Watoto shule za msingi

Watoto shule za msingi

Viva89

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2012
Posts
1,262
Reaction score
530
Huwa inanisikitisha saana nikiwa natoka nyumbani asubuhi mida ya 5.30 - 6am na kuona wanafunzi wa primary school,mmoja mmoja anatembea kwenda shule.

Hapo bado kuna giza fulani na yupo peke yake, na wengi niwaonao nadhani hawajapita miaka 12. Ni hatari sana kwa watoto hao kutembea mida hiyo peke yao,yani hata mtu wa kumsindikiza hata kituo cha basi na kusubiri apande hayupo!..alafu baada ya mda mzazi anaenda kuripoti polisi mtoto amepotea.

Jamani ambao hauna/hatuna watoto tufanye kazi kwa bidii, tusave hela baadae watoto wetu wasitembee kwenye giza peke yao, ni hatari sana na wazazi naombeni waangalieni hao watoto wenu kwa makini,dangerous times we live in.
 
Its true!!!!!!!!!!! watoto wanawahi sana darasani kisa mkakati wa la saba. wanaingia darasani mapema sana na wanachelewa kutoka, Watoto wengine wanaishi mbali na shule na hii inawasababishia usumbufu mkubwa. Ni vizuri hili swala likaangaliwa kwa undani zaidi. Hii nchi sii salama sana
 
Huwa inanisikitisha saana nikiwa natoka nyumbani asubuhi mida ya 5.30 - 6am na kuona wanafunzi wa primary school,mmoja mmoja anatembea kwenda shule.

Hapo bado kuna giza fulani na yupo peke yake, na wengi niwaonao nadhani hawajapita miaka 12. Ni hatari sana kwa watoto hao kutembea mida hiyo peke yao,yani hata mtu wa kumsindikiza hata kituo cha basi na kusubiri apande hayupo!..alafu baada ya mda mzazi anaenda kuripoti polisi mtoto amepotea.

Jamani ambao hauna/hatuna watoto tufanye kazi kwa bidii, tusave hela baadae watoto wetu wasitembee kwenye giza peke yao, ni hatari sana na wazazi naombeni waangalieni hao watoto wenu kwa makini,dangerous times we live in.
Watanzania tunaongozwa na matukio. Mpaka litakapotokea la kutokea la mtoto wa kike kubakwa na kuuwawa ndo watu watastuka! That's how we are, so sorry to say this!
 
Back
Top Bottom