Mbaneingoma Zom
JF-Expert Member
- Feb 23, 2011
- 201
- 14
Wana JF mimi ni mmoja wa wanJF lakini pia ni mfuatiliaji sana wa habari za siasa hasa siasa za upinzani na zaidi sana habari za chadema!! Kwanza ningependa kuwajuza kuwa mimi ni Mwanachama na sio mwanachama tu bali mwanachama mkereketwa na pia ni Kiongozi kwa ngazi ya tawi. Sababu ya kushuka jamvini leo ni kutaka kuuliza kuhusu kitengo cha mawasiliano ya chama chetu. Kama mjuavyo kuwa habari ni jambo la msingi sana katika kuleta mabadiliko yoyote katika jambo lolote na katika nchi yoyote. kupashana habari ni kitu muhimu sana. Na pale inapobidi picha huwa ni moja ya vielelezo muhimu sana kumjuza mtu kuhusu jambo fulani. Sasa kinacho nifanya nije humu ni kwamba habari za chadema hasa kwa kipindi hiki cha ziara ya chama mikoa ya nyanda za juu kusini zimekuwa adimu sana na zinapokuwepo ni kwa kifupi sana na bila vielelezo(picha) sasa mimi najiuliza,tatizo ni coverage ya internet kwenye maeneo yanayotembelewa au vifaa vya kuchukulia picha vinakosekana? au ni nini? kwani siku Mkienda kule Mh. Regia alitupa picha ambazo alisema zilikuwa ni picha za awali tu! tulishukuru sana kwani tulihisi kama na sisi tuko kule!! lakini tangu zile picha zitumwe hakuna picha zingine zilizotumwa ingawa msafara umesikika ukiwa unatoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine. Tulitarajia tungekwenda pamoja hatua kwa hatua lakini haikuwa hivyo!! Je tatizo ni nini? au kuna gharama sana kufanya hivy?(kutuma picha)
Naomba wahusika watujuze nina hakika kuwa si mimi tu mwenye dukuduku hilo.
Nawasilisha
Naomba wahusika watujuze nina hakika kuwa si mimi tu mwenye dukuduku hilo.
Nawasilisha