Watendaji wa kitengo cha habari cha chadema mko wapi?

Mbaneingoma Zom

JF-Expert Member
Feb 23, 2011
201
14
Wana JF mimi ni mmoja wa wanJF lakini pia ni mfuatiliaji sana wa habari za siasa hasa siasa za upinzani na zaidi sana habari za chadema!! Kwanza ningependa kuwajuza kuwa mimi ni Mwanachama na sio mwanachama tu bali mwanachama mkereketwa na pia ni Kiongozi kwa ngazi ya tawi. Sababu ya kushuka jamvini leo ni kutaka kuuliza kuhusu kitengo cha mawasiliano ya chama chetu. Kama mjuavyo kuwa habari ni jambo la msingi sana katika kuleta mabadiliko yoyote katika jambo lolote na katika nchi yoyote. kupashana habari ni kitu muhimu sana. Na pale inapobidi picha huwa ni moja ya vielelezo muhimu sana kumjuza mtu kuhusu jambo fulani. Sasa kinacho nifanya nije humu ni kwamba habari za chadema hasa kwa kipindi hiki cha ziara ya chama mikoa ya nyanda za juu kusini zimekuwa adimu sana na zinapokuwepo ni kwa kifupi sana na bila vielelezo(picha) sasa mimi najiuliza,tatizo ni coverage ya internet kwenye maeneo yanayotembelewa au vifaa vya kuchukulia picha vinakosekana? au ni nini? kwani siku Mkienda kule Mh. Regia alitupa picha ambazo alisema zilikuwa ni picha za awali tu! tulishukuru sana kwani tulihisi kama na sisi tuko kule!! lakini tangu zile picha zitumwe hakuna picha zingine zilizotumwa ingawa msafara umesikika ukiwa unatoka sehemu moja na kwenda sehemu nyingine. Tulitarajia tungekwenda pamoja hatua kwa hatua lakini haikuwa hivyo!! Je tatizo ni nini? au kuna gharama sana kufanya hivy?(kutuma picha)
Naomba wahusika watujuze nina hakika kuwa si mimi tu mwenye dukuduku hilo.

Nawasilisha
 
Naomba wnaohusika ikiwa yupo hata mmoja atujulishe kuhusu hili ambalo mimi nimeliuliza! au hakuna hata mtu mmja aliye online ambaye ni muhusika? au kuna nini jamani naomba kusaidiwa!
 
idara ya habari na uenezi kapewa mtu kilaza sana anaitw Tumbo, pia jamaa amewekwa tu ili apate chochote kinywani hahahahahaaaaaa, ila jamani cdm haina mfumo wa maana sana kwenye uendaji, zaidi sana wanamwachia slaa ahangaike tu ila na yeye ni mzee kachoka na anawaza urais 2015, ndio maana mnyika likuwa anafanya issue za uenezi wakati tumbo yupo.

kwa hili cdm walekebishe kabisaa basi wampe hata heche anayependa kuuza sura na kusema kila jambo, hiki kiherehere chake kitasaidia ila sio awe mwenyekti bavicha...nooooooooooooo
 
idara ya habari na uenezi kapewa mtu kilaza sana anaitw Tumbo, pia jamaa amewekwa tu ili apate chochote kinywani hahahahahaaaaaa, ila jamani cdm haina mfumo wa maana sana kwenye uendaji, zaidi sana wanamwachia slaa ahangaike tu ila na yeye ni mzee kachoka na anawaza urais 2015, ndio maana mnyika likuwa anafanya issue za uenezi wakati tumbo yupo.

kwa hili cdm walekebishe kabisaa basi wampe hata heche anayependa kuuza sura na kusema kila jambo, hiki kiherehere chake kitasaidia ila sio awe mwenyekti bavicha...nooooooooooooo
mbwazoba wewe ndio kilaza namba moja umetumwa na chama cha magamba kuchafua watu lakini umechemka, vipi heche amekuchukulia mke? mbona unaonesha chuki za wazi kwake? inaonekana anakutisha sana, record yake inatosha,
 
mbwazoba wewe ndio kilaza namba moja umetumwa na chama cha magamba kuchafua watu lakini umechemka, vipi heche amekuchukulia mke? mbona unaonesha chuki za wazi kwake? inaonekana anakutisha sana, record yake inatosha,
Jamani cha msingi hapa ni mimi na wanaharakati wengine kupata ufafanuzi juu ya kitengo cha habari cha chadema na sio matusi kwa hiyo naomba kama wanaohusika wapo watupe ufafanuzi juu ya hili!! au hakipo na kama hakipo chama kina mpango gani wa kukiweka kitengo kama hicho? Kwa sababu kama nilivyosema kwenye utangulizi wa mada hii ni vizuri chama kikawa ni mikakati ya makusudi kabisa kushera information na jamii yote siyo tu jamii fulani kwa wakati fulani. Sisemi kwamba hakuna kabisa habari kuhusu kinaxho endelea sasa nyanda za juu kusini ila habari zinakuwa hazima muendelezo wa kuaminika nafikiri ninaposema muendelezo naeleweka. mfano uliwaambia watu tutaendelea kufahamishana juu ya mkutano fulani watu watakaa wakisubiri muendelezo lakini kunaweza kuona siku ikapita bila habari zaidi! Sasa hili di jema sana. Na hata kama chama kilikutana na changamoto fulani za kutokukubalika ni vizuri wananchi wakajulishwa ili waweze kkishakuri chama kupata mwelekeo mpya na sio kuficha kwani waswahili husema mficha maradhi kilio humfichua!! Tusiwe kama hawa wenye mangamba mambo yao mengi ni siri na hufikiri wanajenga lakini kumbe wanabomoa kwani unapo ujulisha umma kuhusu jambo jema linalotokea unaupa umma huo nafasi ya kujikpongeza kwa mafanikio! na unapouhabarisha umma kuhusu suala baya linalotokea unaupa umma huo nafasi na kufikiria jinsi ya kuboresha na kusonga mbele! Naomba nijulishwe seriously msinipuuze kwani mimi nawakilisha mawazo ya wanachadema wengi wanofeel the same way!
 
Jamani watendaji wa idara ya habari chadema mko mbali na mawasiliano mbona hili hamlitolei ufafa nuzi au ni kupuuza? labda hampo mahali palipo na internet access kwa sasa? mbona hili linaonyesha udhaifu jamani!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom