali dhaifu, usitegemee zaidi
 
Sasa yeye kama Waziri kwanini asichukue hatua ya kuwafukuza kazi badala ya kulalamika!? Yeye mpaka kuweza kulalama ina maana ameona kuna ushahidi wa kutosha kutoa malalamiko yake hadharani? Je amechukua hatua zipi hadi sasa kupambana na hao watoto wa vigogo!?

Moja ya vifungu vya kanuni za Sheria ya Barabara ya 2007 zinaipa madaraka TANROAD kuyaondoa barabarani magari yanayoharibika. Lakini cha kushangaza siku hizi barabara zetu zimegeuzwa gereji na malori mitumba ya vigogo. Jana asbuhi lori moja liliharibika enep la Kimara kwenye diversion na kusababisha foleni kubwa sana. Jioni lingine likaharibika Mbezi Mwisho na kusababisha foleni ya kufa mtu. Kama kashindwa kuondoa malori mabovu barabarani atawaweza watoto wa vigogo?

hata yeye ni mmpja wa wanufaika wa hii rotten system
 
Magufuli mnafiki sana, kama kweli ana nia awatimue ndo atutangazie.
Haya maneno yake yamegubikwa na uoga.
Mtu muoga ni muongo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom