Watatu kwa kuombaomba, wa 5 afrika kwa rushwa, wa mwisho kukusanya kodi-hii ndo tanzania

luckman

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,211
371
Nafikiri ni muda muafaka wa kutafakari haya na kuhoji utaifa na manufaa ya kuitwa mtanzania, ni wakati sahihi wa kukataa haya kwa vitendo, tanzania nchi iliyosifika kwa kila kitu sasa imekuwa kinuyume cha hayo na kuwa kijiwe cha wanyanganyi na walanguzi wa nchi.

Napatwa na hasira ninaposoma ripoti mbalimbali na kuona eti sisi ni watano barani afrika kwa rushwa, sisi ni wa 3 kwa kuombaomba hali hatuna vita, hatuna ukame, sema tuna mali kila kona ya nchi, eti sisi ni mwisho kwa kukusanya kodi, hii inasikitisha sana na nakaa na hoji umuhim wa hawa wanaojiita wabunge, hivi kazi yao nini kama kuisimamia serikali wameshindwa, ona posho sasa wanajilipa 28b pa ka posho tu, napatwa na mshtuko, namwangalia mwalimu, polisi ambao kiwastan mishahara yao ni 150,000/ hali mbunge anapata marambili ya hiyo pesa kwa masaa ndani ya siku moja, hii ni chuki ya namna gani inapandikizwa ndani ya vichwa vya watanzania, ni uzalendo gani unajengwa?

Sidhani ka bunge ni sehem ya kujilipa na kuamua wafanye nini na pesa zetu, eti gharama zimepanda, nani asiyejua mfumuko wa bei ni zaidi ya 20% ila kisiasa nalipotiwa 17.9%? je ongezeko hili serikali imefanya nini ili kuwasaidiwa watumishi wake wanacover vipi hii gape??mwanachi mnamjali wakati wa kuomba kura???ipo siku NASEMA IPO SIKU, HAYA YOTE MTAYALIPIA, USANII MNAOFANYA KUKUSANYA KODI, KULINDANA KWA WALA RUSHWA, ITAWAKOST, I AM TELLING YOU. kaa tumefika hatua katibu wa bunge na speaker hawaongei lugha moja hii si hatari??? tunajivunia nini sisi ka watanzania na madini yetu, na bahari yetu, na maziwa yetu, na mbuga zetu, na milima yetu, na makumbusho yetu, haya yote tunakusanya eti billioni mara 480, mara 670? kweli?

Nina uhakika kama tungekuwa makini na kazi tunayoifanya, tukaweka ubinfsi pembeni na kudumisha utaifa aliotuachia mwalimu, elimu, afya, cement na mabo mengine yangekuwa kwa bei ya chini sana, kodi tungeweza kukusanya hata 3b per month! only 1.5 ndo wanalipa kodi alafu leo rais anasema wanachi wamsaidie kuwafichua wakwepa kodi hivi serikali haiwajui wakwepa kodi???mbona usanii ni mwingi? mkapa alijitahidi akakakusanya hadi 400b per month iweje leo for the pats 6 years tumekwama, tunajikwaa wapi? tuna haja ya kukopa for recurrent expenditure??sisi tunakopa kwa ajii ya matumizi ya ndani na si miradi ya maendeleo???

chadema,wanaharakati wa kweli, nccr y kweli, cuf ya kweli na wengine wenye majukwaa mbalimbali please call for action on this, it is very serious kuona mnayo majukwaa na mnakaa kimya, hii si issue ya kuangalia, mnapeana mishahara minono huku watu hata 500 hawapati a day!mnalea watnzania wenye akil na mtazamo wa namna gani???

nasikitika sana juu ya haya yanayotokea tanzania chini ya kikwete
mwananchi wa kawaida
mwenye kilio na majonzi yasioisha hadi niione tanzania niitakayo
luckman-true we created rich sema wachafuzi wamehanisi nchi yetu
 
umenigusa sana juu ya mazingaombwe yanayofanywa na watawala, tungefika mbali ka tungepata viongozi lakini ka ulivosema naamini ipo siku watayajutia haya!
 
ha ha ha dogo punguza jaziba, hapa TZ ukiwa na jaziba utakufa na presha,hata useme nini na ufanye nini huwezi kupandisha maji mlima Kilimanjaro mpaka kileleni kwa gravity
 
ndo Tanganyika yetu hii mkuu,nani wakumfunga paka kengele? hali ya uchumi ni mbaya,mfumko wa bei upo juu kwa wabunge tu.....ama kweli magamba wameamua!
 
mzee usikute wakishasoma hii maneno wanaginganisha glasi zao za mvinyo, halafu maisha yanaendelea tena kwa kunenua hadi magego yao ya mwisho. we acha tuu!
 
mzee usikute wakishasoma hii maneno wanaginganisha glasi zao za mvinyo, halafu maisha yanaendelea tena kwa kunenua hadi magego yao ya mwisho. we acha tuu!

wagnganishe glass sana lakini wajue kila lenye mwanzo lina mwisho, kama ujuavyo aliyezaliwa atakufa na hiyo ndo alama sahihi ya kila kitu kina mwisho,
 
NATAFAKARI PAMAOJA NA MATATIZO HAYO YOTE LEO NASIKIA ETI WABUNGE JUST A DAY
SEATING ALLOWANCE 200,000.00
P/D 80,000.00
POSHO YA GARI 50,000.00
TOTAL 330,000.00 huu ni mshahara wa mwalimu kwa siku sitini lakin mbunge anaupata kwa masaa ya 3-7=4 +11-1=2
total is 6hrs only

sijui na sielewi mwisho wa hili bifu na gap linalopepewa na wabunge!
tukidai katiba wanaiteka hoja nzima, tukisema tuweke vigezo vinavyokidhi haja hadi mtu kufikia hatua kugombea ubunge, watu hoja na mawazo ya kuendesha nchi hawana instead wanajadili posho tu
 
Back
Top Bottom